Jukwaa Huru la Wazalendo latoa maoni serikali kuhamia Dodoma

Andrew Kadege

Member
Jan 1, 2016
6
5
JUKWAA HURU LA WAZALENDO TANZANIA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

TAMKO LA KUUNGA MKONO UAMUZI WA SERIKALI KUHAMIA DODOMA

Ndugu waandishi wa habari, Jukwaa limewaita mahali hapa kuunga mkono na kumpongeza Mhe. Rais John Pombe Magufuli kwa uamuzi wake wa kihistoria wa kutangaza Serikali kuhamia Dodoma.

Uamuzi huo mzito ni kutimiza ndoto ya kizlendo na kiu kubwa si tu ya muasisi wa Taifa letu, Baba wa Taifa, Mwalimu J. K Nyerere bali shauku ya Watanzania wengi tuliokuwa tunasubiri jambo hili kutimia.

Ndugu waandishi wa habari, mtakumbuka kuwa suala la kuhamia Dodoma lilibaki kiporo tangu Rais wa Awamu ya Kwanza hivyo kwa uamuzi huu wa kuhamia Dodoma ni kututhibitishia kuwa Rais Magufuli ni mtu wa vitendo na siku zote anatazama maendeleo na si siasa.

Kwa kasi hii sisi tunachukua fursa hii kumpa pongezi na kumtia moyo aendelee hivyo hivyo kutufanya wananchi wake kuwa na matarijio makubwa sana katika kutekeleza ahadi zake nyingi na kuivusha nchi.

Ndugu Wana habari,tunasisitiza tena na kama alivyoass pia Mzee wetu Rais Mstaafu Ally Hassan Mwinyi mjini Dodoma, kwa kiongozi kama huyu, Watanzania wenzangu hatuna chaguo lingine zaidi ya kumuunga mkono na kumsaidia afikie dira yake.

Pia Jukwaa tunampongeza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa kuonesha njia na utekelezaji wa haraka wa Agizo la Rais kwa kuagiza mawaziri kuhamia Dodoma haraka.

Tunamalizia kwa kusisitiza kwa watanzania wenzetu kwamba kwa kasi na nia njema hii ya Serikali ya Awamu ya Tano hatuna chaguo lingine muafaka zaidi ya kuungana na viongozi wetu hawa katika safari hii ya mabadiliko.

Ahsanteni sana

Imetolewa leo Dar es Salaam
28/07/2016
Andrew Kadege
0756 911 342
M/kiti wa Jukwaa Huru La Wazalendo Mkoa wa DSM.
 
Propaganda at its best ....!!

Kama wangekuja na faida za Kisiasa, Kiuchumi na Kijamii kwenye tamko lao walau ningewaelewa!!

Kwa hiyo Rais ameamua kuhamishia makao Makuu Dodoma ili kutimiza Ndoto za Mwalimu Nyerere!!
 
Naifikiria Dsm ya miaka mitano baadae,na yale magorofa ya posta,nabaki kuona huruma kwa wawekezaji waliojenga hivi karibuni,walipaji wakubwa wa majengo Yale ni ofisi za serikali,nabaki kushangaa tu,
Lakini ndio hivyo,wale ambao tayari mmeshapata barua za kuhamia dodoma mpo?mnajisikiaje?
 
Usifananishe hivyo MKUU uchumi wa Nigeria sio kama wa Tanzania .Hofu yangu Kwa wanaoondoka Viwanja vyao tutaviuza haraka sana
 
Sio rahisi kbsa,biashara nyngi zinategemea zabuni za gvt,jaribu kufikiria kama wizara zote zitaondoa wafanyakazi wake hapa mjini hali itakuwaje?
Dar itaendelea kuwa kitovu cha uchumi wa nchi hii kwa sababu ya mazingira yake na miundo mbinu, hilo halipingiki lakini lisizuie azma ya kuhamia Dom
 
Hilo nalo neno. Nasubiri nitumie dakika 15 mpaka nyumbani. No foleni!!!!!
Swali la kizushi hivi kama taifa tumesimamia kwa sasa
1.Serikali kuhamia Dodoma?
2.Kufufua Viwanda ili tuzalishe na kuuza nje?
3.Kutumbua majipu ya mafisadi?
Mana yooote hayo ni process sio kukurupuka huku.
 
Katika moja ya hotuba zake Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alipata kusema "......katika utawa wangu yapo mambo mazuri tulifanya, lakini pia yapo mambo ya hovyo hovyo tulifanya! Ndiyo tulifanya!!! Sisi ni binadam............... tulifanya! "

Mwalimu alisema katika hotuba ile kuwa alitarajia kuwa tawala baada yake zingeyachukua yoote mazuri yaliyofanywa na utawala wake na kuyaendeleza huku yale ya hovyo hovyo yakitupiliwa mbali.

Akistaajabia kuzikwa kwa azimio la arusha akasema anashangaa kuona mambo mazuri waliyoyafanya ndio yanaachwa na yale ya hovyo hovyo ndio tunayaendeleza.

Tayari mziki wa Dar mpaka Dom unarindima.

Je Mwalimu alitumia vigezo vipi kulinganisha jambo la hovyo na jambo zuri?

Kwa muktadha huo, tumejithibitishiaje kuwa tunaendeleza jambo zuri la Mwalimu Nyerere la kuhamia Dodoma (ambalo halikutekelezwa kwa kwenye zama za Mwalimu, Mwinyi, Mkapa na Kikwete)

Au tunaendeleza jambo la hovyo na tunashindwa kumwambia Amiri jeshi mkuu wetu?


 
Dodoma ni Tanzania, itajengwe na wataz,Uamzi uko sahihi wa kuhamia Dom.Mtoto akishazaliwa,huchukua hatua kwa hatua ktk ukuaji,Naipongeza Serikali kwa uamzi wa sasa, baada ya kuhamia changamoto zitakazojitokeza,tutakabiliana nazo hatua kwa hatua.Kumbuka maendeleo hayana mwisho.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom