Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,463
- 39,929
- Tanzania Mpya Bila Ulinzi Mpya - Inawezekana?
Tanzania inahitaji kujionesha ni taifa linalojiamini na ambalo linajua uwepo wake una maana gani. Ili kuweza kufikia hapo ni lazima kwanza kama taifa tutambue na kuwa tayari kulinda na kutetea uwepo wetu kama taifa kutoka tishio lolote la uwepo huo (existential threat). Karibu mataifa yote ambayo yameweza au yanajenga nchi za kisasa yamejikuta yakiangalia pia dhana hii ya sababu yao kuwepo na hivyo kujenga uchumi na miundombinu ambayo itahakikisha kuwa taifa hilo linakuwepo. Katika nchi kama ya kwetu ambayo inataka kuwa ya kisasa hatuwezi kabisa kutenganisha uchumi kutoka kasika jeshi au nafasi ya jeshi katika kuulinda uchumi huo na hata kuuchochea.
Maswali yanahitaji kujibiwa
a. jeshi letu ni la nini hasa? swali jepesi lakini lina uzito wake. Zamani tulikuwa ni jeshi ambalo lilikuwa zaidi kwa ajili ya ulinzi katika mazingira ya vita baridi na tishio la uvamizi wa Afrika ya Kusini, Wareno n.k Hivyo lilikuwa ni jeshi la kiukombozi zaidi (liberating force) na hivyo tulifanya vizuri sehemu mbalimbali. Lakini leo hii jeshi hili ni la nini? Hatuna tishio la kuvamiwa na Afrika ya Kusini, hatuna tishio la kuvamiwa na Wareno na wala hatuna tishio hasa la kuvamiwa na nchi yeyote jirani so jeshi letu linatulinda kuhusu nini au nani hasa?
Jibu la swali hilo ni msingo wa nadharia ya kijeshi (foundation for the military doctrine). Naomba kupendekeza kwamba lazima jibu lihusiane na uchumi.
b. Jeshi letu linasimamiwaje na siasa zetu liko vipi? Mojawapo ya mambo ambayo binafsi yananitaza ni kuwa jeshi letu liko kama jeshi la CCM hivi ambapo viongozi na muundo wake unafikiria zaidi uwepo wa CCM kuliko kitu kingine chochote. Sasa hili lina sababu za kihistoria bila ya shaka kwani baada ya mgomo wa jeshi wa 1964 jeshi liliundwa likiwa limefungamana na TANU na kwa karibu miaka thelathini uongozi wa jeshi ulikuwa vile vile unahusiana na uongozi wa kisiasa wa chama tawala. Sasa katika mazingira ya vyama vingi jeshi letu linakuwa vipi? Leo hii Dr. Slaa anaweza kwenda na kuzungumza na viongozi wa jeshi kuelezea sera za CDM, je kiongozi wa jeshi anaweza kwenda kutembelea ofisi za CUF kujifunza mambo ya CUF bila kuoneakana anapendelea kitu fulani? Je kiongozi wa CCM anaweza kuwepo kwenye kundi la maafisa wa JWTZ bila kuonekana anapendelewa na jeshi?
Je katika mfumo wa vyama vingi ni taratibu gani zinazoongoza mahusiano ya jeshi na vyama vya siasa? Je jeshi laweza kukaa pembeni na kuacha siasa ziendeshwe huku lenyewe likita tayari kumpigia saluti yeyote anayechaguliwa na wananchi? au linaweza kuapa kama ilivyokuwa kwa jeshi la Zimbabwe kuwa halitompigia saluti kiongozi wa upinzani?
Nadhani kuna mambo ambayo ni muhimu kuyafikiria kidogo - nimewahi kuyaandika huko nyuma kidogo na inshallah, nitaliendeleza kwa kina hili wazo siku moja.
a. Uchumi wa Kisasa unataka Ulinzi wa Kisasa (Moden Economy demands modern defenses)
Mojawapo ya vitu ambavyo unaweza kuviona kirahisi nchini sasa hivi ni msisitizo mkubwa uliopo katika kuufanya uchumi wetu kuwa wa kisasa zaidi na wenye kuendeshwa na sekta mbalimbali. Kutoka kwenye uchumi wa kilimo hasa na kuwa uchumi wa uzalishaji wa viwandani na hata wa sekta nyingine. Kutokana na msisitizo huo uchumi wa Tanzania unazidi kutoa nafasi zaidi kwa wananchi japo naweza kujenga hoja kuwa sidhani kama tumefikia hata 5% ya uwezo wetu kiuchumi. Sasa uchumi wa namna hiyo unavutia watu wengi na mojawapo ya hatari zake ni kuvutia watu wahalifu na watu wenye nia mbaya.
Mwaka huu peke yake tumesikia jinsi madawa ya kulevya kwa mashehena yakikamatwa katika ardhi yetu, ukijumlisha hilo na tuhuma za ufisadi unaweza kuona toka mbali tu kuwa uchumi wetu unavutia zaidi ya watu wema au taasisi njema. Kutoka mbali unaweza kuona kwa urahisi kabisa kuwa bila kuulinda uchumi huu utaenda ile njia ya Nigeria. Binafsi hiyo ndio hofu yangu kubwa sana kwamba Tanzania itaenda njia ya Nigeria kwa sababu tumeshindwa kujipanga na kukabiliana vilivyo na changamoto za uchumi wa kisasa.
Ukiangalia China kwa mfano, tangu walipoanza mabadiliko makubwa ya kiuchumi mwishoni mwa 1970s walienda sambamba na mabadiliko yao mtazamo wao wa kijeshi. Walienda pamoja na kujenga uchumi wa kisasa kujenga jeshi la kisasa. Leo hii japo jeshi la China halijafikia uwezo wa majeshi kama ya Marekani na hata Ufaransa kwa kiwango kikubwa sana limekuwa jeshi la kisasa na linaanza kujitambulisha zaidi. Wiki chache tu zilizopita Jeshi hilo limetoa whitepaper ambayo inaelezea kile kinachoitwa "Peaceful Rise" kwamba China inataka kuinuka kama taifa lenye nguvu bila kulazimisha kukandamiza au kuonesha nguvu hizo kama ilivyokuwa kwa mataifa mengine. Ni wazo zuri lakini ninaamini siku moja china itahitaji kujitutumua kijeshi kutuma ujumbe kuwa "imefika". Na utakuwa mwanzo wa aina nyingine ya Vita baridi.
Kwa tanzania Jeshi na vyombo vyetu vya usalama bado ni vya kizamani sana. TISS, Polisi na TPDF yenyewe bado havijawa katika level ya kuweza kuwa walinzi wa uchumi wa kisasa. Na ninaamini tutapata shida sana siku yakigundulika mafuta na hivyo kufanya "wakubwa" kujichekelesha zaidi na kwa mtu yeyote anayeona yanayoendelea ataelewa wazi kabisa courtship inayofanywa na Marekani haina malengo ya leo bali zaidi ya kesho. Je ni kwa kiasi gani tutangeneza vyombov ya kisasa?
Kati ya vyama vyote vya kisiasa kwenye uchaguzi mkuu uliopita ni CHADEMA ndicho kilichokuwa na maono ya kubadilisha na kuleta mfumo wetu wa vyombo vya usalama kuleta ulinzi wa kisasa wa uchumi wetu. Bila kuongozwa na mtazamo wa kuboresha uchumi na usalama kwa wakati mmoja matokeo yake ni kuwa tutakuwa na uchumi mkubwa ambao utakuwa prone to manipulation n.k the so called the Nigerian Way. Tutapigana, tutachinjana na kufisadiana huku tunachelekea "uchumi wetu unapaa!".
b. Jeshi la WTZ halijaweza kuwa jeshi ambalo linawajibika kwa wananchi sawasawa. Kuna hali ya impunity of sort kiasi kwamba hizi cable zinatuonesha hofu ya viongozi wa kiraia kulisimamia jeshi na hivyo jeshi linaanza kuwa an institution with its own gear. Hii ni hatari sana. Ninaamini mojawapo ya mabadiliko tutakayoyahitaji ni kuhakikisha kuwa jeshi kweli linarudishwa mikononi mwa wananchi. Dhana ya Jeshi katika nchi ya kidemokrasia bado haijazama na angalizo la kina Retzer kuwa jeshi letu bado lina socialist tendencies ni kweli kwani tuliona wenyewe wakati wa uchaguzi mkuu mwaka jana.
Tayari tumeshaona mgongano kati ya Bunge na Urais, tumeona kidogo tu mgongano wa Bunge na Mahakama; bado hatujaona mgongano kati ya Mahakama na Urais na vile vile mgongano wa Serikali (Bunge, Urais Mahakama) na Jeshi. Mgongano huu ni wa lazima ili kuweza kuchora mistari sahihi. Mgongano kama huu umetokea Uturuki ambapo viongozi kadhaa wa jeshi walikamatwa na kufikishwa mahakama na kusababisha wakuu wengine wa jeshi kujiuzulu. je itakuwaje siku current military leaders wa Tanzania wanakamatwa na kufikishwa mahakama kutokana na ufisadi? Je, hofu kuwa ufisadi jeshini ukiumbuliwa jeshi linaweza kuasi ni ya msingi?
Katika kujibu maswali hayo tunakabiliwa na changamoto ya kujiuliza juu ya mahusiano ya jeshi na vyama vya siasa n.k Lakini vile vile inahoji hasa nadharia za kijeshi za nchi je zinatokana na siasa za vyama au zinatoka kwenye jeshi tu? Je ipo haja ya kukaa kama taifa kwanza tunapozungumzia Katiba Mpya kufikiria vile vile juu ya Nadharia ya kijeshi ya nchi yetu? Je katika kujenga uchumi wa kisasa na taifa la kisasa jeshi letu litakuwa na nafasi gani? Tukiangalia kutoka mbali tunaweza kuona kuwa ripoti za Wikileaks hasa kuhusiana na mahusiano ya utawala wa kijeshi na ule wa kiraia tunabakia kujiuliza maswali ambayo labda hatutaweza kuyajibu mara moja.
Lakini ni maswali ambayo yanahitaji na kustahili kujibiwa, kama siyo leo basi siku moja.
MMM