Kabla ya kuanza kudai Tume Huru ya uchaguzi au kuvunja tume iliyopo tafadhali tusaidieni kujibu maswali haya

CalvinKimaro

JF-Expert Member
Sep 11, 2017
244
312
KABLA HUJAANZA KUDAI TUME HURU AU KUVUNJA TUME ILIYOPO TAFADHALI TUSAIDIENI KUJIBU MASWALI HAYA. UKIKOSA MAJIBU YAKE BASI UTAKUWA HUNA TOFAUTI NA JAMAA WA TIGRIS AND EUPHRATES WALIORUHUSU MGENI KUJENGA KWENYE KIHAMBA CHA UKOO.

Disclaimer: huenda kweli tunahitaji tume "nyingine". Nasema "huenda" na natumia neno "nyingine". Nasema 'huenda' kwa kuwa sijathibitishiwa umuhimu wa kubadili iliyopo. Nasema 'nyingine' maana sijasikia kwa kina ni vipi "Uhuru" wa hiyo tume "huru" utakuwa tofauti na uhuru wa tume iliyopo. Huenda majibu yatanibadilisha mwelekeo?

1. Wajumbe watapatikanaje?

2. Nani atawateua?

3. Watawajibika kwa nani ambaye atakuwa huru utakavyo?

4. Nini kilifanya iliyoitwa tume huru kule Zanzibar ife? Walikosea wapi?

5. Unadhani kuna mtanzania ambaye hana chama au mapenzi na chama au mapenzi na mtu? Kama hakuna tume huru itapatikanaje?

6. Unapendekeza taasisi gani zinafaa kutoa wajumbe wa tume ili iwe huru? Taasisi hizo ni huru?

7. Je, kwa nini Kenya ambayo inasifiwa kuwa na tume huru bado walioshindwa hawaridhiki?

8. Je, unadhani hivi vyama vya upinzani vina watu wenye sifa ya kuwa wajumbe wa tume? Toa sababu na walau wataje mtu mmoja kila chama anayefaa kuwa mjumbe wa hiyo tume huru? Kwa yeye kuwa chama cha siasa sio kwamba tayari si mtu huru?

9. Ikitokea wajumbe wa tume wamehitilafiana kama ilivyokuwa Zanzibar Serikali ifanye nini kuepusha nchi isiingie kwenye machafuko?

10. Je, ili tume iwe huru na yenye ufanisi wajumbe wawe wangapi? Wanawake wawe %ngapi? Je makabila na dini yawakilishwe kwenye tume? Ikitokea tume ina wanaume au wanawake tupu, waislamu tupu au wakristo tupu au asilimia kubwa itafaa? Nini kifanyike ili isitokee time ina maaskofu au mashehe tupu au kwa wingi kama kwenye dua au maombi?

11. Utaratibu wa sasa wa tume uendelee? Uwepo wake Una hasara au faida? Yaani hata kama Una hasara lakini faida ikiwa kubwa tuendelee nao au tuachane nao?

12. Je nchi hizi za kiafrika hata tume ingeundwa na malaika na mitume kuna desturi ya kukubali matokeo? Naomba ututajie walau watu 10 tu watanzania ambao unadhani wanaweza kuunda tume huru na kukubalika walau na 70% ya watanzania?

ONYO: Tusipoyajibu maswali haya bila muku, mihemko, migebuka, mbeke au uchama itakuwa hatari kukurupuka na kubadili tume iliyopo. Mihemko aina hii ndio inawakumba Iraq sasa! Kuruhusu mgeni ajenge kwenye kihamba cha ukoo!
 
Habari ya tume huru ni choko choko tu. Hata wangepewa maraika tume bado wapinzani wata lalamika tu.
Mi ninavyojua tatizo cyo tume . Bali tatizo ni vyama vya siasa.
Tanzania na africa kwa ujumla hatuna vyama vya siasa bali tuna magenge na vikundi vya watu vilivyoanzisha vyama kwa lengo la kujipatia rudhuku. Ndo maana wao kila kitu ni kupinga ndo maana wakaitwa wapinzani.
Chama cha siasa cyo kupinga kilakitu, cyo kuhamasisha vurugu, cyo kugombana na serikari!
Chama cha siasa nikuleta siasa mpya mawazo mapya sera mpya mbinu na mawazo mbadara ya kuleta maendereo ambayo mwenzio hana.
Hivyo hawa wanaodai tume huru cjui katiba mpya wawe kwanza nahaya niliyoyasema km vyama vyasiasa harafu ndo lije takwa la wananchi wote kudai katiba na tume kama itaonekana vilivyopo vina mapungufu.
 
