sammosses
JF-Expert Member
- Jan 24, 2011
- 1,682
- 1,110
Ni majira ya saa tisa na dakika ishirini msafara wa mh.Lowasa uliingia kwenye manispaa ya Shinyanga mjini ukiongozwa na gari la askari polisi,ziara hiyo ni miongoni mwa ziara za kuchangia katika harambee za kujenga makanisa mbalimbali ikiwa ni mkakati wa kujiimarisha zaidi na kukubalika na waumini wa madhehebu mbalimabali.Duru za kisiasa mkoani humo zinazidi kutabanaisha kuwa ilikuwa harambee hiyo ifanyike jumapili iliyopita,ila kutokana na msiba mkubwa wa aliyekuwa mzazi mwenzake harambee hiyo iliahirishwa.Harambee hiyo inatarajiwa kufanyika hapo kesho.Nitaendelea kuwaletea kila kinachojiri