Elections 2010 Jumla ya kura walizopata wagombea yazidi number of valid votes

Jackbauer

JF-Expert Member
Oct 28, 2010
6,039
2,199
Katika hali ya kushangaza mh judge lewis makame ajichanganya kwenye kutaja matokeo ya mwisho ya urais.hivi ndivyo alivyosema:
valid votes-8398394
mziray-96933
kikwete-5276827
slaa-2271941
lipumba-695667
rungwe-26388
Tlp-17482
dovutwa-13176
nikifanya mahesabu ya kujumlisha ninapata utofauti wa vichwa 20 kati ya valid votes na kura walizopata wagombea.CHUNGUZA!!
 
Actual = 8398414

NEC= 8398394
Kama hujakosea fig basi ni kweli kuna tofauti ya 20. Nafikiri katika karne hii kuna mtu anajumlisha kura kwa mkono. Hapa nimecopy na kupaste kwenye excel na kupata hiyo tofauti ya 20
 
Actual = 8398414

NEC= 8398394
Kama hujakosea fig basi ni kweli kuna tofauti ya 20. Nafikiri katika karne hii kuna mtu anajumlisha kura kwa mkono. Hapa nimecopy na kupaste kwenye excel na kupata hiyo tofauti ya 20

tunahitaji ku review video au audio clips.ni aibu sana.nahisi walichukua % na kuanza kumultply kwa total.mwisho wa siku ikatokea watu 1/4,1/2 mwisho wakawa 20.
 
hapa mbona kura zilizoharibika hamna au ndiyo hiyo 20 inaonekana uchakachuaji ulikuwa mkubwa sana mpaka akasahau maana alikuwa anacup and paste
 
please can people in the know verify this please (dr slaa people), invisible and others please verify this, this might be the last nail in the coffin of nec:smile:
 
Nilipokuwa shule ya msingi hasebu nilizokuwa nazipenda ni za kujumlisha na kutoa - niliweza kutumia visoda kuhesabu.
 
Hiyo ndo faida ya kuweka wapigadebe kwenye idara nyeti za serikali, bila kuangalia uwezo wao kifikra! Mtu yoyote hapa JF atunge wimbo wa kumsifu JK, kama akikosa cheo naje anilaumu!!
 
sasa ni 21 au 20? ahhhgggggggg
ngoja na mimi nifannye hesabu:-
Kwamujibu wa Kikwete 2010 blog ni kuwa:-

Walio piga kura 8,626,283 – 42.84%

Kura zilizoharibika – 227,889 – 2.64%
Kura halali – 8,393,394 – 97.36%


Idadi ya kura na asilimia kwa kila chama ni kama ifuatavyo:
1. APPT Maendeleo - 96,933 – 1.12%


2. Chama Cha Mapinduzi – 5,276,827 – 61.17%


3. CHADEMA – 2,271,941 – 26.34%


4. CUF – 695,667 – 8.06%
5. NCCR Mageuzi – 26,388 – 0.31%
6. TLP – 17,482 – 0.20%
7. UPDP – 13,176 – 0.15%

sasa basi:-


96,933 + 5,276,827 + 2,271,941 + 695,667 + 26,388 + 17,482 + 13,176 = 8,398,414 kura halali za vyama.
Zilizo haribika ni
227,889, so TOTAL ya kura zote ni 227,889 + 8,398,414 = 8,626,303 JUMLA YA WATANZANIA WALIOPIGA KURA.
sasa basi ni kweli kuna TOFAUTI YA KURA 20. au ndio margin ya error? +20/-20, hawa jamaa hawaishi kuwashangaza watu unaweza kusikia hivyo.
 
Ni kweli hizi kura zina makosa. Kweli idara zetu zina wababaishaji wengi sana. Makosa madogo madogo haya yanaweza kuleta vurugu kwenye nchi.

Wamekosea kura za mgombea wa TLP na wamemuongezea kura 20. Yeye kapata 17,462 lakini msomaji alitamka 17,482.

Nimehakikisha kwenye spreadsheet yao kura za Mgaywa Muttamwega ni 17, 462. Jaji Makame mwenyewe ndiye alikosea wakati wa kusoma. Yaani hakukuwa hata na watu wa kumwambia mzee umekosea?
 
namkumbuka mwalimu wangu wa somo la hisabati enzi zile za shule ya msingi..............
 
