Jumba la kifahari la Raisi wa Tunisia lavamiwa na kuchomwa moto

Mallaba

JF-Expert Member
Jan 30, 2008
2,554
47
Nilikuwa nafatilia news kutoka Tv nimeona jinsi wananchi wa Tunisia walivyokasirika na kuamua kuvamia Mansion la aliyekuwa Raisi wao wakichoma moto na kupora kila kitu kilichokuwemo mle ndani ya lile jumba la kifahari.
Wlikuwa wakisema hizi zote ni pesa zetu, mabilioni yaliyotumika kujenga hapa ndio yaliyosababisha kila kitu kupanda ndani ya nchi yetu na maneno mengine mengi tu.

Nimejifikiria sana , J ehii kitu itakuja tokea pia nchini kwetu? maana mpaka sasa naona Mkwele na viongozi wenzake wanzidi kujijengea makasili na Mansions kubwa zaidi makwao bila kujali hali halisi ya watanzania amabao hata mlo wa siku ni kazi.
Mara tusnasikia kuna walimu tangu mwezi wa kumi hawajalipwa mishahara yao, mara kuna tetesi kuwa mwezi ujao hakutakuwa na mishahara, kisa kuna ujenzi wa viongozi wetu hivyo kila kitu lazima kisimame kwanza.
Mimi nadhani viongozi wetu asipoangalia wataishia kukimbilia nchi za jirani maana wananchi hawatakuwa na furaha nao hakika na wao hawatakuwa na Amani , na suluhisho lao litakuwa ni kama la huyo Raisi wa Tunisia alivyofanya, pamoja na utajiri wake na utawala wa miaka zaidi ya 20 amesoma nyakati na kuona kuwa hapa hapakaliki.
 
Tunisia was the coolest country in Africa kuliko hata Tanzania. Tanzania tunaelekea huko huko.
 
kweli tunaelekea hukohuko ,lakini je ni lazima tupitie njia hiyo hiyo? why cant we use our own way?
Tunisia was the coolest country in Africa kuliko hata Tanzania. Tanzania tunaelekea huko huko.
 
Tatizo la CCM ni kulindana chama kimejaa watu waovu na wadhalimu kwa taifa hili.sasa watawageukaje? hapo ndio kuna issue ndio mana wanatafuta kila jinsi waendelee kubaki madarakani ili walinde maovu yao.Ila mwisho unakuja eeh Mungu utusaidie nchi ni ya kwetu sote iweje wengine waishi kama peponi na wengine waishe kama vibarua?Inauma sana.
 
ni kweli kila kitu kina mwisho wake, na hakuna marefu yasiyokuwa na ncha.
Tatizo la CCM ni kulindana chama kimejaa watu waovu na wadhalimu kwa taifa hili.sasa watawageukaje? hapo ndio kuna issue ndio mana wanatafuta kila jinsi waendelee kubaki madarakani ili walinde maovu yao.Ila mwisho unakuja eeh Mungu utusaidie nchi ni ya kwetu sote iweje wengine waishi kama peponi na wengine waishe kama vibarua?Inauma sana.
 
Kosa kubwa linalofanyika kwa viongozi wa Tanzania ni kujisahau kwa kudhani kuwa mambo yatakuwa sawa tu miaka yote kwa kuwa jeshi lipo, mahakama ipo na vyombo vingine ambavyo vinaweza kutumia nguvu ili kuzima vuguvugu.Lakini ukweli ni kwamba hata katika biashara, Makampuni makubwa yenye nguvu na ushawishi kwa bidhaa zake huendelea kufanya matangazo na mabadiliko ya kiongozi kila wakati ili kuhakikisha kampuni inaelendea kuwa competitive and profitable.Pale CEO anaposinzia na kudhani kwa kuwa kampuni yake ndio inayoongoza kwa kuwa na soko kubwa basi hushangaa pale competitors wanapokuja na mbinu mpya na kuipiku katika soko na ushindani hata kama kampuni kubwa ilikuwa na resources za kutosha.

Binadamu ni kiumbe tufauti hubadilika haraka kutokana na mazingira na hali halisi. Pamoja na utulivu wa Tunisia hapo zamani lakini yametokea yaliyotokea, jeshi likiwepo, polisi, mahakama na vyombo vingine.Ni usingizi wa kiongozi wa Tunisia na wenzie kwa kudhani things will always be under control. Tanzania haina muda mrefu mabadiliko yatatokea. Iwe kwa njia yoyote lakini ni wazi wananchi wamechoka na ni dhambi kufikiri kwamba ni wajinga au hawajui kinachoendelea. Si lazima iwe kama Tunisia kwani kila jamii ina mazingira yake lakini mabadiliko makubwa yako mbioni. Stay tuned.
 
thanks a million for your insight.
well appreciated
Kosa kubwa linalofanyika kwa viongozi wa Tanzania ni kujisahau kwa kudhani kuwa mambo yatakuwa sawa tu miaka yote kwa kuwa jeshi lipo, mahakama ipo na vyombo vingine ambavyo vinaweza kutumia nguvu ili kuzima vuguvugu.Lakini ukweli ni kwamba hata katika biashara, Makampuni makubwa yenye nguvu na ushawishi kwa bidhaa zake huendelea kufanya matangazo na mabadiliko ya kiongozi kila wakati ili kuhakikisha kampuni inaelendea kuwa competitive and profitable.Pale CEO anaposinzia na kudhani kwa kuwa kampuni yake ndio inayoongoza kwa kuwa na soko kubwa basi hushangaa pale competitors wanapokuja na mbinu mpya na kuipiku katika soko na ushindani hata kama kampuni kubwa ilikuwa na resources za kutosha.

Binadamu ni kiumbe tufauti hubadilika haraka kutokana na mazingira na hali halisi. Pamoja na utulivu wa Tunisia hapo zamani lakini yametokea yaliyotokea, jeshi likiwepo, polisi, mahakama na vyombo vingine.Ni usingizi wa kiongozi wa Tunisia na wenzie kwa kudhani things will always be under control. Tanzania haina muda mrefu mabadiliko yatatokea. Iwe kwa njia yoyote lakini ni wazi wananchi wamechoka na ni dhambi kufikiri kwamba ni wajinga au hawajui kinachoendelea. Si lazima iwe kama Tunisia kwani kila jamii ina mazingira yake lakini mabadiliko makubwa yako mbioni. Stay tuned.
 
TUNIS, Jan. 17 (Xinhua) -- New protests have broken out on the streets of Tunisia's capital, shortly before the expected announcement of a new national unity government.
Tunisian security forces used water cannon and fired bullets in the air on Monday to disperse demonstrators who took to the streets to protest against the ruling party of the ousted president, Dubai-based al-Arabiya TV reported.
Prime Minister Mohammed Ghannouchi promised to unveil a new government of national unity to maintain stability in the country and avoid fresh protests.
Ousted Tunisian President Zine El Abidine Ben Ali, who had been in power since 1987, fled to Saudi Arabia on Friday following mass protests against his government over unemployment, price hike and corruption.
 
Kinachoendelea Tunisia ilikuwa kama sinema fulani hivi.
Vijana walianza kulalamika HAKUNA AJIRA ingawa wa elimu ya chuo kikuu, maisha yako juu na hawawezi kujimudu.

Graduate mmoja akaamua kufanya kazi ya umachinga wa kuuza mboga mboga na matunda lakini unavyojua polisi wa Afrika walivyo, wakamzoa mzobemzobe na kutaifisha mali zake alizopata kwa mtaji kwa taabu .
Ili kuprotest hali hilo kijana akaamua kujipiga moto jambo lililosababisha mauti yake. Fujo zimeendelea hadi Rais kuachia ngazi.

Ni bahati mbaya sana viongozi wetu hawajifunzi yakitokea kwa jirani, wanadhani watanzania aliawaongoza Nyerere bado ni wale wale.

Ila huko ndiko tunaelekea ingawa inaweza kuwa kwa namna tofauti.
 
Kweli Tz ndotunaelekea huko kwani Tunisia mpaka wamefika hapo nikutokana na viongozi kujilimbikizia mali na kujali familia zao. NA viongozi wa TZ wengi wao ndo hivyo kwani tunaona mali walizo nazo, hasa baba kama nikiongozi pia na mtoto utakuta anamali kichizi heti ni vyababa wakati wadanganyika tunaona na ukweli hupo. Hila natoa angalizo kwa Jeshi letu lote kuanzia polisi na jwtz kwamba tunawaomba wasifungamane na serikali kabisa kama wadanganyika tukiamua kwamba serikali hiliyoko madarakani hiondoke basi majeshi yawe kwa raia kwan bila hilo patakuwa hapatoshi. Tumechoka kunyanyaswa hapa wengine unakuta mlo mmja napata lakini inaniuma sana wadanganyika wenzangu ambao hata kujua leo kutakuchache au hatakula nini hajui halafu unaniambia kwamba uchumi umekua, mala wananchi wakawaida wanamagari, mara watoto wengi wamedahiliwa shule za msingi hakuna kitu hapa nasema hivi siku za kudanganywa simeisha nasitakuwa na huruma namtu kama nikwenda jela haya au kukufilisi sawa tu hili vizazi vijavyo vitambue kwamba kweli hapa nikila rushwa au nikisaini mkataba feki hapa nitaozea jela.
TUMEDANGANYWA SANA, TUMEIBIWA SANA, NAWANAENDELEA KUTUIBIA NA MSHUKURU MUNGU KUWAPA WATZ HALI YAKUJITAMBUA KWAMBA SASA HATUDANGANYIKI NG'OOOOOOO.
 
