Juzi kati Mtanzania alikamatwa kwa kubaka mbuzi, haya mwingine amebaka nguruwe, kuna uhaba gani huko bandugu

MK254

JF-Expert Member
May 11, 2013
31,757
48,407
MKAZI wa Kijiji cha Mavanga kilichopo katika kata ya Mavanga wilayani Ludewa mkoani Njombe anayefahamika kwa jina la Afro Nyigu (31) anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma ya kumbaka mnyama aina ya Nguruwe.

Afisa mtendaji wa kijiji hicho Ramadhani Kihanga amesema kuwa tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia November 14 2021 ambapo mtuhumiwa huyo alifika katika machinjio ya wanyama hao huku akiwa amelewa na kukuta nguruwe akiwa amefungwa kamba kwa maandalizi ya kuchinjwa ndipo kijana huyo alimvamia na kufanya nae mapenzi.

Amesema wakati akiendelea na tendo hilo mlinzi wa machinjio hiyo alikuwa ametoka kidogo na aliporejea alimkuta kijana huyo akiendelea kufanya kitendo hicho ambapo alimkamata na kumpigia simu balozi na mtendaji wa kijiji ambao walifika katika eneo hilo la tukio.

Amesema kuwa walipomuhoji kijana huyo sababu za kufanya kitendo hicho alidai ni maamuzi yake binafsi hivyo hapaswi kuulizwa ambapo viongozi hao wakamchukua na kumkabidhi mikononi mwa polisi.

“Kitendo alichokifanya huyu kijana mwenzetu ni cha kusikitisha sana! Tunaomba sheria ichukue mkondo wake ili iwe fundisho kwa wengine maana kama ameweza kufanya hivi kwa mnyama anaweza kufanya uharibifu hata kwa binadamu,” amesema Kihanga.

Akizungumza kamanda wa jeshi la Polisi mkoani Njombe Hamiss Issa na mtandao huu amesema ni kweli tukio hilo lipo na kwa sasa Jeshi la Polisi linafanya uchunguzi wa tukio hilo na mtuhumiwa amehifadhiwa katika kituo cha Polisi.
 
MKAZI wa Kijiji cha Mavanga kilichopo katika kata ya Mavanga wilayani Ludewa mkoani Njombe anayefahamika kwa jina la Afro Nyigu (31) anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma ya kumbaka mnyama aina ya Nguruwe.

Afisa mtendaji wa kijiji hicho Ramadhani Kihanga amesema kuwa tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia November 14 2021 ambapo mtuhumiwa huyo alifika katika machinjio ya wanyama hao huku akiwa amelewa na kukuta nguruwe akiwa amefungwa kamba kwa maandalizi ya kuchinjwa ndipo kijana huyo alimvamia na kufanya nae mapenzi.

Amesema wakati akiendelea na tendo hilo mlinzi wa machinjio hiyo alikuwa ametoka kidogo na aliporejea alimkuta kijana huyo akiendelea kufanya kitendo hicho ambapo alimkamata na kumpigia simu balozi na mtendaji wa kijiji ambao walifika katika eneo hilo la tukio.

Amesema kuwa walipomuhoji kijana huyo sababu za kufanya kitendo hicho alidai ni maamuzi yake binafsi hivyo hapaswi kuulizwa ambapo viongozi hao wakamchukua na kumkabidhi mikononi mwa polisi.

“Kitendo alichokifanya huyu kijana mwenzetu ni cha kusikitisha sana! Tunaomba sheria ichukue mkondo wake ili iwe fundisho kwa wengine maana kama ameweza kufanya hivi kwa mnyama anaweza kufanya uharibifu hata kwa binadamu,” amesema Kihanga.

Akizungumza kamanda wa jeshi la Polisi mkoani Njombe Hamiss Issa na mtandao huu amesema ni kweli tukio hilo lipo na kwa sasa Jeshi la Polisi linafanya uchunguzi wa tukio hilo na mtuhumiwa amehifadhiwa katika kituo cha Polisi.
Kenya ndo kunatisha sasa
 
Kenya ndo kunatisha sasa

Awamu hii ya sita naona vyombo vya habari vimepewa ruksa ya kutangaza uchafu wenu wote, awamu ya tano matukio kama haya mlikua mnayaficha chini kwa chini, juzi nimeona hata zile taarifa za kunyofoa viungo vya albino zimeanza kuripotiwa, hapafichwi kitu tena.
 
Back
Top Bottom