MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Sijawahi kuona Rafiki mnayeshibana akakuombea mabaya ila Ndugu kuombeana mabaya hata Kufa Kwako ni Jambo la kawaida.
Sijawahi kuona Rafiki mnayeshibana akawa Mnafiki dhidi yako ila kwa Ndugu Kukusanifu huku akikuchekea ni Jambo la kawaida.
Sijawahi kuona Rafiki mnayeshibana akaona kuna Fursa ya Ajira na asikuunganishe ila ni Nadra mno kwa Ndugu kutaarifiana kuhusu upatikanaji wa Fursa za Kimafanikio.
Sijawahi kuona Rafiki mnayeshibana akaacha kuwa upande wako pale ukiwa na Changamoto za Kimaisha ila Ndugu watakuwa nawe huku wakiwa Wanakusimanga na hata kukuona Kero.
Sijawahi kuona Rafiki mnayeshibana akawa anakuteta na hata Kukuharibia ila Ndugu wengi wana huu Utamaduni wa Kuharibiana na Kuteta tena wengine unakuta Mafanikio yao Kimaisha yametokana na huyo Wanayemteta.
Sijawahi kuona Rafiki mnayeshibana ukiwa na shida na kumuomba Msaada akaanza Kukutangazia kwa Watu ila Ndugu wengi ukiwa na Uhitaji wako tegemea Kusaidiwa nae ila Kutangazwa kwa Ndugu wote wa Ukoo.
Sijawahi kuona Rafiki mnayeshibana akaacha hata Siku Mbili au Tatu asiwasiliane nawe ila kwa Ndugu mnaweza kupitisha hata miaka miwili bila Kuwasiliana na Kuwasiliana kwenu kutakuwa ni kupeana tu taarifa za Msiba au kuletewa Kadi ya Harusi ya Ndugu ya Ukoo.
Jitahidi sana utunze Marafiki ulionao, usiwakosee kwani hao ndiyo Kiuhalisia wenye Uchungu na Upendo nawe kuliko Ndugu ambao ukiwa nacho Wanakuthamini ila Ukianguka kimaisha Wanakukwepa, Wanakudharau, Wanakucheka na hata kuzidi tu Kukuombea mabaya.
Mwenyezi Mungu awabariki Marafiki.
Sijawahi kuona Rafiki mnayeshibana akawa Mnafiki dhidi yako ila kwa Ndugu Kukusanifu huku akikuchekea ni Jambo la kawaida.
Sijawahi kuona Rafiki mnayeshibana akaona kuna Fursa ya Ajira na asikuunganishe ila ni Nadra mno kwa Ndugu kutaarifiana kuhusu upatikanaji wa Fursa za Kimafanikio.
Sijawahi kuona Rafiki mnayeshibana akaacha kuwa upande wako pale ukiwa na Changamoto za Kimaisha ila Ndugu watakuwa nawe huku wakiwa Wanakusimanga na hata kukuona Kero.
Sijawahi kuona Rafiki mnayeshibana akawa anakuteta na hata Kukuharibia ila Ndugu wengi wana huu Utamaduni wa Kuharibiana na Kuteta tena wengine unakuta Mafanikio yao Kimaisha yametokana na huyo Wanayemteta.
Sijawahi kuona Rafiki mnayeshibana ukiwa na shida na kumuomba Msaada akaanza Kukutangazia kwa Watu ila Ndugu wengi ukiwa na Uhitaji wako tegemea Kusaidiwa nae ila Kutangazwa kwa Ndugu wote wa Ukoo.
Sijawahi kuona Rafiki mnayeshibana akaacha hata Siku Mbili au Tatu asiwasiliane nawe ila kwa Ndugu mnaweza kupitisha hata miaka miwili bila Kuwasiliana na Kuwasiliana kwenu kutakuwa ni kupeana tu taarifa za Msiba au kuletewa Kadi ya Harusi ya Ndugu ya Ukoo.
Jitahidi sana utunze Marafiki ulionao, usiwakosee kwani hao ndiyo Kiuhalisia wenye Uchungu na Upendo nawe kuliko Ndugu ambao ukiwa nacho Wanakuthamini ila Ukianguka kimaisha Wanakukwepa, Wanakudharau, Wanakucheka na hata kuzidi tu Kukuombea mabaya.
Mwenyezi Mungu awabariki Marafiki.