Jumuiya ya Kikristo yamtaka Kikwete ataje viongozi wa dini wanaojihusisha na madawa ya kulevya

Mimi sikuongea, nimeweka hiyo habari inayoongewa. Usitie maneno ya mwingine kinywani mwangu, na source nimeiweka, heee babuwee unanini?

FF!
Vizuri umeweka hotuba ya Raisi kuthibitisha hakusema vibaya na kwamba ni kweli kuna baadhi ya viongozi wa kidini wanajishughulisha na hiyo biashara.

Sielewi kuhusu mahusiano ya hotuba uliyoiweka ambayo inasema ni ya Nyamagana - Mwanza wakati muanzisha hoja anasema Raisi alitoa hotuba Mbinga - Songea.

Hebu fafanua hapo tukuelewe na kama vipi hebu weka hiyo hotuba ya Mbinga tuone ili tuweze kujua Askofu Mokiwa kapata wapi uwezo wa kumdai Raisi awataje hao viongozi.

Kwa mtazamo wangu sioni kosa kwa Raisi kuiomba jamii na taasisi zote nchini kusaidiana katika mapambano ya dawa za kulevya na isitoshe hata viongozi wa dini wamekua mstari wa mbele kuwaasa waumini na jamii kwa ujumla kuepuka matumizi ya madawa hayo.

Sasa hizo kauli tata za kutajana zimetokea wapi(chanzo)???
Kwa yeyote mwenye hiyo hotuba ya Mbinga tunaomba atuwekee hapa tuione ili tuweze kupima pia ukweli wa jambo hili.

.
 
FF!
Vizuri umeweka hotuba ya Raisi kuthibitisha hakusema vibaya na kwamba ni kweli kuna baadhi ya viongozi wa kidini wanajishughulisha na hiyo biashara.

Sielewi kuhusu mahusiano ya hotuba uliyoiweka ambayo inasema ni ya Nyamagana - Mwanza wakati muanzisha hoja anasema Raisi alitoa hotuba Mbinga - Songea.

Hebu fafanua hapo tukuelewe na kama vipi hebu weka hiyo hotuba ya Mbinga tuone ili tuweze kujua Askofu Mokiwa kapata wapi uwezo wa kumdai Raisi awataje hao viongozi.

Kwa mtazamo wangu sioni kosa kwa Raisi kuiomba jamii na taasisi zote nchini kusaidiana katika mapambano ya dawa za kulevya na isitoshe hata viongozi wa dini wamekua mstari wa mbele kuwaasa waumini na jamii kwa ujumla kuepuka matumizi ya madawa hayo.

Sasa hizo kauli tata za kutajana zimetokea wapi(chanzo)???
Kwa yeyote mwenye hiyo hotuba ya Mbinga tunaomba atuwekee hapa tuione ili tuweze kupima pia ukweli wa jambo hili.

.

SA, si mimi wa kuweka habari nisyoijuwa na ambayo sijaianzisha, mimi nilichokiweka nnacho kijuwa mimi. Sasa huyo aliyoleta habari za Mbinga yeye ndio angeziwekea source au angetutangazia kama source ni yeye mwenyewe. Mimi nimeyaweka nnayoyajuwa.
 
Habari za Kikwete kuhusu madawa ya kulevya, tumebandika hapo juu, sasa tuoneshe udini uko wapi humo? na ukishindwa basi wewe na wenzako mnaoshabikia uongo ndio wadini. Na kama hizo hazitoshi tuletee souce yako utuambie wapi alipoongea hayo mnayozuwa. Wacheni hizo siasa za chai maharage.

Haya ndio aliyoyaeleza, kipi kibaya hapa?:
We FazaFox
Usidanganye watu kwa kuweka habari ya zamani habari inayoongelewa ni ya jana wakati akiwa Mbinga kama unamtetea kilaza wako mtetee kwa habari iliyopo si kupindisha habari. Habari yenyewe ya Mbinga ni hii....cheki maneno kwenye red ndiyo ambayo Mokiwa anamtaka Kikwete awataje wanaohusika kwa majina.
RAIS Jakaya Kikwete, amewaonya viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini nchini kuacha tabia ya kushiriki biashara ya kuuza dawa za kulevya na badala yake washirikiane na viongozi wa serikali kuidhibiti biashara hiyo haramu.

Alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akihutubia waumini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mbinga wakati wa ibada maalumu ya kupewa daraja la uaskofu na kusimikwa kwa askofu wa jimbo hilo, Mhashamu John Ndimbo, katika kanisa la kiaskofu la Mtakatifu Killian iliyohudhuriwa pia na Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamini Mkapa.

Alisema baadhi ya viongozi hao wamekuwa wakishiriki kufanya biashara hiyo ya dawa za kulevya kwa kuwatumia vijana ambao huwafanyia mipango ya kuwatafutia hati za kusafiria (Passport) kwenda nchi za nje.


Badala yake Rais Kikwete amewataka viongozi hao nchini kuikemea biashara hiyo na kujenga uhusiano mzuri na vyombo vya dola katika kuhakikisha biashara hiyo inakomeshwa kwa kuwafichua wahusika wanaoifanya ili wachukuliwe hatua za kisheria.

"Inasikitisha sana na kutisha, biashara hii haramu sasa inawavutia hata watumishi wa Mungu, taifa letu litaharibika tusipokuwa makini katika hili kwani baadhi yenu tumewakamata.

"Kwa kauli zenu kemeeni jambo hili kwa kuelimisha jamii hususan vijana waweze kuepuka na matumizi ya dawa hizi," alisema Rais Kikwete.

Ameyaomba pia madhehebu ya dini nchini kuweka mipango endelevu ya maendeleo ya ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi katika mipango yao ya kimaendeleo ili kuisaidia jamii katika ushindani wa soko la ajira.

Alieleza kuwa kutokana na wananchi wengi kukabiliwa na tatizo kubwa la ajira ni vyema sasa serikali kwa kushirikiana na madhehebu ya dini kujikita zaidi katika kujenga vyuo vya ufundi ambavyo vitasaidia kupunguza kero iliyopo ya ukosefu wa ajira hususan vijana wanaomaliza elimu ya msingi na sekondari.

"Kufanikiwa kwa viongozi wa dini katika shughuli za kimaendeleo ni faraja kwa serikali iliyo madarakani na Watanzania wote kwa ujumla," alisema Rais Kikwete.

Awali Rais wa Baraza la Maaskofu Kanisa Katoliki, Tanzania, Askofu Yuda Thadei Ruwa'ichi, aliiomba serikali kuwa makini wakati wa kuandaa bajeti ya nchi ambayo inatarajiwa kupitishwa bungeni hivi karibuni.

Alisema bajeti hiyo ni vyema izingatie maendeleo ya Watanzania ambao wengi wao ni maskini.

Aliishauri pia serikali kudumisha amani na utulivu nchini kwa kuhakikisha wakati wote vitendo vya vurugu havipewi nafasi kamwe na kwamba kanisa Katoliki litaendelea kushirikiana na serikali na Watanzania wote bila ubaguzi wa rangi, dini au ukabila.

Naye Askofu Ndimbo baada ya kusimikwa alitoa shukurani zake kwa Rais Kikwete na waumini wa jimbo hilo na kuahidi kushirikiana na serikali katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

Askofu huyo alisema kuwa kazi yake kubwa ni ya kuwachunga kondoo wa Mungu (waumini) pamoja na kuwahamasisha kujikita katika kilimo cha kisasa ambacho kitawasaidia kupunguza ukali wa maisha.
 
Habari za Kikwete kuhusu madawa ya kulevya, tumebandika hapo juu, sasa tuoneshe udini uko wapi humo? na ukishindwa basi wewe na wenzako mnaoshabikia uongo ndio wadini. Na kama hizo hazitoshi tuletee souce yako utuambie wapi alipoongea hayo mnayozuwa. Wacheni hizo siasa za chai maharage.

Rais Kikwete: Viongozi wa dini acheni biashara dawa za kulevya

Na Gideon Mwakanosya
6th June 2011

Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Mhashamu John Ndimbo, askofu mpya wa Jimbo katoliki Mbinga wakati wa ibada ya kumsimika askofu huyo iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Kilian mjini Mbinga leo.

Rais Jakaya Kikwete amepasua jipu mbele ya viongozi wa dini kwamba kuna baadhi yao wanashiriki biashara haramu ya dawa za kulevya.

Akihutubia waumini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mbinga jana katika ibada maalum ya kusimikwa Mhashamu Askofu John Ndimbo wa jimbo hilo, iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Killian, Rais Kikwete aliwataka viongozi hao kuacha biashara hiyo na badala yake washirikiane na viongozi wa serikali katika kuidhibiti.

Katika ibada hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, Kikwete, alisema baadhi ya viongozi wa dini wamekuwa wakishiriki kufanya biashara hiyo kwa kuwafanyia mipango vijana ya kuwatafutia hati za kusafiria kwenda nchi za nje kwa shughuli hiyo.

Rais Kikwete aliwataka viongozi hao kukemea biashara hiyo na kujenga uhusiano mzuri na vyombo vya dola ili kuikomesha kwa kuwafichua wahusika ili wachukuliwe hatua za kisheria.

" Inasikitisha sana na kutisha; biashara hii haramu sasa inawavutia hata watumishi wa Mungu, Taifa letu litaharibika tusipokuwa makini katika hili, baadhi yenu tumewakamata," alisema Kikwete na kuongeza kuwa:

" Kauli zenu kemeeni jambo hili kwa kuelimisha jamii hususani vijana waweze kuepukana na matumizi ya dawa za kulevya."
Aliyaomba madhehebu ya dini katika mipango yao ya maendeleo yaweke kipaumbele kujenga vyuo vya ufundi stadi ili kuisaidia jamii katika ushindani wa soko la ajira.

Alifafanua kuwa kutokana na wananchi wengi kukabiliwa na tatizo la ajira, ni vyema sasa serikali kwa kushirikiana na madhehebu ya dini kujikita zaidi katika kujenga vyuo hivyo ambavyo vitasaidia kupunguza kero hiyo.

" Kufanikiwa kwa viongozi wa dini katika shughuli za kimaendeleo ni faraja kwa serikali iliyopo madarakani na Watanzania wote kwa ujumla, " alisema.

Kwa upande wake, Rais wa Baraza la Maaskofu Kanisa Katoliki Tanzania, Askofu Yuda Thadei Rwaichi, aliiomba serikali kuwa makini wakati wa kuandaa bajeti ya nchi.

Askofu Rwaichi, alisema bajeti hiyo ni vyema izingatie maendeleo ya Watanzania ambao wengi ni maskini.

Pia aliitaka serikali kudumisha amani na utulivu, kwa kuhakikisha vitendo vya vurugu havipewi nafasi na kwamba kanisa Katoliki litaendelea kushirikiana na serikali na Watanzania wote bila ubaguzi wa rangi, dini au kabila.

Pamoja na mambo mengine, Askofu mpya wa Jimbo la Mbinga, Ndimbo, baada ya kusimikwa alitoa shukurani zake kwa Rais Kikwete na waumini wa jimbo hilo kuwa katika uongozi wake atakuwa bega kwa bega kuhakikisha anashirikiana na serikali katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Hata hivyo, Askofu Ndimbo, alisema kazi yake kubwa ni ya kuwachunga kondoo wa Mungu (Waumini) na kuwahamasisha waumini wa jimbo hilo kujikita katika kilimo cha kisasa ambacho kitawasaidia kupunguza ukali wa maisha.

CHANZO: NIPASHE
 
Valentino ni mzee makini na baraza lake lote,J.K kayakanyaga,

Kwake hii ni aibu kubwa sana,sasa akubali kanisa limdharau na tutapruvu kwamba ni kilaza wa karne,yeye alijua anacheza na vihiyo kama yeye?pale watu wamekula vitabu na wanaijua falsafa ya jamii balaa

haya rais anasutwa kwa tabia yake ya kuchanganya akili kama mbayuwayu,ni aibu sana kuongeaongea kama zuzu utadhani yuko saluni ya akina Hadija...kwamtoro!
 
We FazaFox
Usidanganye watu kwa kuweka habari ya zamani habari inayoongelewa ni ya jana wakati akiwa Mbinga kama unamtetea kilaza wako mtetee kwa habari iliyopo si kupindisha habari. Habari yenyewe ya Mbinga ni hii....cheki maneno kwenye red ndiyo ambayo Mokiwa anamtaka Kikwete awataje wanaohusika kwa majina.

Sasa wewe irudie hiyo post yako na uisome vizuri halafu useme wapi imem quote Kikwete kusema hayo maneno? hayo hayo uliyoywakea nyekundu, ndio Kikwete huyo kaysema? unanini wewe?
 
JK awapasha viongozi wa dini

• Asema wapo wanaouza dawa za kulevya

na Stephano Mango, Songea

RAIS Jakaya Kikwete, amewaonya viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini nchini kuacha tabia ya kushiriki biashara ya kuuza dawa za kulevya na badala yake washirikiane na viongozi wa serikali kuidhibiti biashara hiyo haramu.

Alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akihutubia waumini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mbinga wakati wa ibada maalumu ya kupewa daraja la uaskofu na kusimikwa kwa askofu wa jimbo hilo, Mhashamu John Ndimbo, katika kanisa la kiaskofu la Mtakatifu Killian iliyohudhuriwa pia na Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamini Mkapa.

Alisema baadhi ya viongozi hao wamekuwa wakishiriki kufanya biashara hiyo ya dawa za kulevya kwa kuwatumia vijana ambao huwafanyia mipango ya kuwatafutia hati za kusafiria (Passport) kwenda nchi za nje.

Badala yake Rais Kikwete amewataka viongozi hao nchini kuikemea biashara hiyo na kujenga uhusiano mzuri na vyombo vya dola katika kuhakikisha biashara hiyo inakomeshwa kwa kuwafichua wahusika wanaoifanya ili wachukuliwe hatua za kisheria. "Inasikitisha sana na kutisha, biashara hii haramu sasa inawavutia hata watumishi wa Mungu, taifa letu litaharibika tusipokuwa makini katika hili kwani baadhi yenu tumewakamata. "Kwa kauli zenu kemeeni jambo hili kwa kuelimisha jamii hususan vijana waweze kuepuka na matumizi ya dawa hizi," alisema Rais Kikwete.
Usanifu wakati huu wa mtandao wala haupendezi. Unatumia hotuba ya Mwanza kufunika ile ya Mbinga! Unatumia mifano ya Brazil na Marekani kujibu kesi ya Bongo! Wenzako wanachodai ni kuwa kwa vile inaelekea hadi mbinu wanazotumia zinajulikana basi ingekuwa vyema wangetajwa ( au wakamatwe wapelekwe kwa Pilato). Na hata kama wewe unamjua kiongozi wa dini anayejihusisha na biashara hiyo haramu, mtaje au bora zaidi wapelekee wahusika jina lake.

Amandla....
 
Valentino ni mzee makini na baraza lake lote,J.K kayakanyaga,

Kwake hii ni aibu kubwa sana,sasa akubali kanisa limdharau na tutapruvu kwamba ni kilaza wa karne,yeye alijua anacheza na vihiyo kama yeye?pale watu wamekula vitabu na wanaijua falsafa ya jamii balaa

haya rais anasutwa kwa tabia yake ya kuchanganya akili kama mbayuwayu,ni aibu sana kuongeaongea kama zuzu utadhani yuko saluni ya akina Hadija...kwamtoro!

Anataka kuwabambikizia viongozi wa dini kesi?? kaazi kweli kweli. Kwani wameshawashughulikia wale waliokua wanambambikizia mtoto wa Mengi au ile kesi ndio imeisha ?
 
Jk sijui ni kachoka kabisa kuendesha nchi!!!,anajiachia mno bila ya kuwa na uhakika utafikiri mgonjwa wa tumbo la kuhara!!Kama anajua maaskofu wanaojihusisha kwa nini na yeye asiwe wa kwanza kuisaidia polisi kwa kutoa taarifa!!!!?
 

