Jukwaa la Wahariri wampiga BAN Mkuu wa Mkoa wa Dar kwenye Media zote nchini

Tatizo hata media nazo hazina habari zaidi ya makonda na gwajima. Haya sasa waandike za gwajima zitasomwa. Wamepotea
 
Habari sasa hivi zitadoda. No speaking abt makonda anymore na gwajima amesmema hana ugomvi binafsi na paulo. Mwisho wa sinema ya kihindi!
 
deal done..nchi ya ajabu sana hii...sasa wasipomuandika si ndio atafanya anavyoweza!tujiulize bila vyombo vya habari kuripoti tukio la kuvamiwa clouds tungelijuaje?hapa ni kumpa rungu afanye atakavyo.
Kama tutamwandika kwa kuwa kafanya uhalifu ni ruksa na huko si kumpa ushirikiano bali kumfichua mhalifu.
"La Clouds ni uhalifu, la kuzindua barabara au kuhamasisha usafi ni kumpa ushirikiano." Umeelewa?
 
Sasa hivi Makonda ana bad publicity!

Anapata negative press coverage.

Sasa ukimuondolea press coverage unampunguzia nini?
Hawaandiki habari zake wakimaanisha press conference zake na press releases kwa ufupi hawaandiki any news INITIATED BY MAKONDA kwa makonda hii ni blow maana kila alichofanya ikiwemo ziara sijui siku ya usafi na sijui vita ya madawa almost 80% ya kazi zile ilikuwa kwenye media zaidi.......... so ana mengi ya kupoteza.

NOTE: naomba ieleweke ambacho wanasusa ni kuandika habari ambazo ZIPO INITIATED NA MAKONDA ila ikandikwa from a point of view ya nape au gwajima au wao wenyewe itaandikwa
 
Pongezi kwao pia walichewa kutoa maamuzi ndio vizuri hatutoona ujinga wake wa kushikiwa mianvuli na watu walomzidi umri!
 
Wahariri wana njaa sana. Agizo hilo haliwezi kutekelezeka...

Waliwahi kufanya hivyo kwa Juma Nkamia, Tulia Ackson wakaishia wapi?....

Kuna njaa mbaya sana ndani ya media industry. Hilo haliwezekni
na hii inaitwa uvamizi wa makonda clouds nakwambieni source ni njaa ya waandishi wa habari.
 
Vyombo vya habari vina nafasi kubwa sanaa kukuza uchumi wa nchi yetu kutoka sehemu flani mpaka sehemu flani kama vitatumiwa vizuri na wamiliki wenye maono ya maendeleo na sio kisiasa au kwa upendeleo wa aina yoyote ya kundi flani kwenye jamii yetu.

Binafsi sielewi hii nguvu inayotumika na wamiliki wa vyombo vya habari kwa RC wa Dar kama ni sahihi, hivi ni kweli ni kipaumbele cha vyombo vya habarii ni ya makonda na cheti na kwenda clouds(simsapoti makonda) ndo vipaumbele vya habariiiii kwa siku za karibuni....
Naona giza kubwa sanaaa miaka miwili ijayo kila mtu anatumia mgongo wa DINI na maneno ya dini kufikisha ujumbe kwa kutuaminisha yupo sahihi...
Tanzania tumepoteza dira na mwenye dira anajibu mambo ya social media na kuyakataa mwenyewe.

MUNGU LINDA LILILOJEMA NA LAANI LILO NYUMA YA PAZIA TUSILOLIONA NA WASILO LIZUNGUMZA MBELE YETU.
 
TAARIFA KWA WANAMITANDAO.

Ndugu wana mitandao kwa niaba ya wamiliki wote wa akaunti za mitandao yote ya kijamii tumesikitishwa sana na tukio la uvamimizi uliofanywa wa Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Ndugu Paul Makonda kwa kitendo cha Kinyama kuvamia kituo cha habari Clouds Media Group.

Kitendo hichi ni cha kinyama kwani ameingilia uhuru wa habari na kuvunja vifungu vya katiba jambo hili haliwezi kuvumilika kamwe kwetu sisi wanamitandao.

Tunapaswa kujiuliza kama ameweza kuvamia kituo kikubwa kama Clouds sisi wanamitandao Uhuru wetu upo shakani hakuna wa kututetea tutaishia jela, tunapaswa kuwa na umoja na kamwe tusipuuze kwamba hili haliwezi kutufika madhara ni kwa kila mmoja wetu.

Anapaswa kujitathimini na kujipima kwanza kama anatosha kwenye nafasi au hatoshi kwanza. Tulianza kwa kumdai vyeti akagoma kuviweka hadharani sasa tumeamua kwa umoja wetu kutofuatilia habari yake yoyote katika mitandao ya kijamii.

Kuanzia siku ya leo wito wetu kwa kila mwanajamii ni kuacha kabisa kumfollow na kufuatilia juu ya habari zake yeye pamoja na washirika wake waliosapoti kitendo hiki cha kinyama.

Tumeianza kampeni [HASHTAG]#UNFOLLOWMAKONDA[/HASHTAG] katika akaunti zake zote za mitandao ya kijamii kuanzia Instagram, facebook, pamoja na Twitter naimani hili litatekelezeka tumeanza na MAKONDA tunaondoka na BASHITE mwanzo alisema wote wanaowafollow mashoga wakamatwe na sisi tunasema atakaye mfollow Bashite atengwe na jamii.


KWENYE MITANDAO KUNA KELELE NA TUPAZE KELELE ZETU KWA KUMU-UNFOLLOW PAUL MAKONDA.
 
afanye madudu halafu eti tunyamaze tu
kuanika na kusema anayofanya kinyume na taratibu za nchi ni lazima
acha kutupandikiza ujinga wewe

hakili za kukopa hizi ndo zinakusumbua mbwa kinda wewe
 
Makomda asipo andokwa..mtamtafuta hadi kwaa mguu

Ashakuwa maarufu

Mchana niliona baadhi ya mitandao wamefuta..cha kushangaza watu wanaendelea kuandika hadi saa izi 6:57 pm.
 
Issue sio cheti wala nini ni uhuru wa vyombo vya habari. Hii ni issue kubwa sana sana kama kuna mtu hujaona hilo basi una upeo mdogo sana. visingizio vya kusema tuongelee uchumi sasa kuna haraka gani mambo yote yanaweza kuongelewa. vilevile uchumi gani wa kuongelea ?? kuna nini cha kiuchumi kipya barabara lol!!
 
Back
Top Bottom