Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,870
- 155,827
JESHI la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania (JWTZ), linatarajia kuanzisha benki yake itakayowasaidia wanajeshi kupata mikopo ya riba nafuu, kwa ajili ya kuendeleza kipato na mitaji ya biashara zao.
Akizungumza kwenye mkutano wa kuhamasisha shughuli za ujasiriamali ndani ya jeshi hilo Dar es Salaam jana, Mkuu wa Operesheni na Mafunzo, Meja Jenerali Sylvester Rioba, alisema hivi sasa wana mtaji wa Sh1.7 bilioni na kwamba, wanahitaji Sh15 bilioni ili kutekeleza azma hiyo.
Jenerali Rioba alisema kutokana na hali hiyo, fedha hizo zitapatikana kwenye michango ya wanachama wa Chama cha Akiba na Mikopo cha Ngome (Ngome Saccos), kila mwanachama anatakiwa kuchangia kiasi kidogo cha fedha ili kufanikisha mpango
huo.
"Kuanzishwa kwa benki ya jeshi kutaweza kusaidia kuwapatia mikopo ya riba nafuu kwa ajili ya kuendeleza shughuli za ujasiriamali, kutokana na hali hiyo tumepanga kupitisha michango ya wanachama," alisema. Aliendelea kuwa kutokana na hali hiyo, mkutano huo utawasaidia kuelimisha wanajeshi na watumishi wa umma, ili kujiunga kwenye Saccos hiyo ambayo itawakomboa.
Alitoa mfano wa nchi ya Rwanda ambayo wanajeshi wake wamepiga hatua ya maendeleo kutokana na kuanzishwa kwa benki hiyo na kwamba, imetoa mikopo kwa wanajeshi na watumishi wa umma, suala ambalo kwa Tanzania inawezekana.
Alisema mara nyingi wamekuwa wakipata mikopo kutoka Benki ya CRDB ili kukuza mitaji ya biashara, jambo ambalo mpaka sasa limewasaidia kupiga hatua. Hata hivyo, Meneja Mkuu wa Benki ya CRDB, Sebastian Masaki, alisema wamekuwa wakifanya kazi na Ngome Saccos kwa miaka mingi, jambo ambalo limesaidia kuwaongeza idadi ya wanachama na mitaji yao.
Ngome Saccos ni miongoni mwa taasisi 500 ambazo tunafanya nazo kazi na kwamba, wamekuwa wakilipa mikopo yao kwa wakati, jambo ambalo linatufanya tuweze kushirikiana nao kwa ukaribu," alisema Masaki.
Akizungumza kwenye mkutano wa kuhamasisha shughuli za ujasiriamali ndani ya jeshi hilo Dar es Salaam jana, Mkuu wa Operesheni na Mafunzo, Meja Jenerali Sylvester Rioba, alisema hivi sasa wana mtaji wa Sh1.7 bilioni na kwamba, wanahitaji Sh15 bilioni ili kutekeleza azma hiyo.
Jenerali Rioba alisema kutokana na hali hiyo, fedha hizo zitapatikana kwenye michango ya wanachama wa Chama cha Akiba na Mikopo cha Ngome (Ngome Saccos), kila mwanachama anatakiwa kuchangia kiasi kidogo cha fedha ili kufanikisha mpango
huo.
"Kuanzishwa kwa benki ya jeshi kutaweza kusaidia kuwapatia mikopo ya riba nafuu kwa ajili ya kuendeleza shughuli za ujasiriamali, kutokana na hali hiyo tumepanga kupitisha michango ya wanachama," alisema. Aliendelea kuwa kutokana na hali hiyo, mkutano huo utawasaidia kuelimisha wanajeshi na watumishi wa umma, ili kujiunga kwenye Saccos hiyo ambayo itawakomboa.
Alitoa mfano wa nchi ya Rwanda ambayo wanajeshi wake wamepiga hatua ya maendeleo kutokana na kuanzishwa kwa benki hiyo na kwamba, imetoa mikopo kwa wanajeshi na watumishi wa umma, suala ambalo kwa Tanzania inawezekana.
Alisema mara nyingi wamekuwa wakipata mikopo kutoka Benki ya CRDB ili kukuza mitaji ya biashara, jambo ambalo mpaka sasa limewasaidia kupiga hatua. Hata hivyo, Meneja Mkuu wa Benki ya CRDB, Sebastian Masaki, alisema wamekuwa wakifanya kazi na Ngome Saccos kwa miaka mingi, jambo ambalo limesaidia kuwaongeza idadi ya wanachama na mitaji yao.
Ngome Saccos ni miongoni mwa taasisi 500 ambazo tunafanya nazo kazi na kwamba, wamekuwa wakilipa mikopo yao kwa wakati, jambo ambalo linatufanya tuweze kushirikiana nao kwa ukaribu," alisema Masaki.