Juma Duni Haji: CCM wameungana kwa ajili ya Urais 2015 si kutumikia wananchi

kapotolo

JF-Expert Member
Sep 19, 2010
3,727
2,214
Wazir wa Afya (siha) wa Serikali ya Umoja wa kitaifa Zanzibar ndugu Juma Duni Haji akihojiwa katika kipindi cha Saa ya Hamza Kasongo (Hamza Kasongo Hour) cha channel 10 alisema mkutano wa 8 wa CCM huko Dodoma ulikuwa na lengo moja la kuwaunganisha wana CCM kwa lengo la kushinda Uchaguzi wa 2015 lakini si kujenga chama cha kutumikia wananchi.

Alisema wamegundua kwa mgawanyiko uliopo ndani ya chama hawataweza kushinda uchaguzi. Hawana nia ya dhati ya kutumikia wananchi, na hizi ziara zao mikoani ni danganya toto ndio maana hata baadhi ya mawaziri wameanza kuzikwepa.

Ndugu Duni alitumia fursa hiyo pia kuzungumzia uhuru wa Zanzibar na kuwaomba wazanzibar waliopewa vyeo wasikubali kuwa na akili za samaki kwani hivyo vyeo ni chambo kitakachowanasa kwenye mtego wa kushindwa kuitetea Zanzibar yao.

Pia alikanusha vikali CUF kuhusishwa na uamsho na akamtetea pia Rais mstaafu Amani Abeid Karume kuhusu kuhusishwa kwake na uamsho na akatoa tafsiri tano za nini alikimaanisha Rais Karume alipowaambia wanzanzibari wasiwe na akili kama za samaki.

Moja ya tafsiri hizo ni kukubali kumeza chambo na ndoana za vyeo kwenye serikali ya muungano na kushindwa kutetea Uzanzibari.
 
pamoja na kuwa siutaki muungano ila kuna kiasi fulani niliungana na juma duni haji.
ccm wamepotea njia,wanapeleka ziara mikoani kuelezea mafanikio ya serikali utafikiri serikali imepewa ridhaa na wananchi kufanya mambo ya kiroho yanayohitaji imani kuyajua.
 
Mpuuzi tu huyu. Mbona chama chake cha CUF kina ubaguzi dhidi ya W akristo? Rejea kauli ya Jussa.
 
Hawa wapemba watu wa ajabu sana. Wanaupenda sana uzanzibari wao, lakini juzi nimemshangaa sana mmoja wao. Hamd Rashid kafiwa na mke wake maazishi yakawa Dar. Hivi kweli wanamaanisha wanachokihubiri?
 
Mpuuzi tu huyu. Mbona chama chake cha CUF kina ubaguzi dhidi ya W akristo? Rejea kauli ya Jussa.

mbona chama chako kina ubaguzi dhidi ya Waislam, Rejea kauli ya Mkwe wa mwenyekiti na mwasisi wa chama chako!
 
Hawa wapemba watu wa ajabu sana. Wanaupenda sana uzanzibari wao, lakini juzi nimemshangaa sana mmoja wao. Hamd Rashid kafiwa na mke wake maazishi yakawa Dar. Hivi kweli wanamaanisha wanachokihubiri?

labda huyo mkewe alikuwa mtanganyika..
 
Hawa wapemba watu wa ajabu sana. Wanaupenda sana uzanzibari wao, lakini juzi nimemshangaa sana mmoja wao. Hamd Rashid kafiwa na mke wake maazishi yakawa Dar. Hivi kweli wanamaanisha wanachokihubiri?

Kwa nini humshangai baba yako wa Taifa pamoja na kelele nyingi za Ujamaa na kujitegemea kaenda fia kwenye Taifa la kibepari alilowahi hata kufikia kuvunja nalo uhusiano wa kibalozi 1965 Uingereza?
 
Kwa nini humshangai baba yako wa Taifa pamoja na kelele nyingi za Ujamaa na kujitegemea kaenda fia kwenye Taifa la kibepari alilowahi hata kufikia kuvunja nalo uhusiano wa kibalozi 1965 Uingereza?

Alizikwa huko huko?
 
Hawa wapemba watu wa ajabu sana. Wanaupenda sana uzanzibari wao, lakini juzi nimemshangaa sana mmoja wao. Hamd Rashid kafiwa na mke wake maazishi yakawa Dar. Hivi kweli wanamaanisha wanachokihubiri?

Kwani Juma Duni pia Mpemba? Sijui kama unajua kama Juma Duni ni mtoto wa Dada yake aliyekua Raisi wa awamu ya tano Salmini Amour Juma ambaye anatoka Mkwajuni Kaskazini ya Unguja
 
Kwani Juma Duni pia Mpemba? Sijui kama unajua kama Juma Duni ni mtoto wa Dada yake aliyekua Raisi wa awamu ya tano Salmini Amour Juma ambaye anatoka Mkwajuni Kaskazini ya Unguja
Mtoto wa dada yake Salmin? Hivi Duni hakuwa miongoni mwa waliowekwa kizuizini na Salmin?
 
CCM ni Kama Mama au bibi mwenye miaka (60 - 70) ambaye anataka aolewe na kijana wa miaka 20,wakati akijua kuwa hataweza kumzalia kijana wa watu,watakao itoa CCM sio watu wazima,ila ni vijana ambao watajiandikisha na wale waliopoteza kadi wakijiandikisha!!!!!!!! Juma Duni alivyoteswa na CCM hakustahili ashirikiane nao.
 
Juma Duni haji Kasema kweili CCM ni chama cha Kushinda Uchaguzi hakina agenda nyingine! Jana nimeshuhudia doa ya UHURUTO yaani Uhuru na Ruto Kenya Lengo wameungana kwakuwa WOTE wali ni Watumiwa wa ICC. Watanzania tuelewe mapatano ndani ya CCM nia yao kubwa ni kushinda 2015 na wao wanasema hilo bila aibu. Ndiyo maana wanaogopa kuwagusa hata watuhumiwa wa ufisadi kwani wanamchango mkubwa ktk ushindi wa 2015.
 
Mpuuzi tu huyu. Mbona chama chake cha CUF kina ubaguzi dhidi ya W akristo? Rejea kauli ya Jussa.

Maoni ya Jussa siyo ya chama mkuu, kila mtu ana maoni na fikra zake km ilivyoainishwa kwenye Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa TZ, so mawazo ya mpuuzi yapuuzie.
 
kapotolo Thats true mkuu,badala ya kutekeleza ilani yao ya uchaguzi ya mwaka 2010 wao wako busy kujiandaa na next election, so bad!!!!!!
 
Last edited by a moderator:
Mpuuzi tu huyu. Mbona chama chake cha CUF kina ubaguzi dhidi ya W akristo? Rejea kauli ya Jussa.

kauli za kijinga na dharau kwa watu wazima ziaashiria JF kuingiliwa na watu wasiokuwa na nidhamu, Kumdharau Juma Duni Haji ni wehu uliopitiliza kwenye siasa za mageuzi, mzee huyu kasota ndani miaka na miaka kwa kupigania demokrasia, hata kama una maoni tofauti naye acha kutukana huu uhanaharakati wa ovyo ovyo bila heshima ni ujinga.
 
CCM itapita 2015 hata tukimchukua shibuda na kumweka kuwa mgombea. Tutagombana na kutengana lakini akishapatikana mgombea basi atapata support ya wote.
 
Back
Top Bottom