Kama connection hiyo ni ya kweli,najiuliza huyu jamaa katulisha nini hata tunamshindwa ilihali katika kila aina ya ufisadi yumo au ana mahusiano nao? mwenye jibu anisaidie maana mie nahisi nimechanganyikiwa
Jamani mpaka sasa ni tuhuma na fununu na wala si uhakika kwamba hilo hekalu ni la RA, kwanini atupiwe lawama, laana na kejeli?.
Tutafute ukweli kwanza kabla ya kuanza kulaumu.
Na jambo lingine jaribuni kuelewa kwamba hata kama RA alifanya ufisadi huko siku za nyuma ukweli ni kwamba haukuufanya peke yake bali ni kundi kubwa la watu lilihusika na pasipo kushikiwa bunduki wala visu. Waliongea na kuelewana na kuamua kufanya waliyoyafanya. Kwanini alaumiwe yeye tu kwa kila jambo?.