Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Akiongea na BBC Juma Duni Haji "Babu" amesema wameshinikiza tume huru ya uchaguzi na katiba mpya kwa kuwa iliyopo inafanya kazi kama kamati ya CCM kwa kukipendelea chama hicho kikongwe.
Duni akiongea kwa "points" amesema kuwa hata katiba ya nchi iliyopo sasa bado inaegeamea mfumo wa kizamani wa chama kimoja.
"...tume iliyopo sasa haikidhi matakwa ya mfumo wa vyama vingi kwa kushindwa kusimamia majukumu yake kwa uadilifu..." alisema Duni.
Aliongeza kuwa katika chaguzi ndogo zilizofanyika hivi karibu kumekuwa na dosari kubwa hasa idadi ya wananchi wanaojitokeza katika kupiga kura ni tofauti na ile ya wale walioandikishwa kwa kutofikia hata nusu.
"...hii inaonyesha udhaifu mkubwa kwa tume ya uchaguzi... na sisi tukiomba tuonyeshwe daftari tume haitaki kwa kudai kuwa ni kazi zao, tukiwauliza kwa nini idadi ya watu waliojitokeza kupiga kura ni chini ya nusu ya walioandikishwa tume haiotoi jibu.." alihoji "babu" Duni.
Naye Katibu Mwenezi wa chama cha Mapinduzi, Capt. John Chiligati amesema kuwa wapinzani wasitafute mchawi bali watumie muda huu kufanya mambo ya maana zaidi kujiimarisha.
"...ningekuwa mimi ndo Rais Kikwete ningewaingiza wapinzani wote katika tume ya uchaguzi na bado CCM ingeshinda tu..." alisema Chiligati kwa kujilabu.
Duni akiongea kwa "points" amesema kuwa hata katiba ya nchi iliyopo sasa bado inaegeamea mfumo wa kizamani wa chama kimoja.
"...tume iliyopo sasa haikidhi matakwa ya mfumo wa vyama vingi kwa kushindwa kusimamia majukumu yake kwa uadilifu..." alisema Duni.
Aliongeza kuwa katika chaguzi ndogo zilizofanyika hivi karibu kumekuwa na dosari kubwa hasa idadi ya wananchi wanaojitokeza katika kupiga kura ni tofauti na ile ya wale walioandikishwa kwa kutofikia hata nusu.
"...hii inaonyesha udhaifu mkubwa kwa tume ya uchaguzi... na sisi tukiomba tuonyeshwe daftari tume haitaki kwa kudai kuwa ni kazi zao, tukiwauliza kwa nini idadi ya watu waliojitokeza kupiga kura ni chini ya nusu ya walioandikishwa tume haiotoi jibu.." alihoji "babu" Duni.
Naye Katibu Mwenezi wa chama cha Mapinduzi, Capt. John Chiligati amesema kuwa wapinzani wasitafute mchawi bali watumie muda huu kufanya mambo ya maana zaidi kujiimarisha.
"...ningekuwa mimi ndo Rais Kikwete ningewaingiza wapinzani wote katika tume ya uchaguzi na bado CCM ingeshinda tu..." alisema Chiligati kwa kujilabu.