Justice & Respect in Mining

mstahiki

JF-Expert Member
Jul 14, 2007
308
5
Ripoti kuhusu uchimbaji wa dhahabu ambayo hivi karibuni imekuwa ikijadiliwa sana kwenye vyombo vya habari. Kama ilivyo ripoti ya Richmond, hii ni ripoti ambayo kila mtu anayewatakia mema watanzania na vizazi vyao vijavyo anapaswa kuisoma na kuifanyia kazi. Kwa ufupi, haya ndiyo baadhi ya masuala yaliyonigusa ndani ya ripoti hii na ambayo ningependa kuyafahamu/kuyafuatilia kwa undani zaidi:



1. Ardhi yetu ina dhahabu yenye uzito wa 'aunsi' milioni 45 na madini haya adimu yanachimbwa kwa kasi ya takribani 'aunsi' milioni 1.6 kwa mwaka.

2. Kasi hii mpya ya uchimbaji iliyosababishwa na kuwavutia/karibisha wawekezaji inatosha kumaliza hifadhi yetu yote ya dhahabu baada ya miaka 28.

3. Migodi 6 mikubwa ya dhahabu nchini inatazamiwa kufungwa rasmi baada ya miaka 10 maana kwa kasi hii dhahabu yote itakuwa imeshachimbwa.

4. Pamoja na kasi yote hii kwa kipindi cha miaka 5 iliyopita serikali yetu imepata dola milioni 21.7 tu kati ya dola bilioni 2.5 za mauzo ya dhahabu nje.

5. Kuyapa makampuni makubwa ya kimataifa fursa nyeti ya kuchimba dhahabu kumesababisha wachimbaji wadogowadogo 400,000 kupoteza ajira.

6. 'Taasisi' ya Umoja wa Mataifa ya Biashara na Maendeleo (UNCTAD) inakadiria kuwa sekta ya madini nchini inaajiri 0.2% tu ya 'nguvukazi' yetu.

7. Vifungu vya mkataba wa kukagua mahesabu ya makampuni ya uchimbaji vinaizuia kampuni ya ukaguzi ya Alex Stewart Assayers kutoa ripoti yao.

8. Mrahaba wa 3% unatupatia wastani wa dola milioni 17. 4 kwa mwaka ila ungekuwa 10% kama ilivyo Botswana tungepata dola milioni 300 zaidi.

9. Rekodi zinaonesha kuwa serikali haijalipwa kodi ya makampuni, ya 30% ya faida zao, kwa sababu makampuni hayo eti yanadai hayajapata faida.

10. Benki ya Dunia ndiyo 'ilitushauri' mwaka 1992 na 'kutufadhili' mwaka 1997 ili tuanzishe mradi wa kuanzisha/kuendeleza sekta 'binafsi' ya madini.



Ripoti hii inadhihirisha kuwa ulegezaji wa uchumi tuliouanza kwa shingo upande katika miaka ya 80 na kuuendeleza kwa kasi ya ajabu katika miaka 90 ndio umetufikisha hapa. Wakati ndio huu wa kuzipitia upya sera na programu za uchumi wa soko huria 'tulizokopeshwa' na Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa kabla hali haijawa mbaya zaidi. Pengine 'kichwa cha ripoti' kinamaanisha kuwa hii ni 'fursa ya dhahabu' ya kutunusuru.


NBNtaambatarisha RIPOTI yenyewe soon....INATISHA
 
Ripoti kuhusu uchimbaji wa dhahabu Ripoti hii inadhihirisha kuwa ulegezaji wa uchumi tuliouanza kwa shingo upande katika miaka ya 80 na kuuendeleza kwa kasi ya ajabu katika miaka 90 ndio umetufikisha hapa. Wakati ndio huu wa kuzipitia upya sera na programu za uchumi wa soko huria 'tulizokopeshwa' na Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa kabla hali haijawa mbaya zaidi. Pengine 'kichwa cha ripoti' kinamaanisha kuwa hii ni 'fursa ya dhahabu' ya kutunusuru.


NBNtaambatarisha RIPOTI yenyewe soon....INATISHA[/FONT]


Naomba ripoti hiyo Mstahiki, hivi ndiyo vitu tunavyotaka kujadili siyo hayo mambo ya kufeli masomo nk.

Tanzania ni nchi ya tatu (3) katika bara la Afrika kwa kuzalisha dhahabu. More ever dhahabu imepanda bei sana katika kipindi hiki. Nchi zinazo zalisha dhahabu uchumi wao ni mzuri hasa zile zenye amani. Kwanini Tanzania tusiwe nchi tajiri kwa kupitia rasilimali tuliyo pewa na Mungu? You must remember that, minerals are not renewable resourses, once exploitated ndiyo imetoka.

