Kabla ya kua mabilionea walifanya kazi hizi

Chaos Master

JF-Expert Member
Jul 7, 2021
636
1,304
Inaelezwa kila mtu anazaliwa tajiri lakini pia masikini. Utajiri au umasikini wake unategemea na mazingira anayokulia, lakini inategemea zaidi na yeye mwenyewe. Wapo matajiri wengi duniani ambaohawakuzaliwa matajiri. Walitengeneza utajiri wao kwa kupitia maisha ya kawaida kabisa ambayo kila mtu ama wengi wa watu wanayaishi.

Kwa mujibu wa Forbes wapo mabilionea zaidi ya 2,700 duniani lakini wengi wao walianza kufanya kazi za kawaida kabisa ambazo usingedhani kama wangeweza kuwa mabilionea.

Mabilionea kama Elon Musk, Jeff Bezos, Warren Buffet, Mark Zuckerberg, Steve Jobs, Bill Gates, na Ratan Tata ni mfano wa mabilionea tajika walioanza maisha ya utajiri kwa kufanya kazi za kawaida mtaaani ama kuajiriwa katika kampuni ndogo na kuishia kuwa matajiri wakubwa duniani.

1: Jeff Bezos

Huyu ni mmiliki wa kampuni kubwa duniani ya Amazon ambaye kwa sasa ndio tajiri namba mbili duniani. Lakini Bezos kufika kuwa bilionea namba mbili duniani safari yake imetokea mbali. Kazi yake ya kwanza alikuwa mpishi tu, akiandaa vyakula kama baga katika kampuni ya McDonald. Alikuwa na umri wa miaka 16 tu wakati akifanya kazi hiyo na kulipwa dola $2.69, kwa lisaa limoja.

Mbali na Amazon pia anamiliki The Washington Post aliyoinunua mwaka 2017. Mwezi February 2021, Amazon ilitangaza kwamba Bezos atajiuzuli kama mtendaji mkuu wa kampuni hiyo kuanzia robo ya tatu ya mwaka huu.

Disemba 2013, Bezos alishika vichwa vya habari kwa kuanzisha majaribio aliyoyaita "Amazon Prime Air," ambayo ni utumiaji wa ndege zisizokuwa na rubani kupeleka huduma kwa wateja wake. Ndege hizo zinaweza kubeba vifurushi vyenye uzito wa mpaka kilo 2.5 na zinaweza kufika umbali wa mpaka maili 10 kutoka ofisi za usambazaji za Amazon.

2: Elon Musk

Amekulia Afrika Kusini baadae akahamia Canada akiwa na umri wa miaka 17 na kuanzia kazi ya kawaida kabisa kama Mhandisi wa program za Kompyuta. Ilikuwa mwaka 1983 na alikuwa akiuza michezo ya kompyuta na kulipwa dola $500 kwa mwezi. Mwezi Januari 2021, Musk aliripotiwa kumpiku Jeff Bezos kama mtu tajiri zaidi duniani. Inasubiriwa ripoti ya mwaka 2021 kuona matajiri hao wako kwenye nafasi zipi.

Lakini sasa ni tajiri namba tatu duniani akiajiri maelfu ya watu kupitia makampuni zake za Tesla na SpaceX zinazotengeneza roketi, magari ya umeme, umeme wa jua na mabetri akitajwa kuwa na utajiri dola za kimarekani $168.2

Utajiri wake ulianza kukuwa kwa kasi akiwa na miaka kati ya 25 na 30, akianza kwa kuiuza kampuni yake ya mwanzo mwanzo tu ya Zip2 kwenda kuwa sehemu ya Compaq Computers. Wazazi wake walitengana akiwa na miaka 10 na hapo akanza kupenda masuala ya kompyuta.

Alijifunza mwenzewe namna ya kutengeneza program za kompyuta, na akiwa na umri wa miaka 12 tu akauza program yake ya kwanza, ilikuwa ya mchezo ya kompyuta(game) iliyoitwa Blastar, safari ya utajiri ikaanzia hapo, alikuwa akitengeza na kuuza kwa bei chee kidogokidogo baadae ujuzi wake ukampa fedha na kuwa mmiliki wa kampuni kubwa duniani ya masualoa ya teknolojia.

3: Bill Gates

Bill gates ni bilionea namba nne duniani anayefahamika sana na mmiliki wa kampuni ya Microsoft. Amekuwa na mchango mkubwa katika bara la Afrika kupitia taasisi yake na mkewe ya Bill & Melinda Gates Foundation ambayo imekuwa ikisaidia masuala mbalimbali ya kijamii.

Ameongoza pia kwenye zoezi la kusaidia chanjo ya polio kwa watoto barani Afrika. Lakini hakuanza kama bilionea, alianza kama mfanyakazi wa kawaida tu kwenye kampuni iliyokuwa ndogo ya TRW, alikuwa mtengeza program za kompyuta wa kampuni hiyo, lakini sasa ni bilionea namba 4 duniani akiwa na utajiri unaofikia dola bilioni $129.2 kwa mujibu wa Forbes.

Bill gates alikacha shule akiwa mdogo tu akiwa na rafiki ya wa utotoni Paul Allen na kuamua kuanzisha Microsoft. hakuwa anaeleweka na familia yake, lakini aliamini katika fikra zake na kwa kuanza kidogokidogo akajikuta anakuwa na kutengeneza utajiri wa kutosha.

4: Warren Buffet

Warren Buffet, mfanyabiashara na bilionea mkubwa Marekani ambaye kwa mujibu wa mtandao wa Forbes anashika nafasi ya 9 kwa watu wenye utajiri mkubwa dunaini. Alianza kazi ya kusambaza magezeti tu mtaani, majumbani na maofisini akifanya kazi hiyo ya kusambaza magazeti ya The Washington Post na kulipwa kama dola $175 kwa mwezi.

Lakini sasa ni bilionea wa kutupwa akiwa mkurugenzi mtendaji wa wa makampuni ya Berkshire Hathaway nchini Marekani ambayo kwa ujumla yameajiri watu zaidi ya 360,000 na kwa mujibu wa taarifa rasmi za mwaka jana ilikuwa na utajiri wa dola bilioni 42.5.

Aiwa na miaka 11 alianza kuwekeza kwenye kampuni ya Cities Service Preferred akianza kwa kununua hisa tatu tu ambapo hisa moja iliuzwa kwa $38. Akauza hisa hizo kwa faida kiduchu kwa kuuza hisa moja kwa $40, baada ya thamani ya hisa za kampuni hiyo kushuka mpaka $27, baadae akajuta baada ya thamani ya hisa kupanda mpaka $200. Anasema majuto haya ndiyo yaliyomsukuma kufikiria zaidi uwekezaji na kuwa mmiliki wa kampuni kubwa usoni. Kufika huko ilipaswa awe na mtaji wa kuanzia, na kazi yake ya kusambaza magazeti ilikua moja ya njia ya kumfikisha alipofika sasa.

5: Salim Said Bakhresa

Ingawa si bilionea katika orodha tajika ya Forbes, lakini historia yake inamleta kwenye kundi la watu matajiri walioanza kufanya kazi za kawaida kabisa mpaka kuwa matajiri wakubwa Afrika. Ni milionea tajika Afrika akizaliwa visiwani Zanzibar, Tanzania.

Kama ilivyo kwa watoto wengi wa Tanzania na vijana wengi wa nchi hiyo, hupitia kufanya kazi nyingi za kawaida kutokana na uchumi uliopo na mazingira ya nchi hiyo. Bakhresa alianza kuuza mabaki ya mazao ya baharini tu yanayopatikana kwa wingi hata sasa kwenye fukwe za bahari katika maeneo ya Zanzibar, Dar es Salaam na Mombasa.

Bakhresa hakulala na kuamka tajiri bali alianzia mbali kuusaka utajiri wake. Alianza kwa kushona viatu, akauza urojo na viazi kabla ya kufungua mgawaha mdogo lakini leo makampuni yake kwenye sekta ya Usafirishaji, Vinywaji, vyombo vya habari, maji, vyakula, viwanda vya nguo, hoteli na vitu vingine ambayo yameajiri zaidi ya watu 2,000 na kuingiza mabilioni ya fedha.

Makampuni ya Said Salim Bakhresa & Co. (SSB), yananufaisha zaidi ya watu 6,000 kwa ajira rasmi na zisizo rasmi katika nchi za Afrika Mashariki. Bidhaa za makampuni yake zinapatikana karibu nchi sita za Afrika Mashariki. Mwaka 2008 alianzisha mpango wa kukabiliana na Malaria baada ya utafiti kuonyesha mfanyakazi wake mmoja kati ya watano hukumbwa na malaria kila mwezi.
 
Kama ilivyo kwa watoto wengi wa Tanzania na vijana wengi wa nchi hiyo, hupitia kufanya kazi nyingi za kawaida kutokana na uchumi uliopo na mazingira ya nchi hiyo. Bakhresa alianza kuuza mabaki ya mazao ya baharini tu yanayopatikana kwa wingi hata sasa kwenye fukwe za bahari katika maeneo ya Zanzibar
Hapa mkuu kuna habari kwenye mabano inayobeba chanzo cha utajiri wa huyu mfanyabiashara. Huwa haielezwi Sana lkn ndiyo ufunguo mkuu wa utajiri wake.

Kuna ndugu (nadhani baba yake) alipigwa risasi kimakosa na jeshi (sikumbuki ni la polisi ama wananchi). Yakapita mengi katkati .....lkn baadaye familia ikalipwa fidia mkwanja mrefu. Hapo ndipo biashara zikafunguliwa.

Hata hivyo bado anastahili pongezi kwa kuwa na akili ya kuanzisha na kukuza biashara.

Lkn kamwe mzidanganyike eti aliuza urojo ama kusafisha viatu, kisha akafikia hatua aliyo nayo.
 
Kila tajiri ana siri za uhalifu ambazo huwa haziekezwi kwa watu. Mzidanganyike! Ndiyo maana Mungu ameapa kutowaingiza peponi.

Mifano
1. Msukuma alikuwa mtekaji wa mabasi.
2. Diallo alikuwa na shares kidogo Sana ukilinganisha na mzungu, kwenye kampuni ya Sahara media. Akacheza mchezo mchafu akamfurusha mzungu.
3. Mengi aliwaibia sana NIC kwa kuchoma moto vikampuni hewa mara mbili kisha kulipwa bima kubwa Sana mpk NIC wakafilisika
n.k, n.k
4. Mo amepata fedha tika kwa babake ambaye alikopa fedha benki za nje kwa kutumia mashamba makubwa alioomba kama mwekezaji. Lkn akayatelekeza na kuanzisha biashara zingine. .
5. Manji...katajirikia misheni town tu. Alipewa tenda za ku-supply nguzo za umeme tanesco, kushona kombati na vuatu vya jeshi, ku-supply vyakula na sare za CCM (kofia, t-shirt na kanga).

Hata mm ukinipa vitenda kama hv natoboa.

Kwahiyo usiwasifie saaaana!
 
Kila tajiri ana siri za uhalifu ambazo huwa haziekezwi kwa watu. Mzidanganyike! Ndiyo maana Mungu ameapa kutowaingiza peponi.

Mifano
1. Msukuma alikuwa mtekaji wa mabasi.
2. Diallo alikuwa na shares kidogo Sana ukilinganisha na mzungu, kwenye kampuni ya Sahara media. Akacheza mchezo mchafu akamfurusha mzungu.
3. Mengi aliwaibia sana NIC kwa kuchoma moto vikampuni hewa mara mbili kisha kulipwa bima kubwa Sana mpk NIC wakafilisika
n.k, n.k
4. Mo amepata fedha tika kwa babake ambaye alikopa fedha benki za nje kwa kutumia mashamba makubwa alioomba kama mwekezaji. Lkn akayatelekeza na kuanzisha biashara zingine. .
5. Manji...katajirikia misheni town tu. Alipewa tenda za ku-supply nguzo za umeme tanesco, kushona kombati na vuatu vya jeshi, ku-supply vyakula na sare za CCM (kofia, t-shirt na kanga).

Hata mm ukinipa vitenda kama hv natoboa.