Una maanisha hata Tanzania sio huru maana bado tunaishi kwa misaada ya wazungu tulio wafukuza. Tume huru isiyo na mtu ambae kateuliwa na Rais, watu wa tume huru waombe kazi kama ilivyo kwenye taasisi nyingine na si kuteuliwa, taratibu za kutangazwa mshindi zitangazwe na mtu kutoka tume huru hata kama atakula rushwa na kutangaza uongo itakuwa heri kuliko kuwa na tume ya rais na wakurugenzi walioteuliwa na rais na wanaambiwa kabisa ukitangaza mpinzani hutakuwa na kazi. Hii ni dhuluma kubwa sana.

Hizo zilizokufa huko Zanzibar chanzo ni CCM BARA, maana haitaki kuona Zanzibar inatawaliwa na cham kingine, tume ya Zanzibar ilikuwa mbioni kumtangaza maalim 1995 bara wakaingilia wakasababisha machafuko, 2015 ccm walikaa kikao wakamuamuru Jecha afute uchaguzi., so kufa kwa tume ya Zanzibar chanzo ni CCM ndio maana mkapa ameomba msamaha kwa mauaji ya 1995 na kukiri anatamani tume huru anajua udhalimu alioufanya, 2015 alilazimisha mkurugenzi wa jiji la Mwanza amtangaze Mabula na sio Wenje mpaka kumzaba kibao Wenje maana alikuwa na ushahidi wa ushindi. Hakuna mahali pako 100%. Vipi kwenye taasisi nyingine rais ndio angekuwa anachagua waajiriwa nchi ingekuwa na usalama hata huu fake uliopo?
 
wajumbe wa tume wakike kwenye vyama vyote vya upinzani, kila chama kipendekeze watu wake.
 
Ya kwamba mleta mada hujui umuhimu wa tume huru? Kuwa hujui wajumbe watapatikana vipi? Ya kuwa pia hujui watawajibika kwa nani? Na mengi mengine mbona ni vichekesho. Labda kama slow slow ndiye kakutuma kuleta huu Uzi.

Waswahili wanasema asiyejua kufa, asiyejua maana, asiye na macho na asiye asiye kadhaa utamalizia mwenyewe semi hizo.

Kama CCM hawaoni taabu na tume isiyo huru iliyosimikwa na wao, nadhani wawape nafasi wapinzani wasimike tume ili 2020 CCM watakaposhinda na tume si yao wawe wameonyesha pasi na shaka tume huru si suala la msingi.

Ama ukweli mwenye shibe hajui kama na wenye njaa wapo.
 
Ya kwamba mleta mada hujui umuhimu wa tume huru? Kuwa hujui wajumbe watapatikana vipi? Ya kuwa pia hujui watawajibika kwa nani? Na mengi mengine mbona ni vichekesho. Labda kama slow slow ndiye kakutuma kuleta huu Uzi.

Waswahili wanasema asiyejua kufa, asiyejua maana, asiye na macho na asiye asiye kadhaa utamalizia mwenyewe semi hizo.

Kama CCM hawaoni taabu na tume isiyo huru iliyosimikwa na wao, nadhani wawape nafasi wapinzani wasimike tume ili 2020 CCM watakaposhinda na tume si yao waweza wameonyesha pasi na shaka tume huru si suala la msingi.

Ama ukweli mwenye shibe hajui kama na wenye njaa wapo.
Ingekuwa vema kama ungejibu maswali ya mleta mada. Maswali aliyouliza ni ya msingi sana maana tunaweza tukadhani tatizo ni tume kumbe tatizo ni kitu kingine.
 