Kuna siku moja nikiwa katika lecture ya Development Studies kuna muhadhili mmoja maarufu sana kwa majigambo kuwa kitanda chake yeye kina degree saba yaani yeye nne na mkewe tatu. Jamaa huyu aliwahi kutoa statement moja miaka hiyo nanukuu "Kama mimi ningekuwa ni mwanasiasa nisingeogopa wamachinga au wakulima ningewaogopa ninyi, maana ni bomu ninalolitengeneza mwenyewe ambalo nisipolitupa mapema kwa kuhakikisha kunakuwa na ajira za maana za kuwafaa na kuwaridhisha basi litanilipukia", akaendelea kuwa kitendo cha serikali kuwasomesha halafu inajiondoa katika kuwatafutia ajira kama ilivyokuwa mwaka jana kurudi nyuma ni dalili mbaya kwa mustakabali wa taifa. Aliyasema hayo baada ya serikali kutangaza rasmi kuwa inajitoa kuwapatia ajira wasomi wa chuo kikuu. Sooner or later it will blast. CCM itambue kuwa the major threat to our national peace is lack of employment to our graduates and other citizens.

Kuna mtu mmoja aliwahi kunipa msemo kuwa ukipikia ugali kwenye chungu na kumwagia mboga juu basi utakula mboga kwa furaha ila ujue mwisho utakutana na ugali chini usiokuwa na mboga - Komba kasoma ulafika na twimege

Wanachofanya watunga sera sasa ni sawa na msemo huo ila wajue kuwa kazi ipo mbele, wafanye wanavyotaka, walipane mabilioni ya Dowans, wapandishe bei ya bidhaa kwenye biashara zao ila kuna siku watu watasema sasa basi
 
kama kutokumpa kura kiongozi amabye mnaona hawafai. lakini cha kushangaza pamoja na makelee yote haya bado tunaona watu wanaendelea kuwachagua akina LOwasa, LA, Chenge n.k sasa tutafika wapi?
kama zipi ambazo unaona zitafanikiwa?
 
kweli hili la kukosa ajira watu wenye elimu ni bomu ambalo linaweza kulipuka wakati wowote.
Kuna siku moja nikiwa katika lecture ya Development Studies kuna muhadhili mmoja maarufu sana kwa majigambo kuwa kitanda chake yeye kina degree saba yaani yeye nne na mkewe tatu. Jamaa huyu aliwahi kutoa statement moja miaka hiyo nanukuu "Kama mimi ningekuwa ni mwanasiasa nisingeogopa wamachinga au wakulima ningewaogopa ninyi, maana ni bomu ninalolitengeneza mwenyewe ambalo nisipolitupa mapema kwa kuhakikisha kunakuwa na ajira za maana za kuwafaa na kuwaridhisha basi litanilipukia", akaendelea kuwa kitendo cha serikali kuwasomesha halafu inajiondoa katika kuwatafutia ajira kama ilivyokuwa mwaka jana kurudi nyuma ni dalili mbaya kwa mustakabali wa taifa. Aliyasema hayo baada ya serikali kutangaza rasmi kuwa inajitoa kuwapatia ajira wasomi wa chuo kikuu. Sooner or later it will blast. CCM itambue kuwa the major threat to our national peace is lack of employment to our graduates and other citizens.

Kuna mtu mmoja aliwahi kunipa msemo kuwa ukipikia ugali kwenye chungu na kumwagia mboga juu basi utakula mboga kwa furaha ila ujue mwisho utakutana na ugali chini usiokuwa na mboga - Komba kasoma ulafika na twimege

Wanachofanya watunga sera sasa ni sawa na msemo huo ila wajue kuwa kazi ipo mbele, wafanye wanavyotaka, walipane mabilioni ya Dowans, wapandishe bei ya bidhaa kwenye biashara zao ila kuna siku watu watasema sasa basi
 
kweli tunaelekea hukohuko ,lakini je ni lazima tupitie njia hiyo hiyo? why cant we use our own way?

Logic hapo ni ndogo sana, Tunisia tatizo lao ni...."unemployment, price hike and corruption". na Tanzania matatizo makuu ni hayohayo, hivyo the only way to go through this ****n shit will be same like Tunisi...ogopa sana watu wasio na ajira na hilo wameelezwa sana na akina Jenerali Ulimwengu lakini wamekuwa viziwi, Rushwa sasa inaliwa waziwazi bila uoga then unategemea nini? kuchakachua wataendelea na kamwe vyama pinzania havitashinda kwenye box ila vitashinda kupitia njia hii ambayo kwetu tunaita Peoples Pawaaaaaaaaaa!
 
siku zao zimeshafika hivyo hawataendelea kuiba kura siku zote, kwani hata marefu yana ncha.
Sadam aliachia nchi sembuse na ccm?
Logic hapo ni ndogo sana, Tunisia tatizo lao ni...."unemployment, price hike and corruption". na Tanzania matatizo makuu ni hayohayo, hivyo the only way to go through this ****n shit will be same like Tunisi...ogopa sana watu wasio na ajira na hilo wameelezwa sana na akina Jenerali Ulimwengu lakini wamekuwa viziwi, Rushwa sasa inaliwa waziwazi bila uoga then unategemea nini? kuchakachua wataendelea na kamwe vyama pinzania havitashinda kwenye box ila vitashinda kupitia njia hii ambayo kwetu tunaita Peoples Pawaaaaaaaaaa!
 
Back
Top Bottom