Kwahiyo usiwasifie saaaana!
Gain something new here🤔
 
Kila tajiri ana siri za uhalifu ambazo huwa haziekezwi kwa watu. Mzidanganyike! Ndiyo maana Mungu ameapa kutowaingiza peponi.

Mifano
1. Msukuma alikuwa mtekaji wa mabasi.
2. Diallo alikuwa na shares kidogo Sana ukilinganisha na mzungu, kwenye kampuni ya Sahara media. Akacheza mchezo mchafu akamfurusha mzungu.
3. Mengi aliwaibia sana NIC kwa kuchoma moto vikampuni hewa mara mbili kisha kulipwa bima kubwa Sana mpk NIC wakafilisika
n.k, n.k
4. Mo amepata fedha tika kwa babake ambaye alikopa fedha benki za nje kwa kutumia mashamba makubwa alioomba kama mwekezaji. Lkn akayatelekeza na kuanzisha biashara zingine. .
5. Manji...katajirikia misheni town tu. Alipewa tenda za ku-supply nguzo za umeme tanesco, kushona kombati na vuatu vya jeshi, ku-supply vyakula na sare za CCM (kofia, t-shirt na kanga).

Hata mm ukinipa vitenda kama hv natoboa.

Kwahiyo usiwasifie saaaana!
Naombeni muongozo. Nataka kutumia hiyo njia namba 1 ili na mimi baadae nitambulike kama King Tate Mkuu
 
Kila tajiri ana siri za uhalifu ambazo huwa haziekezwi kwa watu. Mzidanganyike! Ndiyo maana Mungu ameapa kutowaingiza peponi.

Mifano
Hapo ni akili ilitumika. Na tabia nzuri ya kumanage fedha. mwingine ukipata kidogo mpaka ziishe ndio unatulia, kwa tabia hizo hutoboi mpaka yesu anarudi.
 
Inaelezwa kila mtu anazaliwa tajiri lakini pia masikini. Utajiri au umasikini wake unategemea na mazingira anayokulia, lakini inategemea zaidi na yeye mwenyewe. Wapo matajiri wengi duniani ambaohawakuzaliwa matajiri. Walitengeneza utajiri wao kwa kupitia maisha ya kawaida kabisa ambayo kila mtu ama wengi wa watu wanayaishi.

Kwa mujibu wa Forbes wapo mabilionea zaidi ya 2,700 duniani lakini wengi wao walianza kufanya kazi za kawaida kabisa ambazo usingedhani kama wangeweza kuwa mabilionea.

Mabilionea kama Elon Musk, Jeff Bezos, Warren Buffet, Mark Zuckerberg, Steve Jobs, Bill Gates, na Ratan Tata ni mfano wa mabilionea tajika walioanza maisha ya utajiri kwa kufanya kazi za kawaida mtaaani ama kuajiriwa katika kampuni ndogo na kuishia kuwa matajiri wakubwa duniani.

1: Jeff Bezos

Huyu ni mmiliki wa kampuni kubwa duniani ya Amazon ambaye kwa sasa ndio tajiri namba mbili duniani. Lakini Bezos kufika kuwa bilionea namba mbili duniani safari yake imetokea mbali. Kazi yake ya kwanza alikuwa mpishi tu, akiandaa vyakula kama baga katika kampuni ya McDonald. Alikuwa na umri wa miaka 16 tu wakati akifanya kazi hiyo na kulipwa dola $2.69, kwa lisaa limoja.

Mbali na Amazon pia anamiliki The Washington Post aliyoinunua mwaka 2017. Mwezi February 2021, Amazon ilitangaza kwamba Bezos atajiuzuli kama mtendaji mkuu wa kampuni hiyo kuanzia robo ya tatu ya mwaka huu.

Disemba 2013, Bezos alishika vichwa vya habari kwa kuanzisha majaribio aliyoyaita "Amazon Prime Air," ambayo ni utumiaji wa ndege zisizokuwa na rubani kupeleka huduma kwa wateja wake. Ndege hizo zinaweza kubeba vifurushi vyenye uzito wa mpaka kilo 2.5 na zinaweza kufika umbali wa mpaka maili 10 kutoka ofisi za usambazaji za Amazon.

