Jussa na Zanzibar huru, ndani ya CNN - Inside Africa

Pulpitis

Senior Member
Jun 24, 2012
116
26
Wadau leo katika kipindi cha inside Africa, ndani ya kituo cha CNN, mmoja wa wadau waliokuwa wanafanyiwa interview ni Ismail Jussa, anasema Zanzibar lazima irudishiwe sovereignty yake iliyopotea na wawe huru na huu ni msimamo wa vyama vikuu viwili huko Zanzibar, CCM na CUF.

May take:

Je, CCM na CUF bara ni tofauti na zile za Zanzibar? Mbona misimamo ni tofauti?
 
naona kaamua kuanzisha filam, wacha tuone mwisho wake...
 
Nimemuona juzi na alimpromis Erol Bennet kwamba hatazungumzia politics but mwishoni akasema Zanzibar lazima iwe nchi huru! I think theres nothing can be done, na kwa hali hii ya kuchoma makanisa, tumwombe Mungu sana
 
Wadau leo katika kipindi cha inside Africa, ndani ya kituo cha CNN, mmoja wa wadau waliokuwa wanafanyiwa interview ni Ismail Jussa, anasema Zanzibar lazima irudishiwe sovereignty yake iliyopotea na wawe huru na huu ni msimamo wa vyama vikuu viwili huko Zanzibar, CCM na CUF.

May take:

Je, CCM na CUF bara ni tofauti na zile za Zanzibar? Mbona misimamo ni tofauti?

Baada ya kuungana na CUF na kuunda serekali wanaona sasa watake serekali yao ambayo wanayo tu wala haiko kwa muungano,halafu wakisha jitenga watasema wanataka Unguja yao na Pemba yao and so on......mwishoni watakuta wanataka koo zao n.k yetu macho kwani Nyerere alishaona hayo siku nyingi sana
 
Mkuu TUKUTUKU, sasa vipi msimamo wa CUF bara? Labda tuseme Jussa kaongopea umma kuhusu cuf na ccm zanzibar lao moja, sasa ni upi msimamo wa CUF bara, na wabunge wao walio ndani ya bunge la muungano,?
 
hivi jussa kwanini amejiuzulu unaibu katibu mkuu cuf znz?
kwanini hakupewa uwaziri smz wakari ameplay big role ktk ushindi cuf znz!
kwanini jk akumpatia ubunge wakuteuliwa kama 2005-2010 alivyopewa?
 
Kwasababu hii ya kutaka kuitetea zanzibar ka kituo:

[h=5]Sasa sikilizeni hivyo alivyo umbuliwa Mhe Ismail Jussa kunako semwa na magazeti ya Tanzania bara na wengi wakawa kama makasuku kkuyakariri ya magazeti kama jukwaa la Jamii Forum. sikilizeni kwa makini baada ya kusha kutowa maoni yake, Jaji warioba na babu butiku walipoanza kujikanyaga. Watu wazima, wenye uzoefu wa sikunyingi kuadhirishwa na kijana mdogo wa miaka arubaini (40). Kutokana na umbri wao huyu ni sawa na mtoto wao....Kamati ya Maridhiano Six: MAONI YA WAWAKILISHI KWA TUME YA KATIBA; 14/10/12; Part 5 - YouTube


[/h]
 
hIVI KILICHOMFANYA MAALIM KUFUNGWA JELA NA HIKI CHA JUSSA KUNA TOFAUTI GANI??


HUU SIO UHAINI??

BTW, SIPENDI MUUNGANO KWA MOYO WANGU WOTE... NINGEPENDA TUISHI NA ZANZIBAR KAMA NCI JIRANI, YENYE TARATIBU ZAKE ILI HATA HESHIMA ZAIDI IWEPO
 
AllyZenj, Janjaweed, Nguruvi3,

..tatizo la Jussa ni kucheza-cheza na maneno.

..Jussa anashindwa kuwa mkweli anaposema kutakuwepo na "muungano wa mkataba."

..ukweli ni kwamba kutakuwepo na mkataba/mikataba, lakini hatukuwepo na muungano tena.

..ingependeza kama Jussa angesema wazi kwamba tunataka kuvunja muungano, na badala yake tuwe na mikataba mbalimbali, mfano ulinzi, uhamiaji, biashara, etc etc.

..Jussa angeeleza hivyo, wala asingeingia ktk malumbano na Mzee Joseph Warioba.

NB:

..hii ni mara ya kwanza kwa Jussa kuzungumza hoja zake ktk kadamnasi inayoshirikisha wa-Tanganyika.

..maswali aliyoulizwa na Mzee Warioba na Mzee Butiku ndiyo ambayo wengi tumekuwa tukiuliza hapa JF.
 
Jussa amekuwa wazi na amesema kabisa kwamba yeye hagusii shirikishi na akasema wazi kabisa kamba hakutakuwa na serikali ya Muungano badala yake kutakuwa na mashirikiano. Muungano sio lazima huu tulio nao. Wa EAC pia ni muungano, wa EU ni muungano na wengine wanweza kuwa na muungano kwa mambo fulani fulani kama ilivyo kwa EU wengine wanataka sarafu ni uhuru wako.

Warioba na wafuasi au waumini wa Muungano huu wanasema kufanya hivyo anavyotaka yeye lazima kuvunja. Kama kweli sisi ni ndugu kwanini ishindikane kukaa pamoja kama ndugu tukaamua kuanzia kesho tunakuwa na mahusiano haya na haya. Kuna mambo kadhaa wa kadhaa ambayo nyerere akiyafanya kwa siku moja tu, yanapitishwa kwenye bunge siku ya pili ihsakua sheria, hata huu muungano wenyewe kwenye miezi mitatu haraka haraka tayari tunaaambiwa tuna muungano, hafla ati atanganyika ikauliwa ikawa Tanzania, katiba yake ikatiwa viraka ikawa ya Jamuhuri ya watu wa Tanzania.... mwisho mwisho wa katiba hiyo ikaengezewa mambo ya Muungano.
 
AllyZenj,

..EAC siyo muungano, bali ni JUMUIYA.

..ndiyo maana wengine tunasema Jussa is not being 100% honest.

..yeye aseme wazi tu kwamba tutakuwa na mikataba kadha wa kadhaa, na siyo kuleta dhana potofu kwamba kuna kitu kama "muungano wa mkataba."

..Off course sisi ni ndugu, lakini wenzetu wa Zanzibar mna ubinafsi mno. Kwa mfano kuna mwakilishi alikuwa analalamika kwamba wa-Tanganyika wanakwenda Zanzibar kuuza dawa za mbu. Sasa labda tuulize: je, hiyo siyo shughuli halali huko Zanzibar? Zaidi, kama Zanzibar haiwezi ku-attract wafanyabiashara wakubwa, au wataalamu toka Tanganyika, je ni nani wa kulaumiwa? Pia mbona hakusema kuhusu mishahara na umeme wa bure ambao wa-Tanganyika huwapa wa-Zanzibari?
 
Last edited by a moderator:
katumia paltforma vibaya ya CNN,kama Barret atapenda weka hicho kipande poa.Ila soon Jussa atabaki kama mshenzi tuu.Akikutana na watu wa kutosha kama warioba biashara yake itakuwa kama ya Lipumba tuu.
 
Kumbe wanaogopa kuvunja muungano. Teh teh teh, sasa mpambanaji gani sasa huyo, kumbe ndiyo maana nimeelewa kwanini muungano haujavunjika. Jussa mchovu sana
 
Back
Top Bottom