Julius Mtatiro apandisha jazba kuhusu Tamko la Chadema kutoungana na CUF Bungeni

Gurudumu

JF-Expert Member
Feb 5, 2008
2,349
261
Akiongea kwa hasira na kupanic, ameshangaa tamko la chadema eti haiwezi kuungana na CUF bara kwa sababu CUF visiwani wameungana na CCM. Hata hivyo aliahidi kwamba CUF bara itaendea kushirikiana na vyama vingine vya upinzani ili kutekeleza majukumu yake.

Source Channel ten taarifa ya habari saa moja usiku
 
mtatiro asijawe na jazba kwan cuf ni cuf tu iwe zanzibar au bara nampa pole kwa kutoswa kwajili ya maamuzi ya chama chake acha ya mkosti namfananisha na matokeo ya form four
 
Cuf si wapinzani.. Ni wakinzani.. Mtu kma Mtatiro is very potential guy hasa kwny kuongea.. I thnk angejiunga na JAHAZI ASILIA.. Coz huko ndo kuna watu wa kubwabwaja bwabwaja ovyo.. Anajua kuongea bila logic..
 
Mbona kanuni za kudumu za bunge ziko wazi kuhusu kambi rasmi ya upinzani Bungeni? Sasa Mtatiro anachokasirikia ni kipi hasa?
 
Katika wanasiasa wa kutumainiwa kwa ajili ya nchi hii Mtatiro naye yupo?!!HAPANA
Mtatiro ana sifa kuu zifuatazo, ambazo sisi tuliofanya nae siasa pale Chuo Kikuu tulimfahamu, na tukamtoa kwenye KUNDI LA WANASIASA-VIONGOZI WA BAADAE WA KTUMAINIWA NCHI HII:

1. Ni mtu wa kuongea tu kabla ya kufikiri..Hufikiria baada ya kutenda..
2. Hatumii logic, hupanic sana...
3. Ana vunga ana msimamo lakini muda wowote anakupotezeni..mfano: Tulipofanya mgomo kuishinikiza serikali kutoa kipengele cha madaraja katika kugawa mikopo, tukafukuzwa miezi miwili..katika kufanya juhudi za kuwarejesha wanafunzi wote salama, sisi vionogzi tulibaki Dar es salaam tukikutana na kujadiliana..haikuchukua muda akatukimbia na kukimbilia Kenya kwa ndugu zake..kisa uoga kwa Serikali.
4. Ni kiongozi mwenyye tamaa na ulafi wa madaraka kila alipo..wengi watakumbuka alivyomlipa fadhila Rais aliyemteua Deo Daudi, kwa kuendesha hila aangushwe madarakani.
-Vivyo hivyo aliwahi kuhatarisha serikali ya Mwita Magesa kuangushwa madarakani, wakati huo akiwa ni waziri wake..Mwita ilibidi amtimue madarakani..ingawaje huwa anatamba kuwa alipeleka barua ya kujiuzulu mapema..si kweli.
5. Ana 'madudu' yake ambayo hutaka kuyatimiza kwa gharama yoyote ile..aliwahi kuishinikiza kamati fulani ya uchaguzi pale DARUSO iwapitishe 'madada' flani kuwa wagombea...kamati ile hata hivyo iliwabwaga kwa kukosa vigezo...ile ilileta uhasama kwake na kwa wanakamati wale.

Huyo ndio 'mwanasiasa' MTATIRO KWA UCHACHE...
Hayo ya CHADEMA NA CUF ayajibu kwa hoja.......sio kuongea tu ilimradi anaongea
 
Ukiwa mtu makini kuna mambo ya kushabikia na kuna mambo ya ku reason out tatizo letu tuna mapenzi ndani ya mioyo yetu na uchangiaji mwingi unakuwa hauna tija ila ushabiki unaoambatana na maneno ya kebehi na kashfa. Itafika wakati tutakuwa real great thinkers tuta reason out na kuja na konklusheni na sio fitna na mapenzi! Ni hayo tu Magreat Thinkers wangu.
 
Nilishawahi kueleza Mtatiro CUF haimfai narudia tena Mtatiro CUF haikufai soma majira ya nyakati na ufanye maamuzi ya kuondoka CUF .......
 
Mh! Mtatiro mbona unapotea mdogo wangu? Hizo sifa za muda mfupi ulzopata usijifanya nguli, ur too young to proud as a good politician be patient mambo mazuri hayataki haraka.
 
Siamini kama Mtatiro haoni mantiki ya kwa nini CHADEMA hawataki kuwajumuisha CUF kwenye kambi ya upinzani,anachojaribu kufanya ni kutaka kutuadaa kwamba cuf zipo mbili,tena zenye misimamo na agenda tofauti.CUF ni moja na uamuzi wao wa kijinga wa kuunda serikali ya pamoja zenji,naamini uliridhiwa kwenye vikao rasmi vya chama...Kaka Mtatiro,huko hakukufai toka mapema kabla hujafulia kisiasa!
 
Huyu mtatitiro, anamatatizo makubwa sana, ambayo alisababisha matatizo mengi pale UDSM, mi namkumbuka vizuri sana, mi nawashangaa watu ambao wanamwamini mtatiro, cause hizi pumba ashaongea sana toka alivyokuwa UDSM
 
Wera wera weraaaaaaaaaaaaaa AIBU YETU AIBU YAOOOOOOOOOOOO. Mbona hawataki kuunda kambi rasimi ya upinzania SMZ (Serikali ya Mseto Zanzibar) Matatilo anakoelekea NITAANZA KUMUONA NAE CHIZI TU KAMA MACHIZI WENGINE wa kindondoni kwa manyanya
 
Katika wanasiasa wa kutumainiwa kwa ajili ya nchi hii Mtatiro naye yupo?!!HAPANA
Mtatiro ana sifa kuu zifuatazo, ambazo sisi tuliofanya nae siasa pale Chuo Kikuu tulimfahamu, na tukamtoa kwenye KUNDI LA WANASIASA-VIONGOZI WA BAADAE WA KTUMAINIWA NCHI HII:

1. Ni mtu wa kuongea tu kabla ya kufikiri..Hufikiria baada ya kutenda..
2. Hatumii logic, hupanic sana...
3. Ana vunga ana msimamo lakini muda wowote anakupotezeni..mfano: Tulipofanya mgomo kuishinikiza serikali kutoa kipengele cha madaraja katika kugawa mikopo, tukafukuzwa miezi miwili..katika kufanya juhudi za kuwarejesha wanafunzi wote salama, sisi vionogzi tulibaki Dar es salaam tukikutana na kujadiliana..haikuchukua muda akatukimbia na kukimbilia Kenya kwa ndugu zake..kisa uoga kwa Serikali.
4. Ni kiongozi mwenyye tamaa na ulafi wa madaraka kila alipo..wengi watakumbuka alivyomlipa fadhila Rais aliyemteua Deo Daudi, kwa kuendesha hila aangushwe madarakani.
-Vivyo hivyo aliwahi kuhatarisha serikali ya Mwita Magesa kuangushwa madarakani, wakati huo akiwa ni waziri wake..Mwita ilibidi amtimue madarakani..ingawaje huwa anatamba kuwa alipeleka barua ya kujiuzulu mapema..si kweli.
5. Ana 'madudu' yake ambayo hutaka kuyatimiza kwa gharama yoyote ile..aliwahi kuishinikiza kamati fulani ya uchaguzi pale DARUSO iwapitishe 'madada' flani kuwa wagombea...kamati ile hata hivyo iliwabwaga kwa kukosa vigezo...ile ilileta uhasama kwake na kwa wanakamati wale.

Huyo ndio 'mwanasiasa' MTATIRO KWA UCHACHE...
Hayo ya CHADEMA NA CUF ayajibu kwa hoja.......sio kuongea tu ilimradi anaongea

mtafute SHIGONGO kipaji unacho mkuu naona unavyomwaga data za udaku..
 
Mbona wameungana na CCM kuunda kambi ya utawala bungeni..... sasa wanataka kuja na huku ili kujua kila tunalopanga??? Wafie mbali
 
Ukiwa mtu makini kuna mambo ya kushabikia na kuna mambo ya ku reason out tatizo letu tuna mapenzi ndani ya mioyo yetu na uchangiaji mwingi unakuwa hauna tija ila ushabiki unaoambatana na maneno ya kebehi na kashfa. Itafika wakati tutakuwa real great thinkers tuta reason out na kuja na konklusheni na sio fitna na mapenzi! Ni hayo tu Magreat Thinkers wangu.

Mkuu hilo haliwezekani hapa, ni lazima watu wawe na mapenzi na watetea upande wao. Bora tu wewe ungetoa mawazo yako kama unadhani kwamba CUF inaweza kuwa chama tawala Zanzibar na wakati huo huo kikawa chama cha Upinzani Bara. Ukizingatia chama kinachotawala Zanzibar ndicho kinachotawa bara.
 
Lakini, kwa kuwa huko zanzibar CUF wameungana na chama tawala, kwa nini huku Bara pia wasiungane na chama tawala? Wakifanya hivyo yaani watapata misuli mikubwa ya kukiteketeza kabisa Chadema. Au?
 
Bwana mtatiro nadhani anaanza kupoteza uwezo wa kufikiri kama ni kweli amepatwa na hasira kwa chadema kukataa kujiunga na chama chao cha CUF. maana kwa mtu makini na anae fikiria vizuri, huwezi ukakasirika kwa chadema kuwakataa cuf kuunda kambi moja ya upinzani bungeni.ki msingi mwenyekiti wa cuf bara na visiwani ni prof lipumba, na mwenzake ni huyo wa visiwani ambae amekula shavu ndani ya serikali, sasa kama cuf zanzibar imo ndani ya serikari iweje wawe wapinzani? mtatiro soma alama za nyakati na utoke cuf kama kweli wewe ni mpinzani la sivyo unatudanganya watanzania.
 
Siamini kama Mtatiro haoni mantiki ya kwa nini CHADEMA hawataki kuwajumuisha CUF kwenye kambi ya upinzani,anachojaribu kufanya ni kutaka kutuadaa kwamba cuf zipo mbili,tena zenye misimamo na agenda tofauti.CUF ni moja na uamuzi wao wa kijinga wa kuunda serikali ya pamoja zenji,naamini uliridhiwa kwenye vikao rasmi vya chama...Kaka Mtatiro,huko hakukufai toka mapema kabla hujafulia kisiasa!

Labda anasubili kuwa kama Augostine Lyatonga Mrema aanze nae kubwabwaja..... kwa sasa awezi kuwabadilisha vijana wa kizazi hiki maana mtazamo wa vijana na wasomi ni kuwa pamoja SIO kuparaganyika tena.

Mtatiro sisi tutaenda na CHADEMA mpaka tuone mabadiliko ndo tutakuja kwako... sijui utakuwa na umri gani

Ondoka sasa ili tuweze kula matunda ya mageuzi pamoja ndugu yangu
 
Back
Top Bottom