2: Elon Musk

Amekulia Afrika Kusini baadae akahamia Canada akiwa na umri wa miaka 17 na kuanzia kazi ya kawaida kabisa kama Mhandisi wa program za Kompyuta. Ilikuwa mwaka 1983 na alikuwa akiuza michezo ya kompyuta na kulipwa dola $500 kwa mwezi. Mwezi Januari 2021, Musk aliripotiwa kumpiku Jeff Bezos kama mtu tajiri zaidi duniani. Inasubiriwa ripoti ya mwaka 2021 kuona matajiri hao wako kwenye nafasi zipi.

Lakini sasa ni tajiri namba tatu duniani akiajiri maelfu ya watu kupitia makampuni zake za Tesla na SpaceX zinazotengeneza roketi, magari ya umeme, umeme wa jua na mabetri akitajwa kuwa na utajiri dola za kimarekani $168.2

Utajiri wake ulianza kukuwa kwa kasi akiwa na miaka kati ya 25 na 30, akianza kwa kuiuza kampuni yake ya mwanzo mwanzo tu ya Zip2 kwenda kuwa sehemu ya Compaq Computers. Wazazi wake walitengana akiwa na miaka 10 na hapo akanza kupenda masuala ya kompyuta.

Alijifunza mwenzewe namna ya kutengeneza program za kompyuta, na akiwa na umri wa miaka 12 tu akauza program yake ya kwanza, ilikuwa ya mchezo ya kompyuta(game) iliyoitwa Blastar, safari ya utajiri ikaanzia hapo, alikuwa akitengeza na kuuza kwa bei chee kidogokidogo baadae ujuzi wake ukampa fedha na kuwa mmiliki wa kampuni kubwa duniani ya masualoa ya teknolojia.

3: Bill Gates

Bill gates ni bilionea namba nne duniani anayefahamika sana na mmiliki wa kampuni ya Microsoft. Amekuwa na mchango mkubwa katika bara la Afrika kupitia taasisi yake na mkewe ya Bill & Melinda Gates Foundation ambayo imekuwa ikisaidia masuala mbalimbali ya kijamii.

Ameongoza pia kwenye zoezi la kusaidia chanjo ya polio kwa watoto barani Afrika. Lakini hakuanza kama bilionea, alianza kama mfanyakazi wa kawaida tu kwenye kampuni iliyokuwa ndogo ya TRW, alikuwa mtengeza program za kompyuta wa kampuni hiyo, lakini sasa ni bilionea namba 4 duniani akiwa na utajiri unaofikia dola bilioni $129.2 kwa mujibu wa Forbes.

Bill gates alikacha shule akiwa mdogo tu akiwa na rafiki ya wa utotoni Paul Allen na kuamua kuanzisha Microsoft. hakuwa anaeleweka na familia yake, lakini aliamini katika fikra zake na kwa kuanza kidogokidogo akajikuta anakuwa na kutengeneza utajiri wa kutosha.

4: Warren Buffet

Warren Buffet, mfanyabiashara na bilionea mkubwa Marekani ambaye kwa mujibu wa mtandao wa Forbes anashika nafasi ya 9 kwa watu wenye utajiri mkubwa dunaini. Alianza kazi ya kusambaza magezeti tu mtaani, majumbani na maofisini akifanya kazi hiyo ya kusambaza magazeti ya The Washington Post na kulipwa kama dola $175 kwa mwezi.

Lakini sasa ni bilionea wa kutupwa akiwa mkurugenzi mtendaji wa wa makampuni ya Berkshire Hathaway nchini Marekani ambayo kwa ujumla yameajiri watu zaidi ya 360,000 na kwa mujibu wa taarifa rasmi za mwaka jana ilikuwa na utajiri wa dola bilioni 42.5.

Aiwa na miaka 11 alianza kuwekeza kwenye kampuni ya Cities Service Preferred akianza kwa kununua hisa tatu tu ambapo hisa moja iliuzwa kwa $38. Akauza hisa hizo kwa faida kiduchu kwa kuuza hisa moja kwa $40, baada ya thamani ya hisa za kampuni hiyo kushuka mpaka $27, baadae akajuta baada ya thamani ya hisa kupanda mpaka $200. Anasema majuto haya ndiyo yaliyomsukuma kufikiria zaidi uwekezaji na kuwa mmiliki wa kampuni kubwa usoni. Kufika huko ilipaswa awe na mtaji wa kuanzia, na kazi yake ya kusambaza magazeti ilikua moja ya njia ya kumfikisha alipofika sasa.

5: Salim Said Bakhresa

Ingawa si bilionea katika orodha tajika ya Forbes, lakini historia yake inamleta kwenye kundi la watu matajiri walioanza kufanya kazi za kawaida kabisa mpaka kuwa matajiri wakubwa Afrika. Ni milionea tajika Afrika akizaliwa visiwani Zanzibar, Tanzania.

Kama ilivyo kwa watoto wengi wa Tanzania na vijana wengi wa nchi hiyo, hupitia kufanya kazi nyingi za kawaida kutokana na uchumi uliopo na mazingira ya nchi hiyo. Bakhresa alianza kuuza mabaki ya mazao ya baharini tu yanayopatikana kwa wingi hata sasa kwenye fukwe za bahari katika maeneo ya Zanzibar, Dar es Salaam na Mombasa.

Bakhresa hakulala na kuamka tajiri bali alianzia mbali kuusaka utajiri wake. Alianza kwa kushona viatu, akauza urojo na viazi kabla ya kufungua mgawaha mdogo lakini leo makampuni yake kwenye sekta ya Usafirishaji, Vinywaji, vyombo vya habari, maji, vyakula, viwanda vya nguo, hoteli na vitu vingine ambayo yameajiri zaidi ya watu 2,000 na kuingiza mabilioni ya fedha.

Makampuni ya Said Salim Bakhresa & Co. (SSB), yananufaisha zaidi ya watu 6,000 kwa ajira rasmi na zisizo rasmi katika nchi za Afrika Mashariki. Bidhaa za makampuni yake zinapatikana karibu nchi sita za Afrika Mashariki. Mwaka 2008 alianzisha mpango wa kukabiliana na Malaria baada ya utafiti kuonyesha mfanyakazi wake mmoja kati ya watano hukumbwa na malaria kila mwezi.
Cc Bbcswahili
 
Kila tajiri ana siri za uhalifu ambazo huwa haziekezwi kwa watu. Mzidanganyike! Ndiyo maana Mungu ameapa kutowaingiza peponi.

Mifano
1. Msukuma alikuwa mtekaji wa mabasi.
2. Diallo alikuwa na shares kidogo Sana ukilinganisha na mzungu, kwenye kampuni ya Sahara media. Akacheza mchezo mchafu akamfurusha mzungu.
3. Mengi aliwaibia sana NIC kwa kuchoma moto vikampuni hewa mara mbili kisha kulipwa bima kubwa Sana mpk NIC wakafilisika
n.k, n.k
4. Mo amepata fedha tika kwa babake ambaye alikopa fedha benki za nje kwa kutumia mashamba makubwa alioomba kama mwekezaji. Lkn akayatelekeza na kuanzisha biashara zingine. .
5. Manji...katajirikia misheni town tu. Alipewa tenda za ku-supply nguzo za umeme tanesco, kushona kombati na vuatu vya jeshi, ku-supply vyakula na sare za CCM (kofia, t-shirt na kanga).

Hata mm ukinipa vitenda kama hv natoboa.

Kwahiyo usiwasifie saaaana!
Matajiri wataingia mbinguni vizuri tuu
Ule mfano wa ni heri kwa Ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko tajiri kuingia mbinguni ni kwamba, sehemu ya kuabudia ya Wayahudi ilikua na milango miwili, mmoja uliitwa mlango mzuri ambao kuna muda ukifika ufungwa na mlango mwingine huitwa tundu la sindano ambao huwa una fungwa nusu...
Sasa hii milango ni ile ambayo huwa inafunguka kutoka juu, hivyo ukifungwa nusu maana yake ili upenye wewe na Ngamia wako kwenda kwenye ibada itabidi yule Ngamia apite pale kwa kutambaa na magoti kwakua ni mrefu.
Elimu hiyo wape na wengine.
 

Similar Discussions

5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom