Jussa na Seif mnawachelewesha Wazanzibari kuwa "huru kamili"!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,988
Seif Sharrif na Jussa wasikie vizuri sana;tupo ambao hatutaki Muungano "wa mkataba"! Kama wao na wale wanaowashabikia wanaona kweli Tanganyika inawanyonya na wanataka uhuru kamili njia iko rahisi kabisa.

Wawaondoe wabunge wao kwenye Bunge la Muungano; waitishe kampeni ya Wazanzibari wanaotumikia serikali ya Muungano kuachia nafasi zao (akiwemo Ghaib Bilal) na wajitangazie "uhuru wao".

Lakini la kwanza ni kwa yeye (Seif) kuacha ziara za kisiasa Tanzania bara na kuamua kuvunja CUF ili chama cha siasa cha Wazanzibari watupu kizaliwe.

Hapo ndio tutajua kweli wanataka kuwa huru. Watoke kwanza wawe na Zanzibari yao halafu ndio watuulize kama tunataka Muungano wowote na wao! Siyo watoke halafu wakati huo huo waamue aina ya mkataba wanaoutaka wao!


LET ZANZIBAR GO!
 
Umenena ukweli mtupu, kwa sababu haiwezekani Jussa kutudanganya kuwa amejiuzulu nafasi ya ukatibu wa CUF kwa lengo la kutetea na kusimamia muungano wa mkataba wakati huo huo anaendelea kuwa mjumbe katika baraza la uwakilishi bara! Waachie nyadhifa zao zote ndani ya muungano ndipo wadai Z'bar huru wao nao wakiwa huru!
 
Muungano upo kwa maslahi ya ccm bara...ccm zanzibar hakuna muungano bali kuna sisi wazanzibar na wao watanganyika
 
Hatuwahitaji wazanzanzibari wala hatuwalazimishi wawepo katika muungano.

Kama wanataka tuendelee na muungano basi kuwe na serikali moja ili kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na zanzibar iwe ni mkoa katika jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Mipango ya Maendeleo ipangwe kwa usawa kutokana na uwiano wa watu bila kujali umetoka katika sehemu gani ya Jamhuri.

Vinginevyo wana uhuru wa kujiondoa na kujiamulia mambo yao wenyewe. Hatutawafukuza.

Wanasiasa wanaotoa wazo la serikali tatu ni wabinafsi wenye uchu wa madaraka. wanataka serikali tatu ili wapate vyeo vya kisiasa.
 
mkuu mwanakjj umenena. kwani muungano kitu gani bhana. miungano yote iliyoingiwa kidwanzi km wetu ilishavunjika. why not ours?

wazanzibari, its very easy fuateni ushauri wa mwanakjj muwe huru. km mseto mliamua wenyewe bila shuruti toka kokote kule, na hili pia mwaliweza wenyewe. ni uamuzi wenu tu.
 
Seif Sharrif na Jussa wasikie vizuri sana;tupo ambao hatutaki Muungano "wa mkataba"! Kama wao na wale wanaowashabikia wanaona kweli Tanganyika inawanyonya na wanataka uhuru kamili njia iko rahisi kabisa.

Wawaondoe wabunge wao kwenye Bunge la Muungano; waitishe kampeni ya Wazanzibari wanaotumikia serikali ya Muungano kuachia nafasi zao (akiwemo Ghaib Bilal) na wajitangazie "uhuru wao".

Lakini la kwanza ni kwa yeye (Seif) kuacha ziara za kisiasa Tanzania bara na kuamua kuvunja CUF ili chama cha siasa cha Wazanzibari watupu kizaliwe.

Hapo ndio tutajua kweli wanataka kuwa huru. Watoke kwanza wawe na Zanzibari yao halafu ndio watuulize kama tunataka Muungano wowote na wao! Siyo watoke halafu wakati huo huo waamue aina ya mkataba wanaoutaka wao!
LET ZANZIBAR GO!
MM, wanataka ZNZ huru wakiwa na 'strings attached' yaani muungano wa mkataba.
Hapo ndipo ninaposema Maalim na Jusa wanauma maneno na sijui kama Wazanzibar wanjua nini wanataka.

Jusa ni mbunge, kwa vile amejiuzulu uongozi wa CUF ili kuimarisha juhudi za ZNZ huru anapaswa pia ajiuzulu ubunge katika bunge la JMT. Akiendelea kuwa mbunge atakuwa anatafuna si maneno bali matapishi.

Maalim Seif hatakiwi kuja Tanganyika katika mikutano ya kisiasa. Kwa kauli ya ujirani mwema kama Kenya, nasi tunataka ujirani mwema hivyo siasa za CUF mwisho Chumbe. Kama ataendelea kuja katika mikutano, kwanza apuuzwe kwasababu anaongea sichokiamini na watu wasiomhusu. Pili atakuwa amekula matapishi achilia mbali kujiuma uma.

Maalimu Seif na Jusa wavunje kwanza CUF ili wawe na vyama huru vya kizanzibar halafu wavunje muungano. Kama hawawezi kuvunja CUF, wafunge midomo na kukaa kimya kwasababu wanakula matapishi yao na si kujiuma uma.

Wamwite Gharibu na wafanyakazi wote wa muungano kutoka ZNZ, watengeneze Passport za ZNZ haraka haraka na watumie Rupee au dollar kama hatua za kuvunja muungano. Wasipofanya hivyo basi wakipanda katika majukwa waiteni manafiki, vizabi zabina, warongo na wahuni.
 
Jussa and Maalimu Seif...two confused minds. Naona mmoja anataka kuwa Rais wa Zanzibar mpya na mwingine sijui anataka kuwa nani.
 
Week iliyopita Maalif Seif alikuja Arusha kwa ndege/gharama za Tanganyika na kuwaambia vijana wanalewa viroba. Jana alikuwa Pemba (ulinzi kwa gharama ya Tanganyika) kuhutubia ni jinsi gani anataka Zanzibar huru na kuachana na koloni Tanganyika. Kesho Jumanne tunaambiwa atakuwa Bukoba (Tanganyika).

Hivi Maalim Seif anaamini anachosema? Afuatafuata nini Tanganyika? Kwanini asikae chini na kuandaa muswada wa kuachana na koloni? Chama chake (CUF) kina wabunge wengi toka toka Zanzibar kwenye bunge la Muungano, asiwapoge marufuku kuja Dodoma?
 
Seif Sharrif na Jussa wasikie vizuri sana;tupo ambao hatutaki Muungano "wa mkataba"! Kama wao na wale wanaowashabikia wanaona kweli Tanganyika inawanyonya na wanataka uhuru kamili njia iko rahisi kabisa.

Wawaondoe wabunge wao kwenye Bunge la Muungano; waitishe kampeni ya Wazanzibari wanaotumikia serikali ya Muungano kuachia nafasi zao (akiwemo Ghaib Bilal) na wajitangazie "uhuru wao".

Lakini la kwanza ni kwa yeye (Seif) kuacha ziara za kisiasa Tanzania bara na kuamua kuvunja CUF ili chama cha siasa cha Wazanzibari watupu kizaliwe.

Hapo ndio tutajua kweli wanataka kuwa huru. Watoke kwanza wawe na Zanzibari yao halafu ndio watuulize kama tunataka Muungano wowote na wao! Siyo watoke halafu wakati huo huo waamue aina ya mkataba wanaoutaka wao!


LET ZANZIBAR GO!

Mkuu so far sijasikia sababu yeyote ya msingi kutoka kwa Seif Sharif Hamad kuhusu kuvunja Muungano. Ninachoona ni kuwa anataka madaraka tu, anataka awe rais wa Zanzibar halafu awe sultani wa Pemba.

Siku zote anadhani watu wote ni wajinga, na kibaya zaidi anadhani kila mtu anamsikiliza.

Kama kweli yuko serious atenganishe CUF bara na CUF visiwani, na ajitoe kwenye serikali ya muungano kwa kuwa inaifuniza ile ya Zanzibar aanzishe movement ya kuwaondoa wazanzibar wote toka bara na kuwapeleka Zenjibar, hapo tutajua kuwa yuko serious.
 
MM, wanataka ZNZ huru wakiwa na 'strings attached' yaani muungano wa mkataba.
Hapo ndipo ninaposema Maalim na Jusa wanauma maneno na sijui kama Wazanzibar wanjaua nini wanataka.

Jusa ni mbunge, kwa vile amejiuzulu uongozi wa CUF ili kuimarisha juhudi za ZNZ huru anapaswa pia ajiuzulu ubunge katika bunge la JMT. Akiendelea kuwa mbunge atakuwa anatafuna si maneno bali matapishi.

Maalim Seif hatakiwi kuja Tanganyika katika mikutano ya kisiasa. Kwa kauli ya ujirani mwema kama Kenya, nasi tunataka ujirani mwema hivyo siasa za CUF mwisho Chumbe. Kama ataendelea kuja katika mikutano, kwanza apuuzwe kwasababu anaongea sichokiamini na watu wasiomhusu. Pili atakuwa amekula matapishi achilia mbali kujiuma uma.

Maalimu Seif na Jusa wavunje kwanza CUF ili wawe na vyama huru vya kizanzibar halafu wavunje muungano. Kama hawawezi kuvunja CUF, wafunge midomo na kukaa kimya kwasababu wanakula matapishi yao na si kujiuma uma.

Wamwite Gharibu na wafanyakazi wote wa muungano kutoka ZNZ, watengeneze Passport za ZNZ haraka haraka na watumie Rupee au dollar kama hatua za kuvunja muungano. Wasipofanya hivyo basi wakipanda katika majukwa waiteni manafiki, vizabi zabina, warongo na wahuni.

Nimekugongea like... Hawa wanatafuta tu umaarufu kuelekea 2015... Hawana la maana.
 
Seif Sharrif na Jussa wasikie vizuri sana;tupo ambao hatutaki Muungano "wa mkataba"! Kama wao na wale wanaowashabikia wanaona kweli Tanganyika inawanyonya na wanataka uhuru kamili njia iko rahisi kabisa.

Wawaondoe wabunge wao kwenye Bunge la Muungano; waitishe kampeni ya Wazanzibari wanaotumikia serikali ya Muungano kuachia nafasi zao (akiwemo Ghaib Bilal) na wajitangazie "uhuru wao".

Lakini la kwanza ni kwa yeye (Seif) kuacha ziara za kisiasa Tanzania bara na kuamua kuvunja CUF ili chama cha siasa cha Wazanzibari watupu kizaliwe.

Hapo ndio tutajua kweli wanataka kuwa huru. Watoke kwanza wawe na Zanzibari yao halafu ndio watuulize kama tunataka Muungano wowote na wao! Siyo watoke halafu wakati huo huo waamue aina ya mkataba wanaoutaka wao!


LET ZANZIBAR GO!

MKUU MMJ, heshima mbele. Naona umeishiwa hoja, hujui hata ulisemalo. Unapapatika tu, kijiba cha roho kimekukaa. Haaa haa haa.
 
Utashangaa Mtikila wanamfungulia kesi za uchochezi, gazeti la Mwanahalisi likafungiwa kwa uchochezi, wananchi wengi tu wanazo kesi eti ni uchochezi lakini hawa akina Jussa, Seif na wengineo haya wayafanyayo sio uchochezi.

Labda tuseme tafsiri ya sheria zetu ina rangi na dini, lakini kama haina basi hawa jamaa wana kesi zaidi ya moja ya kujibu.

Binafsi nimefika mahali sipendi aina yoyote ya muungano kati ya Tanganyika na hawa wazenj, labda ushirikiano kama tulivyo nao na Kenya, Uganda na Rwanda ila sio zaidi ya hapo.
 
