Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,988
Seif Sharrif na Jussa wasikie vizuri sana;tupo ambao hatutaki Muungano "wa mkataba"! Kama wao na wale wanaowashabikia wanaona kweli Tanganyika inawanyonya na wanataka uhuru kamili njia iko rahisi kabisa.
Wawaondoe wabunge wao kwenye Bunge la Muungano; waitishe kampeni ya Wazanzibari wanaotumikia serikali ya Muungano kuachia nafasi zao (akiwemo Ghaib Bilal) na wajitangazie "uhuru wao".
Lakini la kwanza ni kwa yeye (Seif) kuacha ziara za kisiasa Tanzania bara na kuamua kuvunja CUF ili chama cha siasa cha Wazanzibari watupu kizaliwe.
Hapo ndio tutajua kweli wanataka kuwa huru. Watoke kwanza wawe na Zanzibari yao halafu ndio watuulize kama tunataka Muungano wowote na wao! Siyo watoke halafu wakati huo huo waamue aina ya mkataba wanaoutaka wao!
LET ZANZIBAR GO!
Wawaondoe wabunge wao kwenye Bunge la Muungano; waitishe kampeni ya Wazanzibari wanaotumikia serikali ya Muungano kuachia nafasi zao (akiwemo Ghaib Bilal) na wajitangazie "uhuru wao".
Lakini la kwanza ni kwa yeye (Seif) kuacha ziara za kisiasa Tanzania bara na kuamua kuvunja CUF ili chama cha siasa cha Wazanzibari watupu kizaliwe.
Hapo ndio tutajua kweli wanataka kuwa huru. Watoke kwanza wawe na Zanzibari yao halafu ndio watuulize kama tunataka Muungano wowote na wao! Siyo watoke halafu wakati huo huo waamue aina ya mkataba wanaoutaka wao!
LET ZANZIBAR GO!