Saint Anne
JF-Expert Member
- Aug 19, 2018
- 73,601
- 225,196
Kumbe hilo somo wewe unalijua hivyo?Hawajalazimishwa ila waumini wengi wamekuwa brainwashed..Mimi najielewa na siwezi kwenda kusali kwa hawa watu na kama ni sadaka basi nitampa asiyejiweza.
Eti mpe Mungu sadaka ili uendelee kufanikiwa,then wao wanaenda kutumia sadaka hizo kwenye ishu personal na sio hata za kukuza kanisa.
Hilo soma la sadaka inabidi liwekwe wazi sasa,kuwa tunatoa sadaka ili mtumishi aweze kuishi.
Kama unalijua hivyo basi umepotea.
Kama jinsi wewe unavyoguswa sehemu ya wahitaji ,unavyotoa sadaka kwa wasiojiweza vivyohivyo mtu mwingine anaguswa sehemu nyingine kutoa sadaka yake..
Kwahiyo usitake kupangia mtu mahala pa kutoa sadaka..na usiseme mtu hajitambui kwa kutoa sadaka huko.
Una uhakika umeongea na Mungu akakuambia hao watu wako brainwashed??labda Roho wa Mungu amekuonyesha mwenzetu.
Pale juu nimesema mimi nawajua watu wanasali huko na ni matajiri..kanisani kuna kila aina ya watu.
Mwisho nikwambie umasikini siyo sifa na ukiona una mawazo ya kutaka kila mtu aishi kimasikini basi jua una shida sehemu.
Mungu alikuumba ili utawale
Tuanze kwanza na somo la sadaka,inaonyesha haulijui.
Unatia porojo tu,inabidi tuende kwenye Biblia Sasa.