Kazi ya uchakachuaji huwa Mwenyezi Mungu anawapofua macho mafisadi ili uovu wao tuuone mchana kweupe..................

Psalm 50:21 "These things you have done, I kept silent and you thought I was altogether like you, but I will rebuke you and set them in order before your eyes"
 
sasa ni 21 au 20? ahhhgggggggg
ngoja na mimi nifannye hesabu:-
Kwamujibu wa Kikwete 2010 blog ni kuwa:-

Walio piga kura 8,626,283 – 42.84%

Kura zilizoharibika – 227,889 – 2.64%
Kura halali – 8,393,394 – 97.36%


Idadi ya kura na asilimia kwa kila chama ni kama ifuatavyo:
1. APPT Maendeleo - 96,933 – 1.12%


2. Chama Cha Mapinduzi – 5,276,827 – 61.17%


3. CHADEMA – 2,271,941 – 26.34%


4. CUF – 695,667 – 8.06%
5. NCCR Mageuzi – 26,388 – 0.31%
6. TLP – 17,482 – 0.20%
7. UPDP – 13,176 – 0.15%

sasa basi:-


96,933 + 5,276,827 + 2,271,941 + 695,667 + 26,388 + 17,482 + 13,176 = 8,398,414 kura halali za vyama.
Zilizo haribika ni
227,889, so TOTAL ya kura zote ni 227,889 + 8,398,414 = 8,626,303 JUMLA YA WATANZANIA WALIOPIGA KURA.
sasa basi ni kweli kuna TOFAUTI YA KURA 20. au ndio margin ya error? +20/-20, hawa jamaa hawaishi kuwashangaza watu unaweza kusikia hivyo.


Hii hapa ni analysis ya kwangu

Tatizo lipo NEC,nimefanya mahesabu na kuona kuwa kwa mujibu wa NEC

Watu waliopiga kura = 8,626,283

Sasa basi;

Kura zilizopigwa = Kura Halali + Kura zilizoharibika

Kura zilizopigwa = 8,393,394 + 227,889 = 8,626,283
Idadi ya kura walizopata wagombea = 8,626,303
Watu waliopiga kura = 8,626,283

Kura zilizopigwa = Watu waliopiga kura = Idadi ya kura walizopata wagombea
(Mtu mmoja anapiga kura moja TU ya uraisi)

Kwa hiyo kuna tofauti ya kura 20 kati ya kura zilizopigwa na zile walizopata wagombea.
UKIHAKIKI MAHESABU YAO YA ASILIMIA NI SAHIHI ILA IDADI YA WALIOPIGA KURA NA KURA HALALI SI SAHIHI

HUU NI WIZI WA WAZI WAZI!!!!!!!!! AU NEC WAMEKOSEA KATIKA IDADI YA WATU WALIOPIGA KURA NA KURA HALALI(-20 : PUNGUFU KWA ISHIRINI)

http://www.wavuti.com/4/post/2010/1...yotangazwa-na-nec.html#comments#ixzz14QcvnrYm
 
Wamekosea hizo kura za mgombea wa TLP wakati wa kusoma. Wamemuongezea kura 20 ndio maana mahesabu yanakataa.
 
hivi haya makosa wanayoendelea kuyafanya ni mangapi???, naomba na hili wapelekewe ili waliweke sawa kwenye vyombo vya habari ili watu waendelee kuona how incompetent they are please anyone who can pass this info kwa vyombo vya habari please lets do our duty as citizens na kuodoa hii cancer inayoitwa nec:A S angry:
 
hivi haya makosa wanayoendelea kuyafanya ni magapi???, naomba na hili wapelekewe ili waliweke sawa kwenye vyombo vya habari ili watu waendelee kuona how incompetent they are please anyone who can pass this info kwa vyombo vya habari please lets do our duty as citizens na kuodoa hii cancer inayoitwa nec:A S angry:

ni bora ipelekwe mapema panapohusika kabla rais hajaapishwa.sijui katiba/sheria zinasemaje kuhusu jambo hili.aibu aibu aibu sana.
 
Ina maana NEC hawajasoma hisabati za MAGAZIJUTO?
Lakini hili linawezekana kwa kuwa hata JK mwenyewe alikiri kuwa hapendi hisabati wa hesabu.
sasa sembuse Lewis Makame na Kravu?
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom