K Vant na tatizo la kusahau

karibia wote mnasematuK vant inasahaulisha mbona haija wasahaulisha kuwa mlikunywa yenyewe ndo ikawasahaulisha, au unywapo unasahau matukio mengine kabla ya kulewa ila la kuagiza Kvant unywe halisahaulishwi.

nahisi K VANT. ukiinywa sana macho yanakuwakmhuyu
FB_IMG_16447381002832840.jpg
 
We kunywa bia tuu ,k vant waachie wao wenyewe ,k vant haijawai kuwa na mwisho mzuri, kama ujapoteza simu basi umepasua kioo au imearibika vibaya, kama hamjapigana na wale ulioenda nao basi umekwaruzana na muhudumu au meneja ,kama hujamshika mtu makalio basi kunatukio tu utakuwa umelifanya linalofanana nalo kama hukupata ajari basi kulala kituoni ni kawaida.
Wewe sasa umemaliza kila kitu. Kiufupi hiki ni kinywaji unakunywa siku unayosema "leo nataka nijiharibie maisha."
 
Hasa hizi chupa ndogo za konyagi na kvant yani feki zipo mpaka kwenye maduka makubwa,nimeachana na hayo makalakali,yani usiombe ukagongana na hiyo feki ukinywa hata chupa ndogo moja utalewaeea siku tatu.
Unakumbuka kile kiwanda feki Babati. Bora kile. Kuna kile Cha wachina Buguruni mpaka Hennessy wanatengeneza.
Sasa naonaga wanywa Hennessy wanajiona wako matawiii, kumbe wanakunywa mikojo ya wachina.
 
Sio Jack Daniel tu. Ni karibia whiskey zote.hazina hangover.
Jaribu GRANT'S pia utanishukuru
Sema whiskey za dar es salaaam zina tofauti kidogo kwenye ladha na za sehemu nyingine hasa nje ya tanzania.
Brandy nazo hivyo hivyo. Nimewahi kunywa hennessy vs nairobi kwa muda kidogo kisha nikaja kunya dar, tofauti kwenye taste. Labda mdomo wangu unaniongopea au hali ya hewa au nini sijui. Tofauti ipo japo sio kubwa sana
 
Sema whiskey za dar es salaaam zina tofauti kidogo kwenye ladha na za sehemu nyingine hasa nje ya tanzania.
Brandy nazo hivyo hivyo. Nimewahi kunywa hennessy vs nairobi kwa muda kidogo kisha nikaja kunya dar, tofauti kwenye taste. Labda mdomo wangu unaniongopea au hali ya hewa au nini sijui. Tofauti ipo japo sio kubwa sana
Bongo Pombe Kali nyingi sana zinatengenezwa feki..

Jana tu nimekunywa Hunting Lodge ina ladha tofauti kabisa na nilivyozoea.. Hapa nawaza kuachana kabisa na haya ma kali, bora nijinyweege tu vile vi juice wanaitaga Imagi na Dompo..
 
Sasa hivi ugonjwa wa kufeli Figo ni namba nne.
1. Kisukari
2. Presha
3. Ukosefu wa nguvu za kiume
4. Kufeli kwa Figo

Kumbuka Kuna pombe Kali nyingi Sana feki mtaani wanazotengeneza wachina majumbani. Zina sticker za tra na chupa halisi.
Especially konyagi, K vant na Hennessy.
Drink at your own risk.
Hii ilinikutaga nilikunywa ka JD kale kadogo nilikuwa sina mzuka wa kunywa sana.

5 days nilishinda kitandani naumwa balaa.

Nilijua figo tayari sababu ilikuwa rangi ile ile ya JD.

Fake shit everywhere yaani.
 
Back
Top Bottom