Jukwaa la wahariri wagomea kuandika habari zote za jeshi la polisi

Hivi Ma Polisi hawana mwenyewe wala hawana miiko ya kazi yao?naona wanaua tu na hakuna lolote hata kuonywa!ni aibu sana kwa jeshi la Police na IGP wao...
 
hiyo inaitwa kibanga ampiga mkoloni. Toka jana nasema hawa waandishi pia ni tatizo. Huwa wanajifanya kimbelembele sana tena sana hasa hawa wahariri kwa kupindua pindua au kutoandika kabisa habari za waislam, ivi na kikao cha kutoandika au kugeuzageuza habari za waislam walikaa ni lini na tatizo ilikuwa ni nini? Hao wahariri si ndio wale waliambiwa na mwarabu wa richmond waache kamera zao nje? Hao wahariri njaa wanafiki wakubwa, wahariri wamejikita kuandika mambo ya kugombanisha umoja wa watanzania. Wahariri hata wakijifanya eti wameweka hivyo vikwazo je na watbc hawatoripoti? Tbc iko nchi nzima na wanawaandishi wao pia jeshi lina waandishi wao. Kama wanaubavu wageuze habari yoyote ya polisi waiandike tofauti na ilivyotokea tuone itakuwaje. Wahariri wanafiki
Watu wanaongelea habari za msiba, wewe unaleta habari za dini fulani, hivi wewe kweli una akili??
 
Aandikeni kwa nguvu sasa habari za manyanyaso ya wananchi kwa kukosa huduma iili jeshi la polisi lipate nyumba za kuishi, kumbe ni kuibua hasira za kuua- huu ni moyo wa jeshi lisilo na displine kwa wakuu wa kazi
 
Hivi kutikuandika habari za polisi ni kuliadhibu jeshi la polisi au kuwaadhibu watu wanaohitaji hizo habari?
 
...Mkuu drKupeng'e kwenye vita dhidi ya udhalimu hakuna kinachoshindikana. Kutoandika habari za Serikali hii dhalimu na magamba yao hakutaathiri kabisa mauzo ya magazeti, hivyo hili linawezekana kabisa kama wanahabari wakiamua nao kupambana kabla ya mwingine miongoni mwao kuuwawa kinyama kama Mwangosi.

Not possible hapa
 
Ipo TBC itafanya kazi kwa niaba yao...! Mbona walishawahi kugomea kuandika za Magereza, kwani waliishia wapi?
 
Nakumbuka Pasco alisema waandishi hawaandiki kitu mpaka wapewe "bahasha ya khaki". Hapa huu mgomo unachodai ni dau la bahasha kuongezwa tu. Watu wazima washaelewa tatizo liko wapi.
 
Last edited by a moderator:
Nadhani ni kuchukua maamuzi mapema, mimi nashauri, hakuna aja ya kufanya uchunguzi, maana picha zipo wazi kabisa. Mimi nadhani watupe maamuzi full stop. Na mimi nashauri azimio liwe ni kususia habari za jeshi la polisi.
 
Nadhani jukwaa la wahariri mnalotakiwa kufanya ni kukusanya ushaidi na kulishitaki jeshi la polisi nadhani hilo linawezekana,najua mkiwashitaki mtapata msaada mkubwa kutoka kwa wananchi na wanasheria wenye mapenzi mema.
 
Imani ya watanzania ni kwa tume iliyoundwa na waandishi wa habari, nadhani watajituma na kufanya uchunguzi kwa moyo wa kujitolea bila kurubuniwa kwa gharama yoyote ile, bila kuogopa kupelekwa msitu wa pande!
Mungu yupo upande wao nasi tunawaombea watuletee majibu yenye tumaini kwa watanzania ili tuwabaini majambazi hawa wanaoongozwa na Kikwete na timu yake!
 
TAMKO LAINI SANA HILI UKILINGANISHA NA TUKIO LENYEWE... HATA NYIE WAANDISHI HAMNA CHOCHOTE WENGI WENU MNATUMIKIA MATUMBO YENU TU. RIP DAUD MWANGOSI wewe umeifia taaluma yako na hukukubali kutumikia wakubwa na tumbo MUSHI na FRANCIS msitishike kazeni uzi bila kuangalia nyuma yenu yuko nani ila tuko nanyi.
 
Nakumbuka Pasco alisema waandishi hawaandiki kitu mpaka wapewe "bahasha ya khaki". Hapa huu mgomo unachodai ni dau la bahasha kuongezwa tu. Watu wazima washaelewa tatizo liko wapi.
Mkuu Ze Marcopolo, naomba unikumbushe lini na wapi niliwahi kusema "waandishi hawaandiki kitu mpaka wapewe "bahasha"?.

Mimi ni mtetezi wa bahasha halali za waandishi ambazo ni stahili zao!, nisome HAPA nimeeleza kila kitu!.[FONT=Helvetica, Calibri, Verdana, Geneva, sans-serif]
[/FONT]
 
Back
Top Bottom