Jumba la Michael Jackson la Neverland Ranch lauzwa kwa bilionea kwa $22m

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Mar 8, 2020
2,204
4,694
BB1cdsLV.img.jpg

Jumba hilo kubwa la kifahari lililojengwa katika eneo lenye ukubwa wa ekari 2,700, Neverland, Los Olivos, California limeuzwa kwa Mfanyabiashara tajiri aitwaje Ron Burkle kwa Dola za Kimarekani milioni 22.

Marehemu Michael Jackson alinunua jumba katika uhai wake kwa dola za Kimarekani milioni 19 mwaka 1987 , na kulifanya kuwa makazi yake wakati wa umaarufu wake

Alibadilisha jumba hilo na kuwa eneo la burudani , akijenga eneo la kufuga wanyama mbali na ukumbi wa chini ya ardhi ambapo aliwafurahisha watoto na familia zao.

Miaka 1990 na 2000 , Jumba hilo lilichunguzwa sana kutokana na madai ya udhalilishaji watoto kingono dhidi ya msanii huyo.

Bwana Burkle ni mwanzilishi na msimamizi mwenza wa Kampuni ya Yucaipa Companies, LLC na ana utajiri wa dola za Kimarekani Bilioni 1.4

BBC
 
Shamba kubwa la Neverland linalomilikiwa na marehemu Michael Jackson limeuzwa kwa mwekezaji bilionea kwa robo ya thamani.

Ron Burkle, rafiki wa zamani wa Jackson, hivi majuzi alinunua nyumba iliopo katika shamba hilo huko Los Olivos, California, msemaji wake alisema .

Alilipa $22m (£16.2m) kwa jumba hilo la kifahari, limesema jarida la Wall Street Journal, akiweka wazi rekodi zake na kuwataja watu watatu waliohusika katika makubaliano hayo. Jumbe hilo lililojengwa katika ekari 2,700 (1,100 hectare) kwa mara ya kwanza lilinadiwa kwa $100m in 2015.

Tangu wakati huo jumba hilo la Neverland, lililopo kaskazini mwa mji wa Santa Barbara limekuwa likiuzwa hivi karibuni kwa $31m.

Jackson alinunua jumba hilo kwa $19m, ambalo baadaye alililitaja baada ya kisiwa kisichojulikana katika kitabu kilichoandikwa na Peter Pan .

Mwanamuziki huyo alilinunua jumba hilo mwaka 1987 , na kulifanya kuwa nyumbani kwake wakati wa umaarufu wake..

Alibadilisha jumba hilo na kuwa eneo la burudani , akijenga eneo la kufuga wanyama mbali na ukumbi wa chini ya ardhi ambapo aliwafurahisha watoto na familia zao.

Miaka 1990 na 2000 , Jumba hilo lilichunguzwa sana kutokana na madai ya udhalilishaji watoto kingono dhidi ya msanii huyo.

Jackson alilibadilisha jumba hilo na kuwa eneo la watoto kuchezea

Bwana Burkle mwenye umri wa miaka 68 , ni mwanzilishi na msimamizi mwenza wa Yucaipa Companies, LLC, kampuni ya uwekezaji wa kibinafsi .

Thamani ya Burkle kufikia tarehe 24 mwezi Disemba 2020 ilikuwa $1.4bn, kulingana na jarida la Forbes.

BBC
Bado la kule Mgombani sasa
 
Nampenda Sana Michael ..

Lakini Skendo za kuwatafuna watoto zilimchafua Sana ..sijui alikuwa anawala kweli Daahh!!!
 
Nampenda Sana Michael ..

Lakini Skendo za kuwatafuna watoto zilimchafua Sana ..sijui alikuwa anawala kweli Daahh!!!
Luckily scandal zilivuma sana kabla hajafariki, akawa amezisolve. Ingawa kuna watu wanaamini alitumia pesa ndio maana scandal ya hilo Jumba imeshindwa kufutika
 
Nampenda Sana Michael ..

Lakini Skendo za kuwatafuna watoto zilimchafua Sana ..sijui alikuwa anawala kweli Daahh!!!
Alikua juu sana, wazungu walimtafutia zengwe la kumshusha. Baada ya hii scandle hakuweza tena kutengeneza au kuuza album.
 
Alikua juu sana, wazungu walimtafutia zengwe la kumshusha. Baada ya hii scandle hakuweza tena kutengeneza au kuuza album.
Lakini ever since kafa he has been the highest selling dead artist by far every year since kifo chake!
 
Nampenda Sana Michael ..

Lakini Skendo za kuwatafuna watoto zilimchafua Sana ..sijui alikuwa anawala kweli Daahh!!!
Skendo zake hazikuwa zinahusisha moja kwa moja na kuwaingilia .

Ilikuwa zaidi kama kujifurahisha kupitia Watoto, kama vile kuwaambia wavue nguo awaangalie tu wakiwa kama walivyozaliwa, au hata kuwagusa "chululu" zao na vitendo vinavyoendana na hivyo.

Ndio maana hata alifanikiwa kutoka bila kifungo pamoja na kwamba kashfa nyingi zilikuwa hazimuachi salama kwa asilimia mia moja....kama zingehusisha kuwaingilia sidhani kama wangemuacha huru....angalia R Kelly anavyosota.
 
Back
Top Bottom