Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

Sasa hivi utaitwa mchochezi,hili Neno inabidi tupate tafsiri yake, linachanganya sana siku hizi.
Kaz bado zinaendelea




Sio kila anayekamatwa na Jeshi la Polisi ni muhalifu inaweza kuwa ni raia mwema tu ambaye ameshukiwa na polisi ambao wapo kwenye uchunguzi wao, au vinginevyo na hata ukiwa ni mhalifu pia hizi ndizo haki za Raia akiwa akikamatwa na jeshi la Polisi .

Raia ana haki ya kujulishwa kwanini anatiliwa mashaka ama kukamatwa.
Raia ana haki ya kuwajulisha ndugu, jamaa ama sehemu anakofanyia kazi kwamba ama amekamatwa na polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
Raia ana haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa kituo cha polisi ama Taasisi ya kuzuia rushwa.
Raia ana haki ya kumwomba askari ajitambulishe kwako.

Muulize jina lake
Muulize namba yake ya uaskari
Hutakiwi kutoa fedha kama dhamana uwapo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa, isipokuwa maelezo utakayoandika.
Raia ana haki ya kuwaeleza polisi ama Maafisa wa Kuzuia Rushwa kwamba lolote atakalosema linaweza kutumiwa kama ushahidi mahakamani, na asiburuzwe kuandika tu.

Raia ana haki ya kuomba Wakili wake awepo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa wakati anatoa maelezo yake.

Raia ana haki ya kusoma maelezo kabla ya kutia sahihi yake.
Raia ana haki ya kudai risiti ya orodha ya vitu vyake/fedha zake alizozitoa ama kukabidhi kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
Raia kama ni mwanamke ana haki ya kupekuliwa na polisi wa kike, na iwapo hakuna polisi mwanamke, basi mwanamke yeyote na vile vile kwa mwanamume.
Raia ana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda usiozidi saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.

Iwapo askari polisi ataamua kumpekua mtuhumiwa, mtuhumiwa ana haki ya kumpekua askari polisi kabla ya kupekuliwa yeye mwenyewe
Pia, askari polisi hawana haki ya kuingia kwenye gari, nyumba au ofisi ya mtu wanayemtuhumu, kwa madhumuni ya kufanya upekuzi, pasi na kuwapo kwa (a) hati ya upekuzi ambayo hutolewa mahakamani, (b) mashahidi wanaotambulika rasmi kisheria, kama vile, mwenyekiti/mjumbe wa serikali ya mtaa au mwenyekiti wa nyumba kumi kumi (iwapo mfumo huo unatumika), au (c) jirani wa myu anayetuhumiwa
Aidha, mtuhumiwa hatakamatwa au kupekuliwa na askari polisi baada ya saa 12.30 jioni au kabla ya saa 12.30 alfajiri, kwa mujibu wa Mwendendo wa Makosa ya Jinai (Penal Code Act), isipokuwa tu, kama kutakuwa na ushahidi wa kutosha kwamba, kumpekua mtuhumiwa kabla ya saa 12.30 alfajiri au baada ya saa 12.30 jioni kunaweza kuleta madhara kwa askari polisi, mashahidi au watu wengine wowote wale
 
Sheria ni nzuri lakini kwa nchi yetu hii ya Tanzania na afrika kwa ujumla bado sheria hii haizingatiwi vyema hasa polisi.
 



Sio kila anayekamatwa na Jeshi la Polisi ni muhalifu inaweza kuwa ni raia mwema tu ambaye ameshukiwa na polisi ambao wapo kwenye uchunguzi wao, au vinginevyo na hata ukiwa ni mhalifu pia hizi ndizo haki za Raia akiwa akikamatwa na jeshi la Polisi .

Raia ana haki ya kujulishwa kwanini anatiliwa mashaka ama kukamatwa.
Raia ana haki ya kuwajulisha ndugu, jamaa ama sehemu anakofanyia kazi kwamba ama amekamatwa na polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
Raia ana haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa kituo cha polisi ama Taasisi ya kuzuia rushwa.
Raia ana haki ya kumwomba askari ajitambulishe kwako.

Muulize jina lake
Muulize namba yake ya uaskari
Hutakiwi kutoa fedha kama dhamana uwapo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa, isipokuwa maelezo utakayoandika.
Raia ana haki ya kuwaeleza polisi ama Maafisa wa Kuzuia Rushwa kwamba lolote atakalosema linaweza kutumiwa kama ushahidi mahakamani, na asiburuzwe kuandika tu.

Raia ana haki ya kuomba Wakili wake awepo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa wakati anatoa maelezo yake.

Raia ana haki ya kusoma maelezo kabla ya kutia sahihi yake.
Raia ana haki ya kudai risiti ya orodha ya vitu vyake/fedha zake alizozitoa ama kukabidhi kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
Raia kama ni mwanamke ana haki ya kupekuliwa na polisi wa kike, na iwapo hakuna polisi mwanamke, basi mwanamke yeyote na vile vile kwa mwanamume.
Raia ana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda usiozidi saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.

Iwapo askari polisi ataamua kumpekua mtuhumiwa, mtuhumiwa ana haki ya kumpekua askari polisi kabla ya kupekuliwa yeye mwenyewe
Pia, askari polisi hawana haki ya kuingia kwenye gari, nyumba au ofisi ya mtu wanayemtuhumu, kwa madhumuni ya kufanya upekuzi, pasi na kuwapo kwa (a) hati ya upekuzi ambayo hutolewa mahakamani, (b) mashahidi wanaotambulika rasmi kisheria, kama vile, mwenyekiti/mjumbe wa serikali ya mtaa au mwenyekiti wa nyumba kumi kumi (iwapo mfumo huo unatumika), au (c) jirani wa myu anayetuhumiwa
Aidha, mtuhumiwa hatakamatwa au kupekuliwa na askari polisi baada ya saa 12.30 jioni au kabla ya saa 12.30 alfajiri, kwa mujibu wa Mwendendo wa Makosa ya Jinai (Penal Code Act), isipokuwa tu, kama kutakuwa na ushahidi wa kutosha kwamba, kumpekua mtuhumiwa kabla ya saa 12.30 alfajiri au baada ya saa 12.30 jioni kunaweza kuleta madhara kwa askari polisi, mashahidi au watu wengine wowote wale
Nihayo tu
 
mtu anakamatwa kwa kushiriki kwenye maandamano eti kwa mtandao? askar yule anamhenyesha mbele ya kamera tarehe 26/4/ utakuwa wapi? ghhhhhhhhh. polisi hawa wa ccm hovyo kabisa
 
Embu siku ukipekuliwa na polisi kataa halafu mwambie mpaka umpekue wewe,halafu ulete mrejesho!!
 
  • Raia ana haki ya kumwomba askari ajitambulishe kwako.
    • Mwulize jina lake
    • Mwulize namba yake ya uaskari
  • Raia ana haki ya kujulishwa kwanini anatiliwa mashaka ama kukamatwa.
  • Raia ana haki ya kuwajulisha ndugu, jamaa ama sehemu anakofanyia kazi kwamba ama amekamatwa na polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
  • Raia ana haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa kituo cha polisi ama Taasisi ya kuzuia rushwa.
    • Hutakiwi kutoa fedha kama dhamana uwapo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa, isipokuwa maelezo utakayoandika.
  • Raia ana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda usiozidi saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.
-----safi mkuu


Nyongeza kutoka kwa MwanaHaki
  • Iwapo askari polisi ataamua kumpekua mtuhumiwa, mtuhumiwa ana haki ya kumpekua askari polisi KABLA ya kupekuliwa yeye mwenyewe
  • Pia, askari polisi hawana haki ya kuingia kwenye gari, nyumba au ofisi ya mtu wanayemtuhumu, kwa madhumuni ya kufanya upekuzi, pasi na kuwapo kwa (a) hati ya upekuzi ambayo hutolewa mahakamani, (b) mashahidi wanaotambulika rasmi kisheria, kama vile, mwenyekiti/mjumbe wa serikali ya mtaa au mwenyekiti wa nyumba kumi kumi (iwapo mfumo huo unatumika), au (c) jirani wa myu anayetuhumiwa
  • Aidha, mtuhumiwa hatakamatwa au kupekuliwa na askari polisi baada ya saa 12.30 jioni au kabla ya saa 12.30 alfajiri, kwa mujibu wa Mwendendo wa Makosa ya Jinai (Penal Code Act), isipokuwa tu, kama kutakuwa na ushahidi wa kutosha kwamba, kumpekua mtuhumiwa kabla ya saa 12.30 alfajiri au baada ya saa 12.30 jioni kunaweza kuleta madhara kwa askari polisi, mashahidi au watu wengine wowote wale
Nikikumbuka mengine nitawapa mkanda.

./Mwana wa Haki

Zaidi soma=>Sheria :Zitambue haki zako unapokamatwa na Polisi

Zifahamu sheria pale unapokamatwa na polisi
 
1. Je , ni hatua gani za kuchukua iwapo askari amevunja kati ya izo haki zangu?

Ingekuwa vizurii atakaye jibu aonyeshe na taratibu za kufuata.

2. Naombeni mtu atume mfano wa Search warranty kwa maana watu wengi tunatapeliwaa?

Msinicheke kwa sababu tokea nimezaliwa sikijui kituo cha polisii..


3. Je, izo haki zinapatikana seheme gani katika katiba kwa sababu Wengine hatujui / hatujawahi kuisoma hata katiba?

Kama ipo imbara , kifungu ,sijui sehemu mtuambiee
 
Habari za asubuhi wanajamvi wenzangu, kupitia mtandao wa whatsapp kyna ujumbe unasambaa, ujumbe huu unaelezea iwaje endapo utakamatwa na askari, yaani unaelezea haki zako pindi askari akija kukukamata.
Mimi si mjuzi wa hizi sheria za kipolisi , nimeona ni vyema ni share na wanajamvi wenzangu kwa elimu zaidi kwa kuwa naamini hapa jf ni kisima cha maarifa.
Karibuni wajuzi.
 
Habari za asubuhi wanajamvi wenzangu, kupitia mtandao wa whatsapp kyna ujumbe unasambaa, ujumbe huu unaelezea iwaje endapo utakamatwa na askari, yaani unaelezea haki zako pindi askari akija kukukamata.
Mimi si mjuzi wa hizi sheria za kipolisi , nimeona ni vyema ni share na wanajamvi wenzangu kwa elimu zaidi kwa kuwa naamini hapa jf ni kisima cha maarifa.
Karibuni wajuzi.


Ingekuwa jambo jema uuweke hapa kwa faida ya sisi ambao hatujauona huko whatsapp
 
Habari za asubuhi wanajamvi wenzangu, kupitia mtandao wa whatsapp kyna ujumbe unasambaa, ujumbe huu unaelezea iwaje endapo utakamatwa na askari, yaani unaelezea haki zako pindi askari akija kukukamata.
Mimi si mjuzi wa hizi sheria za kipolisi , nimeona ni vyema ni share na wanajamvi wenzangu kwa elimu zaidi kwa kuwa naamini hapa jf ni kisima cha maarifa.
Karibuni wajuzi.
Griti Sinka katika ubora wako.
 
107 Reactions
Reply
Back
Top Bottom