BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,005
ukitazama picha..hiyo ndiyo kariakoo anayoidhania spika Makinda lakini kwa mtazamo wa Mashado(nami namuunga mkono), kariakoo ni zaidi ya huo mtazamo finyu wa spika Makinda, na alichokieleza Mashado ndiyo maana pana ya kariakoo.
Asante sana Mashado....bahati mbaya sana kwa nchi yetu, historia ni kitu cha kupuuzwa(si unaona hata ile sikukuu ya mashujaa walishaifuta!)
Kwa spika Makinda ni aibu kwake kuongea bila kufikiri au kwa lugha ya sasa kuropoka(ukipenda kukurupuka)...ulitegemea asiwe ni mtu wa hivyo lakini ndiyo chaguo letu, tutafanyaje, vinginevyo tungempinga na sasa asingekuwa pale.
Mi nadhani wakubwa wajifunze kufikiri kabla ya kuongea, zile zama za UMC(msema chochote) zimepita, kila kauli itaangaliwa na kupimwa katika 3D, wengi wataangushwa kwa kauli tu na wakati utathibitisha.
Nawakilisha!
Naam Mkuu ukiwa Kiongozi ni lazima uwe makini sana kila unapotoa kauli na siyo kutoa kauli za kukurupuka ili kuhakikisha kwamba hutoi kauli ambazo zina athari ya kudhalilisha kwa namna moja au nyingine wale unaowaongoza. Huyu mama inabidi aombe samahani haraka sana au akichelewa sana hata hiyo samahani yake itakuwa haina maana