We Know Next
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 814
- 380
Ndugu wanzegu wa JF na watanzania wote kwa ujumla wenu, yale yaliyosemwa sana kwamba JWTZ wanawekwa chonjo ktk uchaguzi huu, ni ya kweli tu. Nimeshuhudia kwa macho yangu pale Lugalo jeshini mida hii ya saa saba na nusu mchana, wanajeshi wa JWTZ walikuwa wanajifua pale ktk viwanja vyao. Nimesema hivyo kwasababu zana walizokuwa nazo ni zile zana ambazo hutumika kutuliza ghasia, kama vile virungu, ngao, machela na mabomu ya machozi. Nimewaona wakiwa na zana mpya kabisa, ukiziona zile ngao zao ni rangi ya silver, zinawaka kwelikweli. Nadhani yaliyosemwa si bure. Bila shaka vikosi vyote vitakuwa na zoezi kama hilo hapa nchini.