Kuna mijitu humu hata utoe evidence gani wataendelea na ubishi wao kama ma******sha
 
Mimi sikuongea, nimeweka hiyo habari inayoongewa. Usitie maneno ya mwingine kinywani mwangu, na source nimeiweka, heee babuwee unanini?
Nakushauri kama wewe ni mshauri wa Mh. Rais kaombe msamaha kwa kumpotosha. Haitoshi kuanganisha unganisha stori na kusema wakristo wanafanya biashara ya madawa ya kulevya. Hivi ni lazima uingize udini?
Hivi kweli uislam unawafundisha
Waumini wake kuua watu kwa kujilipua? Au ni wahuni wanatumia uislam kwa manufao yao? Je ni busara kusema ni mafundisho ya uislam? Tafakari.
 
Sasa wewe irudie hiyo post yako na uisome vizuri halafu useme wapi imem quote Kikwete kusema hayo maneno? hayo hayo uliyoywakea nyekundu, ndio Kikwete huyo kaysema? unanini wewe?

Unbelieavable! Wewe uliyeisoma hiyo habari na kuielewa basi tuambie ni nani aliyesema hayo maneno yaliyowekwa wekundu? Ubishi mwingine hauna maana.

Amandla.....
 
SA, si mimi wa kuweka habari nisyoijuwa na ambayo sijaianzisha, mimi nilichokiweka nnacho kijuwa mimi. Sasa huyo aliyoleta habari za Mbinga yeye ndio angeziwekea source au angetutangazia kama source ni yeye mwenyewe. Mimi nimeyaweka nnayoyajuwa.
Usijifanye hamnazo thread yenyewe hiihapa chini katamka wazi ni habari ya Mbinga sasa wewe unajifanya zumbukuku kwa kuja na habari yako ianzishie thread yake ila thread hii tunajadili habari ya Mbinga.
Askofu Mokiwa amemtaka rais Kikwete awataje viongozi wa dini kama alivyosema katika hotuba yake huko Mbinga.
 
We gaidi, una uhusiano wowote wa kingono na Nape? hizo reference zako peleka kwa Magamba wenzio, hatuna muda mchafu wa kutazama upuuzi. Je umesharudi safari ya kwenda sayari nyingine?
 
Nilisha sema humu Jamvini mtu alimpandisha madara haraka haraka alikuwa Mdini wa kupindukia Ali Hassan Mwinyi; na kazi aliyopewa ilikuwa kuendeleza aliyoyaacha...

Kwanini alikuwa anapingana na Kighoma Malima? Mpaka Malima akaamua kuwa Mpinzani wa kiislamu?
 
Haya ndio aliyoyaeleza, kipi kibaya hapa?:

Tuesday, May 31, 2011

VIONGOZI WA DINI NA TAASISI SAIDIENI SERIKALI KUPAMBANA NA MADAWA YA KULEVYA - JAKAYA KIKWETE


1863000103.jpg
Rais Jakaya Kikwete, ametangaza kuwa ataunda chombo maalum cha kupambana na ongezeko kubwa la tatizo kubwa la biashara na matumizi ya dawa za kulevya nchini.

Aidha, Rais Kikwete amewaomba viongozi wa dini na taasisi za dini nchini kusaidiana na Serikali katika kupambana na tatizo hilo lenye madhara makubwa kwa jamii, na hasa miongoni mwa vijana ambao wanaunda asilimia 60 hadi 80 ya Watanzania wanaotumia dawa za kulevya ambazo zinaharibu mwili na akili ya mtumiaji.


Vile vile, Rais amesema kuwa wakati ni kweli kuwa mikoa yote ya Tanzania inakabiliwa na tatizo hilo, lakini ni mikoa saba inayoongoza kwa kuwa na tatizo kubwa zaidi ikiwa ni Dar es Salaam, Mwanza, Mjini Magharibi – Zanzibar, Arusha, Tanga, Mbeya na Dodoma.

Rais Kikwete alitangaza kusudio lake la kuunda chombo maalum cha kupambana na dawa za kulevya jana wakati wa sherehe za kusimikwa kwa Askofu Mteule Albert Jella Randa wa Kanisa la Mennonite, Tanzania, kuwa Askofu wa Dayosisi ya Mwanza ambako alikuwa mgeni.


Sherehe hizo zilifanyika kwenye makao ya Dayosisi hiyo Nyakato, mjini Mwanza.


Akihutubia mamia ya waumini wa Kanisa hilo pamoja na wananchi wengine waliohudhuria sherehe hizo, Rais Kikwete amewaomba viongozi wa dini, madhehebu ya dini mbali mbali nchini kuongeza juhudi za kupambana na biashara na matumizi ya dawa za kulevya.


Akisema kuwa pamoja na kwamba matunda ya juhudi za Serikali katika kupambana na tatizo hilo yameanza kuonekana bado kazi iliyoko mbele ya jamii ya Tanzania ni “kubwa sana”.


“Mwaka jana, 2010, watu 12,119 walikamatwa na kufikishwa mahakamani kwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya. Katika kipindi hicho, dawa za kulevya zilizokamatwa ni heroine kilo 190 na gramu 780, cocaine kilo 65, morphine kilo 11, bangi kilo 279,520 na mirungi kilo 10,317. Takwimu zinaonyesha kuwa mkoani Mwanza tatizo linakua kwa kasi sana,” amesema Rais Kikwete na kuongeza:


“Dawa za kulevya zina madhara makubwa kwa watumiaji na kwa jamii. Kwa watumiaji hatima yake ni mtu kuharibikiwa kimwili na kiakili. Watu huwa mazezeta na hivyo kushindwa kutokuwa na manufaa kwa jamii. Hii ni hasara kwa familia, jamii na taifa. Bahati mbaya sana waathirika wengi ni vijana. Tafiti zilizopo zinaonyesha kwamba asilimia 60-80 ya watu wanaotumia dawa hizo ni vijana wenye umri kati ya miaka 15 hadi 30, alisema.”


Aliongeza: “Hii ni hasara kubwa kwani vijana ndio nguvukazi ya leo na kesho. Ndiyo roho ya taifa na warithi wa familia, jamii na taifa. Wakiharibikiwa taifa letu litaangamia. Tusikubali. Ni wajibu wa kila mmoja wetu kulichukia tatizo hili na kulikemea kwa nguvu zake zote ili kuokoa taifa letu. Nawaomba viongozi wa dini kushirikiana na Serikali na watu wote wenye mapenzi wa nchi yetu kupambana mpaka tufanikiwe kudhibiti na hatimaye kulitokomeza tatizo hili.”


Sherehe za leo za kusimikwa Askofu Randa (50) kuwa Askofu wa Kanisa Mennonite, Jimbo la Mwanza, pia zilihudhuriwa na mamia kwa mamia ya waumini wa Kanisa hilo na wananchi wengine.


Kwenye sherehe hizo, Askofu Mkuu wa Kanisa la Mennonite Tanzania (KMT), Mhashamu Severin Watson Mang’ana amemkabidhi askofu huyo mpya nguvu kuu ishara za mamlaka na madaraka ya uaskofu ikiwamo Biblia, Katiba ya KMT, Cheti cha Uaskofu na vitabu vya taratibu ya kuendesha ibada za Kanisa hilo na nyimbo.

Kanisa la Mennonite lililoanzishwa duniani mwaka 525 na Mchungaji Menno Simon mjini Zurich, Uswisi, liliingia nchini miaka 77 iliyopita mwaka 1934 na liko katika maeneo yote ya Tanzania isipokuwa Zanzibar, Ruvuma na Pwani. Kanisa hilo lina makao yake mkoani Mara.

Source: Maganga One.: VIONGOZI WA DINI NA TAASISI SAIDIENI SERIKALI KUPAMBANA NA MADAWA YA KULEVYA - JAKAYA KIKWETE


Faiza umedandia treni kwa mbele usitake kutubabbaisha hapa. Unataka kusema akina Mokiwa hawakumwelewa JK; wewe na Mokiwa nani mwelewa?
 
Back
Top Bottom