Deva
JF-Expert Member
- May 29, 2018
- 1,238
- 1,800
Wakuu habari ya asubuhi.
Moja kwa moja niende kwenye mada, huyu mwanamke nimekuwa naye kwenye mahusiano kwa miezi kadhaa, kuna wakati alishika ujauzito, tukakubaliana kulea mimba hiyo, basi tukalea mpaka ilipofika miezi mitatu ndio balaa likaanza, yeye kutaka tuachane.
Kuna siku alikuja kunitembelea, alipofika akawa anachat sana na simu nikamuuliza vipi mbona uko busy na simu? Akanijibu "hata hivyo ni simu yangu" nilichukizwa na jibu hilo nikanyamaza, nikampa muda zaidi, nilivyoona kazidisha nikamnyang'anya hiyo simu nikaiweka pembeni, basi tukaendelea na mazungumzo, wakati simu yangu mimi iko pembeni ilipigwa na sms ziliingia ila sikupokea wala kusoma sms, baada ya muda nikasema ngoja niichungulie, nikajibu sms za muhimu kwa dakika chache, nikamrudia tukaendelea kuongea, tukamaliza tukaagana akaenda.
Alipofika nyumbani, akaniuliza hivi ulinionaje pale ulivyokuwa unajibu sms mimi nipo pale, nikamueleza vizuri kuwa nilijibu kuwa kuna ujumbe wa muhimu nilitumiwa, basi akaanza kusema hanitaki tuachane, sikumtilia maana nikihisi ni hali ya mimba, ila aliendelea kukaza msimamo wake, baadae nilikuta ameniblock njia zote, sms, calls whatsapp, njia zote za mawasiliano nikawa simpati, hiyo hali ikaendelea kwa week mbili.
Jana ndipo alinitumia sms ya kunijulia hali, nikamuuliza mustakabali wa mahusiano, akanijibu kuwa kashaanzisha mahusiano mengine, yana wiki moja, na amemueleza huyo mwanaume kuhusu mimba akakubali kuilea, nikamuuliza sababu ya kufanya hivyo endapo mimi mhusika wa mimba hiyo nipo na nimekubali kuilea akaniambia ni kwa sababu mimi hawezi kunitambulisha kwao kama baba wa mtoto, nikamueleza sio vizuri alivyofanya, nikamuuliza kuwa kuhusu suala la clinic akasema kuwa nikitaka nitampeleka au nisipotaka huyo jamaa atampeleka! akiwa katika mizunguko yake na huyo jamaa siku ya jumatatu nimpitie nimpeleke clinic.
Nikauliza kuhusu hatma ya mtoto alichonijibu kuwa mtoto atakuwa na baba yule atakayefahamika kwao kama baba mtoto na mimi nitakuwa kama baba mzazi, kitu asichoweza ni kunitambulisha kama baba mzazi wa mtoto na yule jamaa anafahamu hilo kuwa mimba ni yangu ila yeye ni mlezi, sasa wakuu niko njia panda.
Mtu aliyeamua kuwa nae ni doctor wa hospital ambayo nimekuwa nikimpeleka kwa ajili ya kucheck ultrasound scan, mwanzoni nilikuta mawasiliano yao akasema amemcheck kwa ajili ya issue za kiafya nikamzuia asiwasiliane naye, kumbe hakufanya hivyo aliendelea kuwasiliana nae kwa siri, ndipo imefikia mahali hapa.
Nifanyeje.
Moja kwa moja niende kwenye mada, huyu mwanamke nimekuwa naye kwenye mahusiano kwa miezi kadhaa, kuna wakati alishika ujauzito, tukakubaliana kulea mimba hiyo, basi tukalea mpaka ilipofika miezi mitatu ndio balaa likaanza, yeye kutaka tuachane.
Kuna siku alikuja kunitembelea, alipofika akawa anachat sana na simu nikamuuliza vipi mbona uko busy na simu? Akanijibu "hata hivyo ni simu yangu" nilichukizwa na jibu hilo nikanyamaza, nikampa muda zaidi, nilivyoona kazidisha nikamnyang'anya hiyo simu nikaiweka pembeni, basi tukaendelea na mazungumzo, wakati simu yangu mimi iko pembeni ilipigwa na sms ziliingia ila sikupokea wala kusoma sms, baada ya muda nikasema ngoja niichungulie, nikajibu sms za muhimu kwa dakika chache, nikamrudia tukaendelea kuongea, tukamaliza tukaagana akaenda.
Alipofika nyumbani, akaniuliza hivi ulinionaje pale ulivyokuwa unajibu sms mimi nipo pale, nikamueleza vizuri kuwa nilijibu kuwa kuna ujumbe wa muhimu nilitumiwa, basi akaanza kusema hanitaki tuachane, sikumtilia maana nikihisi ni hali ya mimba, ila aliendelea kukaza msimamo wake, baadae nilikuta ameniblock njia zote, sms, calls whatsapp, njia zote za mawasiliano nikawa simpati, hiyo hali ikaendelea kwa week mbili.
Jana ndipo alinitumia sms ya kunijulia hali, nikamuuliza mustakabali wa mahusiano, akanijibu kuwa kashaanzisha mahusiano mengine, yana wiki moja, na amemueleza huyo mwanaume kuhusu mimba akakubali kuilea, nikamuuliza sababu ya kufanya hivyo endapo mimi mhusika wa mimba hiyo nipo na nimekubali kuilea akaniambia ni kwa sababu mimi hawezi kunitambulisha kwao kama baba wa mtoto, nikamueleza sio vizuri alivyofanya, nikamuuliza kuwa kuhusu suala la clinic akasema kuwa nikitaka nitampeleka au nisipotaka huyo jamaa atampeleka! akiwa katika mizunguko yake na huyo jamaa siku ya jumatatu nimpitie nimpeleke clinic.
Nikauliza kuhusu hatma ya mtoto alichonijibu kuwa mtoto atakuwa na baba yule atakayefahamika kwao kama baba mtoto na mimi nitakuwa kama baba mzazi, kitu asichoweza ni kunitambulisha kama baba mzazi wa mtoto na yule jamaa anafahamu hilo kuwa mimba ni yangu ila yeye ni mlezi, sasa wakuu niko njia panda.
Mtu aliyeamua kuwa nae ni doctor wa hospital ambayo nimekuwa nikimpeleka kwa ajili ya kucheck ultrasound scan, mwanzoni nilikuta mawasiliano yao akasema amemcheck kwa ajili ya issue za kiafya nikamzuia asiwasiliane naye, kumbe hakufanya hivyo aliendelea kuwasiliana nae kwa siri, ndipo imefikia mahali hapa.
Nifanyeje.