Wanajamvi, tusisahau kuwa sera za CUF ni serikali 3. Sera za Jusa na Seif ni mkataba.
Seif alikuwa arusha anaimarisha CUF na yupo njiani kwenda Bukoba kwa mikutano ya kisiasa.
Swali ni je anakwenda kuhutubia mikutano kuhusu nini ikiwa yeye haamini katika sera za chama anachokitumikia?

Je, ujirani mwema anoutaka ni upi huo ikiwa bado anakuja kueneza sera za CUF huru kwa 'wakoloni'?
Huo mkataba anaosema ni upi zaidi ya mkataba tulio nao?

Kwanini asiwazuie wabunge wa ZNZ kuhudhuria bungeni, kuwataka wajumbe 15 wa tume ya katiba wajitoe na watumishi wa SMZ ikiwa ni pamoja na wanafunzi warudi kwanza ZNZ kudai nchi huru kabla hawajaomba kujiunga na si muungano na Tanganyika?

Maalimu anauma maneno, anakula matapishi halafu anawafanya WZNZ kama maliwato!
Huyu ni mnafiki sana, anataka ZNZ huru akiwa anapata mafao kutoka hazina Dar es Salaam!
 
jussa na wenzie wanataka madaraka tu........... hakuna cha zaidi, bahati mbaya kwa chuki walizonazo wazanzibari zimewafumba mambo kuona lengo halisi la jussa na seif, lakini ndo heri yetu watanganyika, hatutaki muungano wala mkataba waende.....kuvuja kwa pakacha...



MM, wanataka ZNZ huru wakiwa na 'strings attached' yaani muungano wa mkataba.
Hapo ndipo ninaposema Maalim na Jusa wanauma maneno na sijui kama Wazanzibar wanjaua nini wanataka.

Jusa ni mbunge, kwa vile amejiuzulu uongozi wa CUF ili kuimarisha juhudi za ZNZ huru anapaswa pia ajiuzulu ubunge katika bunge la JMT. Akiendelea kuwa mbunge atakuwa anatafuna si maneno bali matapishi.

Maalim Seif hatakiwi kuja Tanganyika katika mikutano ya kisiasa. Kwa kauli ya ujirani mwema kama Kenya, nasi tunataka ujirani mwema hivyo siasa za CUF mwisho Chumbe. Kama ataendelea kuja katika mikutano, kwanza apuuzwe kwasababu anaongea sichokiamini na watu wasiomhusu. Pili atakuwa amekula matapishi achilia mbali kujiuma uma.

Maalimu Seif na Jusa wavunje kwanza CUF ili wawe na vyama huru vya kizanzibar halafu wavunje muungano. Kama hawawezi kuvunja CUF, wafunge midomo na kukaa kimya kwasababu wanakula matapishi yao na si kujiuma uma.

Wamwite Gharibu na wafanyakazi wote wa muungano kutoka ZNZ, watengeneze Passport za ZNZ haraka haraka na watumie Rupee au dollar kama hatua za kuvunja muungano. Wasipofanya hivyo basi wakipanda katika majukwa waiteni manafiki, vizabi zabina, warongo na wahuni.
 
Wawaondoe wabunge wao kwenye Bunge la Muungano; waitishe kampeni ya Wazanzibari wanaotumikia serikali ya Muungano kuachia nafasi zao (akiwemo Ghaib Bilal) na wajitangazie "uhuru wao".

Lakini la kwanza ni kwa yeye (Seif) kuacha ziara za kisiasa Tanzania bara na kuamua kuvunja CUF ili chama cha siasa cha Wazanzibari watupu kizaliwe.

Hapo ndio tutajua kweli wanataka kuwa huru. Watoke kwanza wawe na Zanzibari yao halafu ndio watuulize kama tunataka Muungano wowote na wao! Siyo watoke halafu wakati huo huo waamue aina ya mkataba wanaoutaka wao!


LET ZANZIBAR GO!

Hapa mkuu umegonga msumari wa moto kwenye kidonda wataweza kujiondoa na kuacha asali na maziwa wanayo kunywa sasa hivi?
 
Back
Top Bottom