Jussa na wawakilishi wenzake wasema kama Muungano uwepo basi ni wa mkataba kila nchi kuwa na Malaka

Mkuu, Jussa sio Mbunge, hawezi kupeleka hoja yake kwenye Bunge la Muungano.

Kwenye Baraza la Wawakilishi haya mambo anayaongea kila wakati. Lakini yeye ni mwakilishi wa chama minority, hoja za minority mara nyingi zinazidiwa na nguvu ya namba. CCM, the majority hawataki muungano uvunjike, sababu CCM nayo itabidi ivunjike.

Ndio maana anafanya jitihada za kuzitoa hoja zake nje ya bunge, ku sensitive wananchi. Namuunga mkono asilimia 100, ni mkombozi wa wenzake Wanzanzibari na sisi pia Watanganyika.

Tunataka kila upande uwe ni dola huru yenye mamlaka yake kamili, ndani na nje ya nchi.
Taso,

..kama umesikiliza mahojiano ya Jussa na aljazeera, amekiri kwamba Baraza la Wawakilishi lina mamlaka ya kuitisha referendum kuhusu muungano.

..kutokana na ukweli huo ndiyo maana baadhi yetu tumekuwa tunasisitiza kwamba suala hili lishughuliki haraka, sasa hivi, na BARAZA LA WAWAKILISHI.

..anachotakiwa kufanya Jussa siyo "kuyaongelea" tu masuala ya muungano, anatakiwa awasilishe hoja binafsi inayopendekeza Zanzibar ipewe FULL AUTONOMY, na kuwepo kwa "muungano wa mkataba."

..nadhani unakosea unapodhani kwamba Jussa anatutakia mema wa-Tanganyika. Kuwa makini sana na hayo mapendekezo ya "muungano wa mkataba." Hiyo ni hila tu ya wanasiasa wa Zanzibar kuendelea kuinyonya Tanganyika.
 
Last edited by a moderator:
..nadhani unakosea unapodhani kwamba Jussa anatutakia mema wa-Tanganyika. Kuwa makini sana na hayo mapendekezo ya "muungano wa mkataba." Hiyo ni hila tu ya wanasiasa wa Zanzibar kuendelea kuinyonya Tanganyika.
Okay Mkuu, ni kweli kabisa "Muungano wa Mkataba" unaweza kuwa ni nefarious agenda ya Wazanzibari kuendelea kutunyonya.

I have a two-fold reason for supporting that approach anyway. Kwanza ujue Watanzania (Bara na Visiwani) ambao kwa kweli hawataki Muungano tuko kama kumi na tano hivi, hatujai sebuleni! Kwa hiyo kuwa convince hawa super majority wakubaliane nasi kuuchukia Muungano ndio inabidi sasa tuwadanganye kwamba jamani eeh Muungano utaendelea kuwepo, lakini wa mkataba. Kitu ambacho si kweli, kitakachokuwepo ni jumuiya au umoja, sio Muungano, Muungano wa Mkataba hata huu wa sasa una mkataba! So it is just an end-run toward reaching the ultimate goal, kuwafanya Watanzania wakubali kuvunja Muungano bila wao kujua, kwa sababu Watanzania wamelala, hawajui Muungano hautufai, hasa hasa wa huku kwetu nchi kavu huku, ndio kuna matatizo zaidi ya usingizi.

Lakini kingine kinachonigusa zaidi, kinachoniuma zaidi Jokakuu, ni unaposema - ambacho ni kweli - kwamba eti kwenye huo mkataba mpya sisi Bara tutanyonywa. Yani mkataba haujaandikwa lakini Watanzania tushajua tutalaliwa! Hahahaaa.... Nataka kuukataa huo ukweli! Sitaki kuwaogopa Wazanzibar kwenye meza ya majadiliano ya mkataba! Jamani, Wazanzibar wamesoma wapi sheria kama sio University of Dar-es-Salaam? Kitaalam na kitaaluma huwa tunakiri tunawaogopa Wakenya, sasa mpaka Wazanzibar? Kweli Wazanzibar? Wanasheria wa Kiembe-Samaki na Makundu-Uchi? Kuna wataalam gani wa kuandika mikataba Zanzibar ambao hatukuwafundisha sisi kwenye vyuo vyetu Bara?

Ni kweli tunaogopa tutanyonywa kwenye mkataba na Wazanzibar. But why tukubali kunyonywa, sisi Wabara tuna nini vichwani, mashudu?
 
Taso,

..U have made some valid points.

..wa-Tanganyika tuanze kufikiria ni mambo gani tunahitaji toka Zanzibar ili yaingizwe ktk mkataba mpya wa muungano.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom