Jumanne nyeusi kwa Rais Magufuli inakuja

Nyote mnaompinga JPM ni WAPUMBAVU , jifunzeni kufanya kazi. Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni John Joseph Pombe Magufuli mpaka 2025, endeleleeni kusubiri hizo sijui jumanne nyeusi, sijui ijumaa za blue au jumamosi za njano, mtangoja milele Kama wafuasi wa Kibwetele. Nyambafu.
 
Ni vzr tuilekeze serikali kuwa wanaposema wanataka uchumi ya viwande basi waandae mazingira za uchumi unaotegemea viwanda yaani uchumi unaotegemea uzalishaji tofauti na hali ilivyo kwasasa uchumi wetu ni uchumi kukusanya kodi.

Uchumi unaotegemea uzalishaji ni ile unaovutia wawekezaji kuwekeza na njia pekee ya kuvutia wawekezaji ni kuwapunguzia kodi. Na wao watawekeza na kuongeza ajira ambapo uzalishaji wa maligafi utaobgezeka na hivyo kupunguza utegemezi. Baada ya kutengeza ajira na uzalishaji wa bidhaa kuongezeka hapo ndipo serikali inakusanya kodi ambayo ni Mdogo lkn walipaji ni wengi.
Mfano wa nchi inayofanikiwa kwa uchumi wa viwanda kwasasa ni Ghana.

Napenda waziri mpango angepitia link hii naamini kuna kitu atajifunza ikiwa kweli a nahitaji Tz kuingia kwenye uchumi wa uzalishaji kinyume chake tujiandae kisaikologia kupokea anguko LA uchumi.



Kwa uchache ili bidhaa imfikie mlaji Tz bidhaa hiyo itatozwa kodi zaidi ya 100%. Yaani bidhaa inayopaswa kuuzwa kwa sh 20 itauzwa 40 na inayopaswa kuuzwa sh 1200 inauzwa 2400.

Nini tofauti ya awamu ya 4 na awamu ya 5 wakati chama kinachotawala ni kile kile. Tofauti kubwa ni kuwa awamu ya 4 kodi nyingi zilikuwa zinalipwa pungufu yaani kulikuwa na ukwepaji Mkubwa wa kodi ilhali kiasi kidogo cha kodi wakilipa . awamu ya 5 imeona changamoto hizo na kuamua kusimamia kodi ilipwe kama inavyostahiki, serikali inapaswa kurasimisha mapungufu yaliyojitokea ili kila upande ufurahie yaani wawekezaji wapinguziwe kodi ili bidhaa iwafikie wananchi kwa gharama nafuu na serikali ipate kodi yake na kwakuwa itakuwa ndogo wafanya biashara watalipa bila shuruti na hivyo kupelekea mianya ya rushwa kutokuwapo.


Kwasasa hali ya kodi kwa bidhaa ilivyo ni kuna
Direct taxes
Import duty 25%
Vat on import duty 18%
Income tax 30%
Vat on sales 18%
Levy 0.5%
Road toll 1%
Inderect taxes
Kwenye mafuta
Umeme
Halmashauri


Uchumi wa ghana unakuwa kwa 7% in 2017/2018

 
Hana akili vipi...???
Acha kutumia lugha za maudhi...mbona jamaa katiririka vizuri acha wivu na uvivu wa kufikiri... Suala la uchumi kushuka/kupanda ni la kutafakari binafsi sio kusingizia GDP....
Wajinga ni wengi na watu makini ni wachache.. Suala la kushuka au kupanda kwa uchumi ni kujumlisha/kutoa na kulinganisha tuu sio mpaka mzungu aje akufundishe ndo uelewe.. Ndo maana jambo la msingi ww unaleta mzaha...

Well said! Kuna watu wamempa like za kutosha!! Hapa ndo utajua watz wasivyokuwa makini! Kila kitu ni ushabiki tu, hakina kufikiria mkuu
 
Duuuuh, nchi hii tu wajinga kupindukia. Tunamkubalia kabisa mtu anayetuambia Great Depression ilisababishwa na mtu aitwae Herbert Hoover.

Nafahamu wengi wetu wajinga na wengi wengi tumapenda kuongopewa jambo lolote litskaloisema vibaya serikali, imekuwa hulka yetu.

Lakini sikuwahi kufikiri ujinga na hulks yetu ingetufanya tudanganywe hata kwa mambo dhahiri yanayofahamika duniani kama Great Depression.

Hongera mtoa post umefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika uongo wako huu. Wacha wajinga tuendelee kukuunga mkono na sisi tunaopenda kudanganywa no wakati wetu kushiriki kuzidanganya nafsi zetu.
 
ANGUKO LA UCHUMI KWA TAIFA LA MAREKANI (1929~1933)

Aliyeitwa Herbert hoover aliyekuwa na miezi nane tu kwenye uongozi wake kutokana na kutokujuwa vema nini maana ya urais wa marekani uchumi ukaanguka, siku ambayo wao waliyoitaja kama jumanne nyeusi hali ilikuwa mbaya zaidi 0.75 walipoteza ajira.

Sababu kubwa ya Herbert Hoover kushindwa ni kufa kwa ununuzi wa hisa (New york stock exchange) ambayo ilipelekea watu kuchukuwa pesa zao kwenye mabenki na kufirisika kitendo ambacho kilipelekea wamerikani kumkataa rais HERBERT HOOVER.

View attachment 441037
Utawala wa herbert hoover ni wazi mambo yalionekana kuwa mabaya katika maeneo mengi muhimu kwa uchumi wa Marekani. Ni wamarekani ndio waliyofahamu kuwa Hoover mambo kwake alikuwa mabaya lakini kwa Tanzania mambo tofauti sio kama watu makini hawapo la, ni wajinga wengi sana kuliko watu makini na ndio sababu kubwa ambayo CCM wanayotumia.

View attachment 441038
Rais Herbert Hoover.

Mwaka 1929 akaja mkombozi wa uchumi wa marekani rais Franklin Delano Roosevelt na kauli yake "The only thing we have to fear is fear itself".

View attachment 441043

Mipango madhubuti ya rais Franklin delano roosevelt baada ya kuwa rais mwaka 1929

1. Nafuu(Relief): Alitoa pesa kusaidia wazee wasio na ajira.

2. Akafanya mabadiliko katika sector tofauti tofauti miongoni ni mabenk akazipa mitaji ili kurejesha matumaini kwa wananchi kutunza hela zao kwenye mabenk.

3. Rais franklin alitoa ajira kwa vijana.

4. Kutengeneza uhusiano mzuri wa wafanya kazi na waajiri wao ili kuteta ufanisi wa kazi hatimae marekani ikawa kubwa tena kwa uchumi.

View attachment 441059
The only thing we have to fear is fear itself.

View attachment 441060
It is common sense to take a method and try it. If it fails, admit it frankly and try another. But above all, try something.

RAIS JOHN POMBE MAGUFULI.

View attachment 441063

Utawala wa rais John Pombe Magufuli una zaidi ya mwaka moja na miezi kadhaa madarakani. Kama taifa, hatuwezi kuendelea na fungate (honeymoon) ya utawala wake wakati ni wazi mambo yanaonekana kuwa mabaya katika maeneo mengi muhimu kwa uchumi wa Tanzania.

Ufike wakati sasa tuanze kizungumzia mambo mazito yanayotukabili kama taifa.

Magufuli atambue kuwa hata Mungu mwenyewe alianza na mwanga

"Mungu akasema, iwe nuru, ikawa nuru. Mungu akaiona nuru na giza. Mungu akaiita nuru mchana, na giza akaiita usiku. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya kwanza"

Ni maneno kutoka katika kitabu cha mwanzo(1: 3~5)

Tunatakiwa kufikiria kwamba tunaweza kuumizwa na tunaweza kujiumiza wenyewe, Magufuli anatakiwa kuambiwa kuwa safari yake ni ngumu katika uchumi.

Note: Magufuli utashi wa kisiasa ni muhimu katika kuendesha taifa.

Mipango ya rais Herbert ni sawa na mipango ya Magufuli.

Msema ukweli ni mpenzi wa Mungu.

By mr mkiki
"Ni kiburi cha ovyo mtu kuropoka yale anayoyaona kuwa ya kweli bila kujali matatizo yatakayowapata wananchi. Maana hakuna hata mmoja wetu anayejua ukweli wote; tunaweza tukagundua sehemu mpya ya ukweli, lakini hatuna haki ya kujidai kwamba tunajua zaidi " - Nyerere, Feb 29th,1968
 
Hii ni analogy nzuri sana. Kuweka kumbukumbu sawa ni kwamba Rais Rooservelt aliingia madarakani mwaka 1933.