Tume huru itaruhusu kutangazwa kwa matokeo ya kura za urais vituoni, wananchi watajumlisha wenyewe na kukubali matokeo au kupinga mahakamani.
 
Ya kwamba mleta mada hujui umuhimu wa tume huru? Kuwa hujui wajumbe watapatikana vipi? Ya kuwa pia hujui watawajibika kwa nani? Na mengi mengine mbona ni vichekesho. Labda kama slow slow ndiye kakutuma kuleta huu Uzi.

Waswahili wanasema asiyejua kufa, asiyejua maana, asiye na macho na asiye asiye kadhaa utamalizia mwenyewe semi hizo.

Kama CCM hawaoni taabu na tume isiyo huru iliyosimikwa na wao, nadhani wawape nafasi wapinzani wasimike tume ili 2020 CCM watakaposhinda na tume si yao waweza wameonyesha pasi na shaka tume huru si suala la msingi.

Ama ukweli mwenye shibe hajui kama na wenye njaa wapo.

Hiyo tume huru itatoka mbinguni?
 
wajumbe wa tume wakike kwenye vyama vyote vya upinzani, kila chama kipendekeze watu wake.

Hao wajumbe wa vyama hawatapendelea vyama vyao? Kuuza vyama vyao na hapo itabaki kuwa tume huru au ni tume ya vyama vya siasa?
 
..CCM na wapinzani wawe wanapokezana kuteua mwenyekiti na wajumbe wa tume ya uchaguzi.

..kwa mfano, 2015 to 2020 tume iliteuliwa na CCM. Basi kwa kipindi cha 2020 to 2025 tume iteuliwe na wapinzani.
 
Ulivyoandika 'MARAIKA' badala ya MALAIKA nmeshajua wewe ni mtu wa aina gani
Habari ya tume huru ni choko choko tu. Hata wangepewa maraika tume bado wapinzani wata lalamika tu.
Mi ninavyojua tatizo cyo tume . Bali tatizo ni vyama vya siasa.
Tanzania na africa kwa ujumla hatuna vyama vya siasa bali tuna magenge na vikundi vya watu vilivyoanzisha vyama kwa lengo la kujipatia rudhuku. Ndo maana wao kila kitu ni kupinga ndo maana wakaitwa wapinzani.
Chama cha siasa cyo kupinga kilakitu, cyo kuhamasisha vurugu, cyo kugombana na serikari!
Chama cha siasa nikuleta siasa mpya mawazo mapya sera mpya mbinu na mawazo mbadara ya kuleta maendereo ambayo mwenzio hana.
Hivyo hawa wanaodai tume huru cjui katiba mpya wawe kwanza nahaya niliyoyasema km vyama vyasiasa harafu ndo lije takwa la wananchi wote kudai katiba na tume kama itaonekana vilivyopo vina mapungufu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ingekuwa vema kama ungejibu maswali ya mleta mada. Maswali aliyouliza ni ya msingi sana maana tunaweza tukadhani tatizo ni tume kumbe tatizo ni kitu kingine.

Mkuu hoja zote alizotoa zimejibiwa tena kimahesabu (by contrapositive) pasi na kuacha shaka yoyote.

Msumari wa mwisho uko hapa: "CCM ajaribu uchaguzi wakati tume si yake. Akishinda, basi uchaguzi bila ya tume huru kwa yeyote si suala."

"Ya nini kuandikia mate hali wino upo?"
 
Tume huru ni kiswahili tu,kwani wajumbe wanateuliwa na binadamu awe Raisi,au Bunge au Jaji.
Kitu muhimu ni wajumbe wa tume kufanya kazi bila kuingiliwa au kupendelea upande wowote.Lakini wawajibishwe na Jumuiya ya Madola ikibidi.
 
MTU mzima akikuuliza kuna ulazima gani kujenga choo mbona ng'ombe na mbuzi hawana na maisha yanaenda na wako comfortable unajua ni mtu was aina gani.
Mleta mada anapouliza swali hili LA Tume katika dunia ya sasa anatofauti gani na huyo anaye uliza kuhusu kujenga choo?
 
Back
Top Bottom