Jukumu la kumsafisha mtoto pale anapojisaidia ni la mama peke yake?

lwambof07

JF-Expert Member
Jul 12, 2016
4,593
5,202
Habar JF

Wote tunajua kuwa suala la kulea mtoto ni jukumu la wazazi wote baba na mama, hakuna kitu kinaboa na kuchosha kama kuhakikisha mtoto yupo msafi muda wote, wakina mama hubadilisha nepi hadi huchoka na kuamua kuacha tu na kuangalia unakuta dogo nguo yake imeloa mikojo na wengine hadi inaanzia kutoa harufu.

Zishukuriwe pampasi kwa sababu hiyo mtoto akipigwa kuja kumtoa sio leo.

Wababa wengi huwa hawapendi kabisa kuwasafisha watoto wao pale wanapokuwa wameharibu mambo iwe haja kubwa au ndogo ila hasa hasa haja kubwa hii ndogo anaweza akavumilia.

Unakuta baba kashika mtoto au anacheza na mwanaye yaan dogo akishajisaidia tu utamsikia we mama fulani mwanao amejinyea huku njoo umchukue.Baba yeye anapenda kucheza na mwanaye akiwa msafi tu akishaharibu mambo kosa hilo.

Kwani baba fulani ukimsafisha utapungukiwa na nini huwezi kumsafisha mtoto wako hadi umuite mama watoto??au kumsafisha mtoto hilo ni jukumu la mama peke yake baba halimuhusu??

images (35).jpg


images (34).jpg


images (33).jpg


images (32).jpg


baby-diaper-changing--157636249-59790b20aad52b0011b1b537.jpg


images (30).jpg


images (31).jpg
 
Mpaka uwe unajua mkuu, kuna watu malezi yao ya hovyo sana hata kumwogesha mtoto hawezi.

Mtu kama unajua kupika kuna siku utapika bila hata kuombwa na mkeo,kama unajua kuogesha utaogesha watoto hii pia inajenga ukaribu zaidi na mtoto.

Unakuta mama anapika halafu mtoto kaharibj mazingira,unamwita aje kumsafisha,unataka kutengeneza kitu gani hapo kati!!!
 
Wanaume Wana kinyaa na kukwepa majukumu ndio wajue ulezi ni kazi ngumu, pia kumsafisha mtoto na ku take care huwa ni bonding nzuri, na wengi Wana okwepa ndio baadae hulalamika watoto huwa side na mama kuliko wao
 
Ukitaka kupata jibu hilo ebu angalia michezo ya watoto wa kiume na wakike mingi utofautiana na hakuna aliyewafundisha wanajifunza wenyewe

Kwa hiyo kwenye majukumu ya kulea familia ni mama na mwenye majukumu ya kuhudumia familia ni baba japokuwa wote wanategemeana

Ila wanaweza kusaidiana kulingana na mazingira na malezi waliyokulia

Ila dunia imelikataa hilo wanataka mambo yawe changanyikeni. ""eti nimuogeshe mtoto wakati mama yake yupo bize anasuka"" ukiona unafanya hayo basi jua tayari ulishakunywa chai ya chupi
 
mpaka uwe unajua mkuu,kuna watu malezi yao ya hovyo sana hata kumwogesha mtoto hawezi.

mtu kama unajua kupika kuna siku utapika bila hata kuombwa na mkeo,kama unajua kuogesha utaogesha watoto hii pia inajenga ukaribu zaidi na mtoto.

unakuta mama anapika halafu mtoto kaharibj mazingira,unamwita aje kumsafisha,unataka kutengeneza kitu gani hapo kati!!!
Na hilo ulilosema ndilo linalofanyika sasa hata awe na kazi aisee ataitwa tuu
 
Wanaume Wana kinyaa na kukwepa majukumu ndio wajue ulezi ni kazi ngumu, pia kumsafisha mtoto na ku take care huwa ni bonding nzuri, na wengi Wana okwepa ndio baadae hulalamika watoto huwa side na mama kuliko wao
Duh kinyaa tena ndiyo mwanao huyo sasa
 
Back
Top Bottom