Jamani Tanzania tunanini? mbona Mungu katubariki sana? kwanini tuibiwe mali zetu mchana? hawa viongozi wetu wanashindwa nini kuleta mageuzi? wanapewa nini hawa na wazungu hao wa canada nk?.

Hili halivumiliki!!!!!
 
Gold hits $1,000 for first time

The price of gold reached a record, trading at $1,000 an ounce for the first time, pushed higher by a weak US dollar and fears about the US economy.
Concerns about a possible US recession are seeing investors buy up commodities such as gold as an alternative to company shares and the US dollar.
Since the beginning of the year the value of gold has increased by about 20%, after it rose 32% in 2007.
Gold eventually settled for the day at $993.80, up $13.30 an ounce.
Analysts say gold will stay high as long as dollar and growth fears remain.
"Every bit of bad US economic data boosts gold in two ways," said Fortis Bank.
"First because it reinforces the return of its role as a safe-haven asset, and second because the dollar falls on expectations of further Federal Reserve rate cuts."
Gold is measured and sold in troy ounces. One troy ounce equals 31.1035 grams or 480 grains. One troy ounce is equal to 1.09711 avoirdupois ounce - those widely used to measure weights in the US and UK.

Story from BBC NEWS:
http://news.bbc.co.uk/go/pr/fr/-/2/hi/business/7294040.stm

Published: 2008/03/13 21:36:16 GMT

HIYO NDIYO BEI YA DHAHABU KWA SASA KWENYE SOKO LA DUNIA. JARIBU KULINGANISHA BEI HIYO, KIWANGO CHA DEPOSIT KILICHOPO NA UMASKINI WA WATANZANIA!.
 
Wanafanya hivyo ili mikataba itakapoangaliwa upya na SK ya Muungwana, sijui mwaka gani, na kama wataamua kuibadilisha ili kuhakikisha Watanzania tunafaidika na rasilimali zetu, basi wawe wameshamaliza dhahabu yote au iliyobaki iwe ni kidogo sana.
 
mstahiki:
Asante sana kwa hoja hii.

Hiyo namba saba inakatisha tamaa kabisa:
"Vifungu vya mkataba wa kukagua mahesabu ya makampuni ya uchimbaji vinaizuia kampuni ya ukaguzi ya Alex Stewart Assayers kutoa ripoti yao."

Ni mtumishi wa namna gani wa serikali yetu tukufu anayeweza kujadili na kufikia maafikiano ya namna hii?
Halafu, huyo mkaguzi analipwa asilimia 1.9 kati ya ule mrahaba wa asilimia 3; kwa ripoti ambayo ni siri kubwa!

Halafu tunasema hawa wananchi wenzetu wanaitakia mema nchi yetu.
 
kwa mikataba kama hii ndo pale unakuta watu wansema hata hizo rasilimali zinazogunduliwa sasa kama mafuta yasichimbwe kwanza. mpaka tutapoweza kuweka mikataba yenye maslahi kwa taifa.
ni aibu, na inashangaza kuwa aibu hiyo tunaiona sie wananchi na sio viongozi.
kweli wizi unaziba watu macho!
 
Halafu ndio Ngurdoto anataka tuache kujadili haya mambo ili wale kwa mapozi. Tutaendelea kuwazodoa angalau wakila na watoto wao wajue kwamba tunawaona na tunajua wameiba japokuwa wao wameshika mpini, kuna siku watashika makali,hakuna kulala hapa...
 
Hakuna kizazi cha viongozi ambao hawana uchungu na nchi yao kama kizazi kilichopo sasa madarakani.

Yaani watu hawaoni aibu kuinadi nchi kwa vijiten % vya kipumbavu tuu bila kungalia impact ya ayafanyayo siku za mbele.

Upumbavu huu.

Inauma pale wajukuu zetu watakapokuwa hawana ata deposits na kuanza kusoma kwenye historia tz ilikuwa ya tatu ktk ili bila kufaid matunda yake.

Ivi hawa viongozi wetu izi data wanazo na kama wanzo mbona sioni initiatives.

Nchi ilishaharibika toka enzi za Mkapa as a result ten % imekuwa ni sehemu ya maisha ya watu.

Ubunafsi...Ubinafsi..........Ubinafsi.....utatupeleka pabaya jamani.
Ebu tuwaonee huruma watz wanaotaabika vijijini mlo mmoja,dawa hakuna.Tena uku wakiamini kuna wasomi wanawatetea kumbe ndo mabogus
Nsije tukana bure naomba niishie apa
 
Mkuu Mstahiki mbona hivyo? kwanini usizimwage hapa hizo data kama ulivyo ahidi? kuna sababu gani ya kumtumia mtu mmoja mmoja kwenye E mail yake? The best is to display it here.

Nimeshakutumia kwenye email yako...sikuweza kuiattach hapa nsio maana nimekutumia...Still more Habari MOTO to come...Stay tuned wajomba mambo yanatisha sana..Mliopo ughaibuli rudini BONGO mje kutusaidia kuokoa NCHI yetu..
 
Kuna kipande kinasema


Box 4: Poverty reduction through small scale mining
A 2004 report for the British government’s Department for International Development states
that ASM (small-scale artisan mining) ‘has considerable potential to reduce poverty… what
emerges from the study is that income from mining, particularly gold mining, is a more regular
source of income than from [sic] other livelihood sources, such as agriculture, and it has been
instrumental in reducing household food shortages… It also generates numerous opportunities
for employment, however backbreaking and menial… There are therefore strong indications that
if ASM is given due attention by authorities it could offer opportunities for self-suffi ciency of
communities and reduce dependence on government’123. In Geita district, near the AGA mine, it
is commonly estimated that an average small-scale miner wins about one half a gram of gold per
day worked, earning about US$6 a day on average, or US$120 a month124 - this is four and a half
times the average income.
 
quote:

The researchers estimate that mining companies have earned about USD2.5 billions from exports but Tanzania only records about USD100 million from gold earnings. The researchers estimate that Tanzania is loosing more than USD400 million from tax concessions as well as tax evasion e.g. non payment of corporation tax and waivers on income tax on expatriate workers
 
Can anyone share with us this report if they have it?

According to the report, a total of $3 billion was taken out of the country by mining investors while $400 million was lost due to tax incentives offered to mining companies. A further $700 million, according to the report, was lost in dubious circumstances, mainly because of lack of key documents. The report shows that the country exported gold worth more than $2.5 billion in the past five years while it has received an average of only $21.7 million a year in royalties and taxes on these exports, which is less than 10 per cent of the annual total value. On average, the three per cent royalty earns the Government about $17.4 million a year, and raising the royalty to 5 per cent would have increased Government revenue by $ 61 million in the past seven years. An increase to 7.5 per cent would have increased revenue by $131 million, while an increase to 10 per cent, would have earned the country over $300 million per year.
 
Kuna vitu vichache tunatakiwa tuvibadilishe kwenye mada hii. Moja ni kuhusu na kiasi cha ounce kilichopo ardhini. Kiasi ulichoandika ni cha Bulyanhulu + Geita. kwani Buly walikuwa na ounce 30mil na Geita kulikuwa na ounce 15mil kabla ya mavumbuzi mapya. hiyo ni kusema kiasi cha ounce kitakuwa kimeshaongezeka kwani kwani tafiti zinaendelea katika maeneo yao.
Kwa sababu hiyo ni kwamba ardhi yetu ina kiwango kikubwa cha ounce zaidi ya hizo zilizoainishwa hapo juu. kwani kuna deposit nyingine nyingi ambazo hazijaingizwa kwenye utajiri tulionao.
Suala la wachimbaji wadogo wadogo mimi naona si vema kulizungumzia kwani nimekaa nao na inaonekana kutetea wachimbaji wadogo wadogo ni kutetea ukoloni. Sababu kubwa ni kwamba ukiangali kazi ya mchimbaji mdogo na hali ya maisha yake ni tofauti na ukimuangali mnunuzi wake na wale ma-quarter ambao ndo wauzaji wakubwa wa hizo dhahabu.
Kuna siri kubwa imejificha kwenye machimbo kwani hata kuna ajali wanazozipata na kupoteza maisha na inakuwa siri kubwa kwani hakuna ripoti yoyote inayotolewa.

Suala la makampuni si tatizo kwangu ila tatizo langu ni kwa sera za nchi yangu na viongozi wangu. Nadhani kuna kila haja ya wahusika kuangalia njia mbadala na kuiwezesha nchi kufaidika na kile kilichopo. Kama wenzetu wameweza sisi itakuwaje?
 
Je idara ya utunzaji kumbukumbu au takwimu ipo? Na je inafanzaje kazi zake na nani ni mkurugenzi au kamishna?

Na hapo nafikiri ndipo pa kupata kila kitu kuhusu mstakabali mzima kuhusu madini ya Tanzania, nani anafanza nini kuhusu madini hayo na nani anafaidika na anafaidikaje.

Vipi kuhusu "freedom of information", serikali inasemaje hapo je inaruhusu watu kujua inafanzaje mambo yake au ndio inaendelea kuwa siri?
 
Kuna vitu vichache tunatakiwa tuvibadilishe kwenye mada hii. Moja ni kuhusu na kiasi cha ounce kilichopo ardhini. Kiasi ulichoandika ni cha Bulyanhulu + Geita. kwani Buly walikuwa na ounce 30mil na Geita kulikuwa na ounce 15mil kabla ya mavumbuzi mapya. hiyo ni kusema kiasi cha ounce kitakuwa kimeshaongezeka kwani kwani tafiti zinaendelea katika maeneo yao.
Kwa sababu hiyo ni kwamba ardhi yetu ina kiwango kikubwa cha ounce zaidi ya hizo zilizoainishwa hapo juu. kwani kuna deposit nyingine nyingi ambazo hazijaingizwa kwenye utajiri tulionao.
Suala la wachimbaji wadogo wadogo mimi naona si vema kulizungumzia kwani nimekaa nao na inaonekana kutetea wachimbaji wadogo wadogo ni kutetea ukoloni. Sababu kubwa ni kwamba ukiangali kazi ya mchimbaji mdogo na hali ya maisha yake ni tofauti na ukimuangali mnunuzi wake na wale ma-quarter ambao ndo wauzaji wakubwa wa hizo dhahabu.
Kuna siri kubwa imejificha kwenye machimbo kwani hata kuna ajali wanazozipata na kupoteza maisha na inakuwa siri kubwa kwani hakuna ripoti yoyote inayotolewa.

Suala la makampuni si tatizo kwangu ila tatizo langu ni kwa sera za nchi yangu na viongozi wangu. Nadhani kuna kila haja ya wahusika kuangalia njia mbadala na kuiwezesha nchi kufaidika na kile kilichopo. Kama wenzetu wameweza sisi itakuwaje?


Ngonalugali,

Heshima yako mkuu,

Mimi juzijuzi kuna mtu amenipa data ambazo nimeona ni muhimu kuzijadili hapa JF ili kama kuna mwenye ufahamu wake basi naomba anieleweshe kwa ufasaha.

Huyu jamaa ambae naona nimweke kama "primary source" yangu ya habari anafanya kazi pale idara ya ardhi na yupo pale kwa muda mrefu sana hivo kuwa na uzoefu mkubwa na masuala yote yanayohusu mambo ya ardhi, mipango miji na kadhalika.

Jambo moja ambalo ameniambia ni kwamba wazungu kabla ya uhuru, walikuwa wametayarisha michoro yote muhimu ikiwemo ya wapi yalipo madini nchini Tanzania.

Michoro mingine kwa mfano ni ile ambayo inasema wapi yapo mafuta na kadhalika kwa nchi zingine kama Iraq ambapo inakuwa rahisi kuvamia baadae.

Sasa kuhusu michoro ya wapi yapo madini na ni ya aina gani, wapi kuna uwezekano wa kupata madini mengine na kadhalika yote hayo ama bado wanayo au wanakuwa wanawasiliana na watu wa serikali na hapo ndio "Buzwagi style of contract" inaandaliwa na mwishowe kusainiwa tayari kuipa kampuni husika haki ya miaka zaidi ya ishirini kuchimba madini hayo.

Sasa kwa mawaziri, wataalam na wasomi wengine wafanzao kazi serikalini na kwa ujumla watu wote walioko katika "visual circle" ya hujuma, wanakuwa wanashirikiana kuiba mali ya nchi kwa ushirikiano na hao wachimbaji wakubwa.

Kwa ufupi hii ndio dondoo ya jamaa ambae yeye jina lake sio kubwa saaana na anaendelea kufanza kazi yake pale ardhi.

Hivo watanzania tuna kazi kubwa ya kukomboka kutoka katika lindi la umaskini kama mambo yenyewe ndio haya.

NB:

Kuna mtu yeyote yupo na data zaidi kuhusu hii hoja yangu achangie?
 
Mining.JPG


Contents
  1. Foreword by the religious councils of Tanzania
  2. Executive Summary
  3. About the authors
  4. INTRODUCTION
  5. CHAPTER 1 – TAX REVENUES FROM GOLD MINING
  6. Tax payments
  7. Royalties
  8. Corporation tax and company profits
  9. Tax evasion
  10. Tanzania’s lost income
  11. The government’s mining review and its forked tongue
  12. The Buzwagi contract. Reform? What reform?
  13. International comparisons
  14. The state of the reserves – is time running out?
  15. CHAPTER 2 – DEMOCRACY AND CORRUPTION
  16. CHAPTER 3 – LOCAL ECONOMIC DEVELOPMENT
  17. Local employment
  18. Discrimination against Tanzanians?
  19. Buying local goods and services?
  20. ‘Community development’ spending
  21. Harnessing mining to development?
  22. RECOMMENDATIONS
  23. REFERENCES
  24. ACRONYMS
  25. GLOSSARY
 
Back
Top Bottom