kinyamkela mahaba
JF-Expert Member
- May 4, 2022
- 1,181
- 1,574
Mnaendeleaje na ujenzi wa Taifa? Jumapili nilifanya kitendo ambacho kimenipa maswali mengi ya namna ya kumtazama Mchungaji na washirika wenzangu kwa jicho lile lile la mwanzo. Naumia sana, na sijui hali itaishaje!
Ulikuwa ni wakati wa sadaka kanisa Z la kiroho hapa Dar, tulishakubaliana tutatoa 2000 kama familia ya Mr na Mrs X, sasa mfukoni nikabakiwa na 500 ya kununua maji njiani ili tunywe. Mwishoni wakatangaza sadaka inayohusu wamama, sasa akawa analazimisha achukue jero langu akatoe mchango.
Nikamuambia hatukukubaliana hivi, kikubwa sadaka tumeshatoa basi inatosha, hivyo tusubiri Jumapili ijayo kwani chaguo lilikuwepo. Lakini mwenzangu hakunielewa kabisa hivyo akalazimisha kuingiza mkono mfukoni mwangu, nikamfinya.
Akanisukuma kidogo nikahamaki nikasubiri ibada iishe, tulipotoka nje akaanza tena kuleta mdomo, nikamsukuma akaanguka, kuua aibu nikatengeneza mazingira ionekane kajikwaa. Ila nahisi wameshtuka kuwa nilimsukuma. Tumerudi nyumbani kanuna mpaka muda huu, na anaonesha kidonda kile ambacho kilitokana na kumfinya kule kanisani.
Hivi nauaje aibu hii? Na kwa nini huyu Manka hana heshima kabisa? Naona taswira yangu itachafuka nisipofanya kitu.
Ulikuwa ni wakati wa sadaka kanisa Z la kiroho hapa Dar, tulishakubaliana tutatoa 2000 kama familia ya Mr na Mrs X, sasa mfukoni nikabakiwa na 500 ya kununua maji njiani ili tunywe. Mwishoni wakatangaza sadaka inayohusu wamama, sasa akawa analazimisha achukue jero langu akatoe mchango.
Nikamuambia hatukukubaliana hivi, kikubwa sadaka tumeshatoa basi inatosha, hivyo tusubiri Jumapili ijayo kwani chaguo lilikuwepo. Lakini mwenzangu hakunielewa kabisa hivyo akalazimisha kuingiza mkono mfukoni mwangu, nikamfinya.
Akanisukuma kidogo nikahamaki nikasubiri ibada iishe, tulipotoka nje akaanza tena kuleta mdomo, nikamsukuma akaanguka, kuua aibu nikatengeneza mazingira ionekane kajikwaa. Ila nahisi wameshtuka kuwa nilimsukuma. Tumerudi nyumbani kanuna mpaka muda huu, na anaonesha kidonda kile ambacho kilitokana na kumfinya kule kanisani.
Hivi nauaje aibu hii? Na kwa nini huyu Manka hana heshima kabisa? Naona taswira yangu itachafuka nisipofanya kitu.