Julius Nyerere: Tunakataa na tunapinga kabisa hii tabia ya Mtu kufukuza Mfanyakazi

Kuna kamsemo kamoja nimekasikia kuwa msiwaite watu nyumbu ila waacheni matendo yao yaonyeshe kuwa wao ni nyumbu na huo ndio ubinadamu hahahahhaha
 
Maneno haya ya mwalimu ndio yalifanya utendaji kazi nchi hii udorore. Sheria alizotunga za kumlinda mfanyakazi ndio zilifanya tija ikapungua sana nchi hiikwa sababu ya vikao vya kujadili mfanyakazi aliyefanya kosa.
Mahali popote sheria za kumlinda mfanyakazi zikiwa nyingi basi tija hupungua.
Hofu ya kufukuzwa na kukosa kazi ndio inajenga nidhamu ya ufanyaji kazi. Hata mkisema inakuwa nidhamu ya woga lakini bila woga hakuna linalifanyika.
Hata kwenye familia watoro wanaogopa kuchelewa kurudi nyumba kwa hifu ya kuadhibiwa.
Tujirekebishe
 
Heshima kwenu wakuu,

Kuna sehemu nimesikia audio ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius K Nyerere akikemea Tabia ya watu kujifanya Mungu watu na kuanza kufukuza kazi wafanyakazi kisa tu wapo juu ya hao wafanyakazi. Baba wa Taifa alikemea tabia ya Mtu kujifanya anafukuza wafanyakazi kisa tu yupo juu yao.

Anaanza kwa kusema;

"Na huyu ni mtu sawasawa, ana akili sawasawa na mwenzie lakini anamwambia Mtu mwingine "Tangu leo huna kazi". Aah! bwana mkubwa, kazi ni uhai kazi ni kufa na kupona nina watoto nyumbani, unaniambia tangu leo sina kazi nifanye nini?

Lakini anao uwezo, Mtu mmoja anapewa uwezo wa namna hii wa kushiba au kutoshiba, wa kula au kutokula, wa kujua wapi pa kulala au ulale polini, anapewa mtu mmoja juu ya mtu mwingine.

Tukakataa siku za mwanzo kabisa za kupata uhuru wetu, tukageuza sheria tukatunga sheria kwa kufanya kazi iwe ni kazi ngumu sana kwa msimamizi wa kazi kumfukuza mfanyakazi, tumefanya makusudi kabisa kuweka sheria ile, lakini inalalamikiwa "Lakini wewe Mwalimu wewe rudisha unyampala bwana, mambo hayawezi kwenda vizuri. Rudisha unyampala bana, wewe ndiye umeharibu nchi unaona sasa wafanyakazi hawakubari kila mtu anajidai sana". Ulipata kuona kuna mahala watu wote wapo sawa?

sasa hili tunalikataa kabisa...KABISA...!!

Hayo yalikuwa ni maneno ya Hayati Baba wa Taifa Nyerere.

Umesikika
 
Maneno haya ya mwalimu ndio yalifanya utendaji kazi nchi hii udorore. Sheria alizotunga za kumlinda mfanyakazi ndio zilifanya tija ikapungua sana nchi hiikwa sababu ya vikao vya kujadili mfanyakazi aliyefanya kosa.
Mahali popote sheria za kumlinda mfanyakazi zikiwa nyingi basi tija hupungua.
Hofu ya kufukuzwa na kukosa kazi ndio inajenga nidhamu ya ufanyaji kazi. Hata mkisema inakuwa nidhamu ya woga lakini bila woga hakuna linalifanyika.
Hata kwenye familia watoro wanaogopa kuchelewa kurudi nyumba kwa hifu ya kuadhibiwa.
Tujirekebishe

mkuu, huo ndio msimamo wangu hata mimi. watanzania tulikuwa tumefikia pabaya sana, kina mnyika walikuwa wanamtukana tuu JK bila hofu, wafanyakazi wa UMMA walikuwa wanaboronga tuu majukumu yao bila hofu, watu walikuwa wanajichukulia tuu mikopo benki bila kurudisha, watu walikuwa wanawaza dili mwanzo mwisho bila hofu.

leo JPM anawanyoosha watu wawe na nidhamu potelea mbali hata kama ni ya uoga, kuna watu tena wenye maono yao kabisa kama kina jenerali ulimwengu eti wanabeza. WATANZANIA TUKUBALI TUKATAE, HAKUNA NIDHAMU BILA WOGA/ HOFU.

JPM awapige kwanza mkwara wa kufa mtu, watanzania wawe na hofu kuwa wakiharibu, watawajibika. ikiwakaa akilini vizuri hii, ndio utaona nidhamu inashamiri. narudia tena, HAKUNA NIDHAMU BILA HOFU, kanyaga twende JPM, hapo hapo usiachie, ikibidi kanyaga zaidi kwa nguvu zaidi mpaka watanzania tutie adabu. tumedeka mno ndio maana maendeleo yetu duni.
 
Haya mambo ya kuishi kimazoea na kuleana ndiyo yaliyotufiksha hapa! Hakuna haja ya kurudi huko tena! Tunasonga mbele! Mh. rais wapo wanaoguswa sana na jitahada zako! Ongeza bidii watakuelewa tu! Kila mahali kuna wanaochelewa kuelewa na hawa ni mmoja wa hao! Ila watakuelewa tu!
 
Hivi kuna watu wana mental constipation au, ni kwanini Cdm hutajwa tajwa hata kwenye mambo yakipuuzi yasiyoihusu bila hata chembe? Shame on u! Au hujalipwa hebu isome namba hata kwa vibration

Mkuu, tangu CDM mjitoe akili na kumsujudia Lowasa, haitatokea mkawadanganya watanzania tena wakawaelewa. mlishaga jivua nguo hadharani, kwa hiyo hamna tofauti na wehu.

kama mngekomaaga tuu vilevile na babu Slaa, ingewalipa sana siku za mbeleni kwenye siasa. ila kwa sasa mnajidanganya tuu, subiri uchaguzi huu wa madiwani na mbunge kule Dimani utaona ni kwa kiasi gani mnavyopotea. mmeshatuona watanzania hatuna akili, mnatugeuza geuza tuu kama chapati sio.?
 
mkuu, huo ndio msimamo wangu hata mimi. watanzania tulikuwa tumefikia pabaya sana, kina mnyika walikuwa wanamtukana tuu JK bila hofu, wafanyakazi wa UMMA walikuwa wanaboronga tuu majukumu yao bila hofu, watu walikuwa wanajichukulia tuu mikopo benki bila kurudisha, watu walikuwa wanawaza dili mwanzo mwisho bila hofu.

leo JPM anawanyoosha watu wawe na nidhamu potelea mbali hata kama ni ya uoga, kuna watu tena wenye maono yao kabisa kama kina jenerali ulimwengu eti wanabeza. WATANZANIA TUKUBALI TUKATAE, HAKUNA NIDHAMU BILA WOGA/ HOFU.

JPM awapige kwanza mkwara wa kufa mtu, watanzania wawe na hofu kuwa wakiharibu, watawajibika. ikiwakaa akilini vizuri hii, ndio utaona nidhamu inashamiri. narudia tena, HAKUNA NIDHAMU BILA HOFU, kanyaga twende JPM, hapo hapo usiachie, ikibidi kanyaga zaidi kwa nguvu zaidi mpaka watanzania tutie adabu. tumedeka mno ndio maana maendeleo yetu duni.
Nakubaliana na wewe kabisa. Hata nyumbani bila mkwara mambo hayaendi sembuse nchi. Ndio maana kuna sheria tena sheria kali ili kuwe na nidhamu.
 
Nyerere naye ndie alietufikisha hapa tulipo na katiba feki inayofanya inchi iwe ilivyo leo bora pombe kaleta nidhamu maofisini wewe sisi choka mbays tunaheshimika tukiingia ofisini ila bdo hili suala la simu inchi liangariwe upya bora zuziwe muda wa kazi na mwandika barua jpm maana watu wana peruzi sana.
Ila jpm naye atakwama kutokana na mfumo wa kutawala ambao hauendani na ukubwa wa inchi
 
Muda wa Nyerere ulipits na wenzake.

Hapa kazi tu

Mtamshukuru JPM mbeleni

Watanzania wavivu na wapenda dezo, huu ni mwala 2017 kama hamjajibadili...mtaji jj now.
 
Enzi za JK tulisema ni dhaifu, anahamisha na kuwalinda watumishi wabovu sasa hv tumebalisha gia angani yunawatetea tuliokua tunasema watimuliwe.................kweli siasa zimeathiri bongo zetu
Enzi za JK tulisema ni dhaifu, anahamisha na kuwalinda watumishi wabovu sasa hv tumebalisha gia angani yunawatetea tuliokua tunasema watimuliwe.................kweli siasa zimeathiri bongo zetu
Ulitegemea bavicha watapata agenda gani ya kuzungumzia utawala huu na kuikosoa serikali Mkuu?
Enzi za JK tulisema ni dhaifu, anahamisha na kuwalinda watumishi wabovu sasa hv tumebalisha gia angani yunawatetea tuliokua tunasema watimuliwe.................kweli siasa zimeathiri bongo zetu
 
Haya mambo ya kuishi kimazoea na kuleana ndiyo yaliyotufiksha hapa! Hakuna haja ya kurudi huko tena! Tunasonga mbele! Mh. rais wapo wanaoguswa sana na jitahada zako! Ongeza bidii watakuelewa tu! Kila mahali kuna wanaochelewa kuelewa na hawa ni mmoja wa hao! Ila watakuelewa tu!
Kuishi kwa mazoea kwa bahati mbaya bado kunaendelea. Rasimu ya Katiba ya Jaji Warioba ilikua ni mwarobaini. Ilipendekezwa kuundwa chombo cha kushughulikia jinsi ya kuwapta viongo waandamiz, lakini kwa sasa tuko pale pale kwenye mazoea. Unateuliwa badala ya chombo kimoja tena chenye mchanganyiko wa watu. Ni hadi pale Katiba itakapowekwa sawa. Kwa sasa mazoea yataendelea kuwepo. Inawezekana kutoa mazoea kwa usoni yakaja mgongoni, sasa hapo ni sawa na kaz bure.
 
Nyerere was the GREATEST.
Najua lengo lako ni nini,mtu pekee katika dunia hii anayestahili kuitwa GREATEST ni Mungu,unaweza tu ku edit ukaweka neno lingine la kumsifia Raisi wetu mpendwa hayati Julius K.Nyerere ili ilete maana inayokusudiwa.
 
Ni kuvuliwa madaraka tena ya kuteuliwa na rais hata nyerere aliwatumbua wengi na wengine kuwaweka kizuizini.
Hivi hujui hizo ni mamlaka tu za uteuzi,haiwezekani mkuu wa idara akateuliwa na rais,lakini yule anayemteua anafanya kwa niaba ya rais..hiyo ni sheria ya utumishi wa umma 2007 inavyosema
 
Mtoa mada ume mnukuu JKN Kwa makosa ili roho zenu ziridhike.
JKN alisema Hayo Kwa Wafanyakazi wasio Na makosa yeyeto.Hajasema Kwa Wafanyakazi walio fanya makosa.
Mtasema Na mtanukuu sanaaa tu.
 
Heshima kwenu wakuu,

Kuna sehemu nimesikia audio ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius K Nyerere akikemea Tabia ya watu kujifanya Mungu watu na kuanza kufukuza kazi wafanyakazi kisa tu wapo juu ya hao wafanyakazi. Baba wa Taifa alikemea tabia ya Mtu kujifanya anafukuza wafanyakazi kisa tu yupo juu yao.

Anaanza kwa kusema;

"Na huyu ni mtu sawasawa, ana akili sawasawa na mwenzie lakini anamwambia Mtu mwingine "Tangu leo huna kazi". Aah! bwana mkubwa, kazi ni uhai kazi ni kufa na kupona nina watoto nyumbani, unaniambia tangu leo sina kazi nifanye nini?

Lakini anao uwezo, Mtu mmoja anapewa uwezo wa namna hii wa kushiba au kutoshiba, wa kula au kutokula, wa kujua wapi pa kulala au ulale polini, anapewa mtu mmoja juu ya mtu mwingine.

Tukakataa siku za mwanzo kabisa za kupata uhuru wetu, tukageuza sheria tukatunga sheria kwa kufanya kazi iwe ni kazi ngumu sana kwa msimamizi wa kazi kumfukuza mfanyakazi, tumefanya makusudi kabisa kuweka sheria ile, lakini inalalamikiwa "Lakini wewe Mwalimu wewe rudisha unyampala bwana, mambo hayawezi kwenda vizuri. Rudisha unyampala bana, wewe ndiye umeharibu nchi unaona sasa wafanyakazi hawakubari kila mtu anajidai sana". Ulipata kuona kuna mahala watu wote wapo sawa?

sasa hili tunalikataa kabisa...KABISA...!!

Hayo yalikuwa ni maneno ya Hayati Baba wa Taifa Nyerere.

Sheria ya kazi iliyotungwa baada ya maneno hayo ilikuwa moja kati ya sheria mbaya iliyoathiri sana mazingira ya kazi, mahusiano ya kazi na ufanisi mahali pa kazi.
Ikaleta wafanyakazi wavivu, viburi na miungu watu.
Hashima ya kazi ikashuka, ufanisi ukashuka, uzalishaji ukashuka na uchumi nao ukaathirka.
Ndo chanzo pia cha ufanisi mdogo wa wafanyakazi katika sekta ya umma.
Kazi zao ni za 'milele' na matokeo tuliyaona.
Tusirudi tulikotoka kisa tu Nyerere alisema..
 
Kauli ya Nyerere haikuimarishwa na Katiba sahihi wala mfumo au utamaduni sahihi wa demokrasia. Siku tutakapokubali kuwa na uongozi unaodhibitiwa na Bunge na wananchi; siku tutakapokuwa na mfumo unaowezesha rais kuhojiwa kama ilivyotokea Argentina, Brazil na Korea Kusini ndipo maneno ya Nyerere yatakuwa na maana.

Lakini kwa kadiri tunavyoendelea kushabikia viongozi wenye mwelekeo wa kimungu; watakatifu ambao kauli yao ni Alfa na Omega, basi ni wakati muafaka wa mtu aina ya Magufuli kuwa rais wa nchi hii. And he's doing all the right stuff, by the way!
 
Back
Top Bottom