Rais Rooservelt ndiye alikuwa muasisi wa utaratibu wa tathmini ya siku 100 za rais kukaa madarakani. Katika siku zake 100 madarakani, Rooservelt alipeleka miswada 13 ya sheria bungeni.

Mabadiliko makubwa aliyoyasimamia Rooservelt aliyapa jina "The new deal", ikiwa ni pamoja na kuachana na sera za uchumi zilizotokana na nadharia za Adam Smith (Classical Economic Theory) ambazo zilikiwa zinajali tu matajiri na wawekezaji na akakumbatia nadharia za kiuchimi za John Keynes zilizosisitiza serikali kuratibu shughuli za kiuchumi ili manufaa ya kustawi kwa uchumi yawanufaishe wote.

Ni wakati wa urais wa Rooservelt ndipo taasisi imara za kiuchumi (kama CMSA, FCC, nk) zolipoanzishwa huko Marekani na kuliwezesha hili taifa kuwa kinara duniani kiuchumi.

Haya yaliwezekana kwa Rooservelt kwa kuwa alikuwa na muongozo wa imani ya kiikadi kisiasa, pamoja na mrengo wa kiuchumi, ambavyo vilimpa dira ya kufanya aliyoyafanya na kufanikiwa.

Hizi sifa Magufuli hana. Ni vyema akatumia zaidi washauri wake wa kiuchimi na kuachana na kutafuta umaarufu. Awe strategist zaidi.
Asante
 
Sifa za mtu asiyeweza kujifunza
1.Kutokuwa na kumbukumbu aka historia
2.Kiburi
3.kupenda sifa (huwexi kuuliza utaonekana dhaifu)
4.kuwamiongoni mwa wajinga kuliko wewe
5. Kuwa miongoni mwa wanafiki
 
Ulitakiwa useme ni Mambo gani unayaona hayapo vizuri kwa utawala huu.

Kwa sababu, Mishahara analipa kama kawaida, yeye anataka kodi yake tu halali ilipwe.

Labda useme kwamba, Rais alegeze masharti ya kuweka fedha kwenye Bank Binafsi ili watu na makampuni wakope, hapa Rais anaweza kukaa na jopo lake na kuandaa utaratibu mzuri wa kuzitoa Fedha BOT na kuzipeleka kwenye Mabank binafsi huku BOT ikizi-monitor lakini Bank nazo lazima zidai kwanza madeni yao toka kwa waliowakopesha.

Mimi sioni tatizo lolote juu ya Utawala wa JPM Zaidi ya kusikia malalamiko ya watu kuwa hakuna pesa mifukoni.
Pole sana....Ina maana nchi inavyoangamia ktk Hali ya kawaida huoni...au mwenzetu uko stockhom
 
Uchumi unaomaanisha ni upi? Maana siye wenye maisha ya chini tunaona mambo yanaenda tu hela ya kula hatukosi, sasa wanaolia wengi ni wale waliozoea kupata hela ambazo hawakuzistahili na ndo maana matumizi yake yalikuwa ya kutapanya, mfano watu walikuwa na nyumba ndogo wanazihudumia kwa kila kitu Magufuli kaja kawabana wote wamerudi njia kuu. Sasa michepuko lazima iseme uchumi kwa sababu walizoea kulishwa. Hakuna uchumi utakaotetereka tupige kazi kwa bidii.
 
Uchumi unaomaanisha ni upi? Maana siye wenye maisha ya chini tunaona mambo yanaenda tu hela ya kula hatukosi, sasa wanaolia wengi ni wale waliozoea kupata hela ambazo hawakuzistahili na ndo maana matumizi yake yalikuwa ya kutapanya, mfano watu walikuwa na nyumba ndogo wanazihudumia kwa kila kitu Magufuli kaja kawabana wote wamerudi njia kuu. Sasa michepuko lazima iseme uchumi kwa sababu walizoea kulishwa. Hakuna uchumi utakaotetereka tupige kazi kwa bidii.
Upata hela ya kula
 

Similar Discussions

64 Reactions
Reply
Back
Top Bottom