Membensamba
Senior Member
- Nov 4, 2010
- 157
- 10
Dr. Slaa na chama chake cha CHADEMA wamezindua zama mpya katika ulingo wa siasa Tz. Ni zama za siasa za mabadiliko. Mabadiliko ya kifalsafa, na kisera yanayotoa mtazamo mpya na dira mpya kwa taifa.
Kawaida ya mabadiliko huitaji viongozi ambao ni "charismatic" au "transformational" kuyaongoza. Viongozi hawa huwa na mvuto unaosababisha mkondo wenye nguvu wa wafuasi wasioweza kupingwa katika azma yao, kama vile mkondo wa mafuriko ya maji usivyoweza kupingwa au kuzuiwa. Kwa kawaida mkondo huu huvunja kila kizuizi na kupita kuelekea kwenye shabaha yake. Viongozi "charismatic" na "transformational" kama Martin Luther King, Nelson Mandela nk ni mifano mizuri. Hawakukatishwa tamaa na kufungwa, kubezwa, wala chochote. Na ingawa wengine wao walikufa kabla ya kuyaona matunda ya juhudi zao, wamebaki kuwa mashujaa wakuu wa mabadiliko duniani.
Namtia moyo Dr. Slaa na wote wanamapinduzi, mshike uzi ule ule, hata baada ya uchaguzi mpaka ufisadi uwe historia nchini Tz. Nanyi wana JF, nawaalika kuchangia hoja za kujenga na kuchochea mabadiliko nchini. Hebu tusahau kidogo maumivu tuliyoyapata kwenye uchaguzi. Sasa tuambiane, CHADEMA IFANYE NINI ILI 2015 TUANDIKE HISTORIA? LETE HOJA.
Kawaida ya mabadiliko huitaji viongozi ambao ni "charismatic" au "transformational" kuyaongoza. Viongozi hawa huwa na mvuto unaosababisha mkondo wenye nguvu wa wafuasi wasioweza kupingwa katika azma yao, kama vile mkondo wa mafuriko ya maji usivyoweza kupingwa au kuzuiwa. Kwa kawaida mkondo huu huvunja kila kizuizi na kupita kuelekea kwenye shabaha yake. Viongozi "charismatic" na "transformational" kama Martin Luther King, Nelson Mandela nk ni mifano mizuri. Hawakukatishwa tamaa na kufungwa, kubezwa, wala chochote. Na ingawa wengine wao walikufa kabla ya kuyaona matunda ya juhudi zao, wamebaki kuwa mashujaa wakuu wa mabadiliko duniani.
Namtia moyo Dr. Slaa na wote wanamapinduzi, mshike uzi ule ule, hata baada ya uchaguzi mpaka ufisadi uwe historia nchini Tz. Nanyi wana JF, nawaalika kuchangia hoja za kujenga na kuchochea mabadiliko nchini. Hebu tusahau kidogo maumivu tuliyoyapata kwenye uchaguzi. Sasa tuambiane, CHADEMA IFANYE NINI ILI 2015 TUANDIKE HISTORIA? LETE HOJA.