silent lion
JF-Expert Member
- Feb 28, 2012
- 1,161
- 1,535
Wakuu saa moja ilopitA kulikua na taharuki kubwa Darajani watu walikua wanakimbia ovyo. Tetesi ni kuwa kuna bomu la kutegwa.
Sasa hivi kuna mshindo mkubwa umesikika sasa cjui kama ndio hilo bomu . Mwenye taarifa atujuze.
UPDATES:
Ni bomu kweli lilitegwa karibu na kituo cha polisi Mkunazini . Kuna clip iko facebook inaonyesha wakati wa kuteguliwa.
Kwa mujibu wa Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamdan Omar, amesema jana Jeshi la Wananchi kwa kushirikiana na polisi wametegua bomu lililotegwa pale Mkunazini
Sasa hivi kuna mshindo mkubwa umesikika sasa cjui kama ndio hilo bomu . Mwenye taarifa atujuze.
UPDATES:
Ni bomu kweli lilitegwa karibu na kituo cha polisi Mkunazini . Kuna clip iko facebook inaonyesha wakati wa kuteguliwa.
Kwa mujibu wa Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamdan Omar, amesema jana Jeshi la Wananchi kwa kushirikiana na polisi wametegua bomu lililotegwa pale Mkunazini
Wanabodi,
Zanzibar hali tete!. Kuna bomber mmoja, katega bomu eneo la Darajani Zanzibar, kisha huruma kuhusu vifo ikamuingia, akaogopa na kuamua karipoti polisi, polisi nao wakaogopa bomu, wakaripoti JWTZ, JWTZ wakaingilia kati, wakalitegua bomu hilo kwa kulilipua bila kuleta madhara.
Kwa mujibu wa Radio One, Wataalamu hao, wamefanikiwa kulilipua bomu hilo lililokuwa limetengwa eneo la Darajani Zanzibar!.
Kama mambo yenyewe ndio haya, kuna uwezekano wa uwepo wa suicidal bombers!.
Haya yamechangiwa na huruma na udhaifu wa dhaifu!, ingekuwa ni enzi za Nyerere, hakuna mtu yoyote Zanzibarr ambaye angethubutu hata kukohoa!. Leo mtu anajitangazia ushindi halafu bado yupo, anaachwa tuu hivi hivi tukiendelea kumchekea!. Si mnakumbuka ya Jumbe?!.
Suluhisho la Zanzibar ni ama CCM wakubali matokeo, mshindi halali atangazwe, akabidhiwe madaraka, au SMZ ifunge tuu macho ichukue maamuzi magumu, vinginvyo Zanzibar ita suffer the consequences!.
Tanzania bara hatuwezi kuiacha Zanzibar situation ikiwa volatile hivi ilivyo, ama Rais Kikwete afanye kitu, au Magufuli aapishwe kesho Jumapili, ili tangu Jumatatu, "hapa kazi tuu" ianze rasmi Jumatatu, na kazi number 1 ni Zanzibar Heshima!, Adabu!.
Mkumbuke Zanzibar haiwezi kuachwa hivi hivi kwa kisingizio, uchaguzi ni mambo ya ndani ya Zanzibar, Zanzibar sio nchi, ni sehemu ya JMT!, Tanzania ni nchi moja, yenye upande mmoja wenye amani tele, na upande mwingine wenye hali tete!.
Huyo kijana aliyekiri kutega bomu Darajani, akimtaja aliyemtuma, asikamatwe, wala asifunguliwe mashitaka yoyote!, inatakiwa akimtaja tuu aliyemtuma, ni kimya kimya!.
Pasco
Attachments
Last edited by a moderator: