Joto la Mwili

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Na. M. M. Mwanakijiji

Sijui kama niite hii ni laana au baraka, mkosi au bahati. Lakini kwa vyoyote vile ilivyokuwa ilikuwa ni kheri na shari kwa wakati mmoja. Tangu utoto nilijua ya kuwa mwenyezi Mungu amenijalia uzuri wa sura, umbo, na tabia. Nilitokea kupendwa na kila mtu mtaani kiasi cha kudekezwa nikadekeka. Na nilipoanza kukomaa macho ya watu yalikuwa yakinifuata kila ninakopita, nilizoea kupata vizawadi vya bure bure, na watoto wenzangu wengi walipenda niwe rafiki yao. Zaidi ya yote nilikuwa nimejaliwa akili ya darasani pia.

Wazazi wangu walijua hilo pia na kabla sijavunja ungo, mama na baba walinikalisha chini wakaniasa waziwazi kabisa. Waliniambia kuwa nisitiwe wingu la kujidanganya kuwa wote wanaonichekea ni rafiki zangu. Waliniambia niutumie uzuri wangu vizuri kwani ni neema ya Mungu tu. Niliwasikiliza wazazi wangu na kamwe hata mara moja sikuwahi kutumia vipaji vyangu vibaya. Majaribu yalinizunguka kila nilikokwenda. Nilipokuwa Loleza majaribu yalikuwa ni kama mvua. Mmoja wa maofisa wakuu wa Polisi pale Mbeya alikuwa ananiwinda utadhani simba anavyomnyatia swala. Hata hivyo nilimtolea nje, kwa tabasamu. Alinitumia zawadi za kila aina lakini zote nilizikataa. Walionufaika walikuwa ni marafiki zangu kwani wao walijifanya wanauwezo wa kumuunganishia kwangu.

Lakini yote hayo tisa, kumi ni hili lililonikuta wiki chache kabla ya Pasaka. Nilikuwa ninatoka nyumbani Mbagala (karibu na ukumbi wa misheni), barabara ya kwenda Kilwa nikielekea zangu mjini ndani ya gari langu jipya kabisa la Toyota RAV4 rangi ya kibluu (zawadi ya mume wangu). Nilikuwa nimevalia miwani yangu ya jua, na Tsheti ndefu, na sketi ndefu ya mauaua. Ilikuwa ni safari ya haraka haraka tu kwenda kufanya manunuzi sokoni. Nikiwa sina hili wala lile mara tu baada ya kupita eneo la Mtoni kwa Azizi Ali niliona gari jingine la Toyota Prado likiwa pembeni yangu. Ndani ya gari hilo kulikuwa na kijana ambaye na yeye alikuwa amevalia miwani ya jua na akiwa hana hili wala lile. Nilimwangalia kwa chabo, na sijui ni kitu gani kilichonikumba, sijui ni mashetani gani ya kichagga niliyokuwa nayo siku hiyo. Niliuma mdomo wangu wa chini na kujilaani.


Tulikuwa tumefika kwenye taa za uwanja wa Sabasaba, na lile gari la yule kijana lilikuwa bado pembeni yangu. Nilipomuangalia, nikakuta na yeye ananiangalia. Akatabasamu, moyo uliniyeyuka, nikajikuta na mimi natabasamu. Joto lilianza kunipanda. Tukawa tunaenda huku tukiangaliana na kutabasamiana utadhani watoto wadogo. Kijana alikuwa na sura nzuri, na meno yake meupe na yaliyopangaliana vizuri utadhani suke la mpunga! Niliamua kuteremsha kioo cha gari ili niweze kumuona vizuri na yeye alifanya hivyo hivyo. Nikachukua simu yangu iliyokuwa kwenye kiti cha abiria na kumnyoshea kama ishara ya kumuuliza "na wewe una simu hapo?" Na yeye akachomoa simu iliyokuwa ikining'inia kiunoni na kunionyesha.

"Nipigie namba hii basi 744-5556768" Nilimuambia, na baada ya kuirudia mara mbili basi aliingiza namba yangu kwenye simu yake. Nilipandisha kioo na sekunde chache baadaye simu yangu iliita.

"Hallo Binti mzuri" Sauti kakamavu lakini iliyojaa kila aina ya upole ilinisalimu. Ilikuwa ni sauti kama ya yule Malaika Gabrieli. Nilijihisi mwenye heri.

"Halo, kijana mtanashati" Nilimjibu kwa madaha. Katika maisha yangu yote sijawahi kufanya kitu kama hiki. Joto lilianza kunipanda tena.

"Unaitwa nani" Aliniuliza

"Nipe jina" Nilimjibu huku nikimtega.

"hahaha! Nitakuita Malkia" alinijibu huku akiendelea kucheka.

"Sawa na wewe nikuite nani?" Nilimuuliza

"Sina Jina" Alinijibu.

"Ok Sina Jina, umenipa wehu hapa" Nilimjibu ni bila haya za kichagga wala nini nilikiri udhaifu alionipa.

"Angalau wewe mwehu, miye hapa mwendawazimu!" Alinijibu. Kijana alikuwa ni fundi wa maneno.


"Unataka unifuate ninakokwenda?" Nilimuuliza wala sikujua ninakokwenda ni wapi. Safari ya sokoni nilijua imekufa kifo cha kienyeji.

"Nitakufuata, ukinitangulia" Alinijibu. Gari lake lilikuwa nyuma yangu na akaniashiria kwa taa kuwa yuko tayari kunifuata.

Badala ya kuendelea kuelekea mjini nilienda mbele kidogo na kugeuza kurudi ili niichuke barabara ya Mandela kuelekea Kurasini. Sina Jina alikuwa akinifuata kwa umbali kidogo kwa kila kona niliyokuwa nikikata. Nikaelekea kwenye eneo la Baraza la Maaskofu na mbele kidogo kuna Hoteli ya Usambara. Niliingia hotelini na kukodi chumba kwa usiku mmoja. Baada ya kupewa funguo ya chumba nilimpigia simu Sina Jina aliyekuwa ananisubiri nje na kumpa namba ya chumba. Baada ya dakika kadhaa mlango wa chumba ulibishwa. Nilipofungua karibu moyo wangu unitoke. Sina Jina alikuwa ni kijana mzuri, mkakamavu na mwenye macho mazuri kweli. Tamaa yangu ya kike ilipanda, na joto lilizidi kunipanda!

Aliufunga mlango na kusogea karibu yangu.

"Kabla hatujafanya lolote tukubaliane mambo machache" Nilianza kumwambia

"Ok" Alijibu huku akiwa amesimama karibu yangu akiniangalia utadhani anaangalia picha ya Mona Lisa

"Sitaki kujua chochote zaidi ya kujua kuwa una afya nzuri" Nilimuambia
"Nina afya nzuri" Alinijbu.

Nikiwa bado nimesimama, alisogea karibu yangu zaidi. Niliweza kuhisi pumzi yake karibu ya shingo yangu. Joto la mwili wake lilianza kunifanya nianze kutoka jasho kidogo. Pole pole utadhani fundi umeme alianza kunishika kiunoni na kunivuta karibu yake. Nilikuwa nimesimama mbele yake nikiwa nimempa mgongo. Sikukataa nilijisogeza karibu. Moyo ulianza kunidunda kwa kasi. Akanivuta karibu zaidi; sikufanya ajizi. Nilihisi uume wake uliosimama ukigusa makalio yangu. Ulikuwa mgumu utadhani gunzi la mahindi! Nilizungusha mkono wangu na kuanza kuupapasa. Mikono yake ilianza kunipapasa na kunitomasa matiti yangu. Joto liliongezeka. Nilihisi miguu yangu inaniishia nguvu. Nilizungusha mikono yangu nyuma yake na kumvuta karibu yangu huku nikizungusha zungusha kiuno changu kumsugua.

Aliiteremsha mikono yake hadi kwenye ukingo wa sketi yangu. Alianza kufungua zipu yangu iliyokuwa upande wa kulia. Kama kipande cha karatasi sketi yangu ilidondoka sakafuni. Nilikuwa nimevalia kichupi cha kamba maarufu kama "thong". Nilimgeukia. Nilianza kumsaidia kufungua mkanda wa suruali yake wakati yeye mwenye akifungua vifungo vya shati lake na kuliweka kando. Alikuwa amejaliwa mwili uliogangamaa kweli kweli. Bila ya shaka alikuwa anapenda kufanya mazoezi ya viungo. Kutokana na joto lililokuwa likiongezeka humo chumbani, mwili wake ulikuwa ukimeremeta kwa jasho liling'arisha mwili wake utadhani umepakwa mafuta ya alizeti. Alimalizia kuchojoa nguo zote. Mama yangu! Kijana hakuwa tu na umbo zuri bali pia alikuwa "amejaliwa" kinamna. Niliungalia uanaume wake uliokuwa ukinikodolea kwa ashki na tamaa kubwa. Ulikuwa ukipwita pwita utadhani chura aliyetayari kuruka. Nilikuwa kama mtoto aliyepelekwa kwenye duka la pipi! Sikujua kama nitafune, ning'ate, nilambe, nifyonze au nimung'unye! Uanaume wake ulikuwa mrefu, mnene, na ulionyoka utadhani fimbo ya kichawi! Ulikuwa kama ile fimbo aliyoiimba yule mwanamuziki wa Kimarekani 50 Cents. Kijana alikuwa na "magic stick"!

Nilipiga magoti, na kama nilipata ukichaa wa ghafla nilimuingiza mdomoni pole pole utadhani mwanamazingaombwe anayejaribu kumeza sime! Na kwa taratibu tena nilibanisha midomo yangu huku nikiuzunguza ulimi wangu na kuanza kumtoa nje tena. Nilipofika kwenye kichwa nilikichezea kwa ulimi kwenye kingo zake! Aliguna kwa raha! Mikono yake ilikuwa ikichezea nywele zangu. Mkono wangu wa kushoto nikauingiza ndani ya chupi yangu nikaanza kujichezea mwenyewe huku nikiendelea kumnyonya taratibu. Nilianza kuongeza kasi kwa kadiri ile ile nilivyokuwa nikijisisimua kwa vidole vyangu.

Nilijua yuko karibu kufika kilele. Nikaacha kumla koni. Ute mwepesi ulichuruzika kidogo toka kwenye kitundu cha uanaume wake. Nikatabasamu. Taya langu liliniuma kidogo lakini nikajisemea moyoni kuwa kazi na dawa.

Tukasogea kitandani. Nikajilaza chali. Sina Jina akaja juu yangu na kwa kweli hakuwa na papara kwani alijua anachokifanya. Akaanza kunilipa kiufundi. Kwanza alichodoa kichupi changu na kukitupa pembeni. Akapanua miguu yangu na kwa kutumia vidole vyake alianza kunichezea. Lazima nikiri, kuwa huyu alikuwa fundi. Wanaume wengine wao wanakimbilia kuchokomeza vidole tu badala ya kuchezea nje kwa nje kwanza. Kwa utaratibu alikichezea kisima na kuta zangu. Niliendelea kulowa utadhani mafuriko ya mto Ruvu! Sikuweza kuvumilia nilimsihi aniingie. Kama gwiji la mapenzi sina jina alianza kuniingia taratibu na akaanza kunikatikia. Na mimi sikumkopesha nikaanza kumjibu. Tulikuwa kama tunafuata mapigo ya ngoma ya mganda, kwani ilikuwa ni kudunda na kudunduana kwa stepu! Tulifanya mapenzi kwa takribani nusu saa na maajabu ya firauni nilifika kileleni kwanza! Na sekunde chache baadaye na yeye alinimwagia! Miili yetu ilikuwa imelowa jasho!!! Kitanda kilikuwa kimelowa jasho na vitu vingine!! Nilijihisi raha tele.

"Asante sana" Nilimwambia nikienda bafuni kuoga. Na yeye alinifuata tukaoga bila kusema lolote na kabla hatujatoka bafuni tukapeana uroda tena. Tulipoachana wala sikujua ni kitu gani kiliniingia. Kesho yake nilipata simu kutoka kwake. Sikuijibu. Kila jambo lina mwanzo na mwisho wake. Sikutaka kuendeleza mahusiano yale kwani ilikuwa ni mara moja tu! Nilibadilisha namba yangu ya simu na sikuwasiliana naye tena.


* * *

Mume wangu hakuwa na safari yoyote wiki ile ya pasaka, hivyo nilifurahi kuwa naye nyumbani. Pasaka tulienda kwenye kanisa la Kilutheri la Magomeni kwenye ibada ya tatu. Wakati ibada inaanza mwinjilisti alituambia kuwa ibada inaongozwa na Mchungaji Dr. Elibariki Swai toka Moshi. Wakati wa mahubiri ulipofika, nilijikuta ninapatwa na kizunguzungu kwani kwenye mimbari alitambulishwa si mwingine bali mtu niliyemfahamu kwa jina la "Sina Jina" Alikuwa ni mchungaji!! Pumzi ilianza kunitoka, jasho likaongezeka, na bila kufahamu nilidondoka ardhini na kupoteza fahamu. Nilipozinduka nilijikuta nimezungukwa na wazee kadhaa wa kanisa waliokuwa wakinipepea. Mume wangu alikuwa karibu yangu.


"Unajisikiaje" Mume wangu aliniuliza.

"Nafuu kidogo" Nilimjibu kwa sauti dhaifu. Sikumuona mchungaji na ibada ilikuwa bado inaendelea kanisani. Baada ya kupewa glasi ya maji niliweza kusimama mwenyewe na mume wangu akanisaidia kuingia kwenye gari letu la Toyota RAV4 na kurudi nyumbani. Niliibeba siri yangu moyoni. Nilifahamu jina la "Sina Jina" bila shaka ni haki kuwaambia na mimi jina langu. Naitwa Mayasa.
 
Mwanakijiji ama kwa hakika wewe ni mtunzi mahiri na mwalimu imara wa lugha yetu adhimu ya kiswahili..

Nimeifurahia hadithi hii.
 
asa huyu mbona alienda kuosha bakuli mara tu?

asante kwa hadithi...lakini ingekuwa ndefu kidogo bana
 
duh mwanakijiji wee kiboko.......bonge la story......tamu kweli kweli
 
mmmmmmmmmh yani mwanakijiji ww!hadhithi nzuri sana,zo ni hadith but sadasada hakuna mataa bana na wala jamaa hawana mpango wwte wa kuyaweka yani ni chinja chinja tu!pia huyo mama mmmh mbn maharage ya mbeya hivyo?
 
Kaizer kasoma para ya kwanza na zile ''quotes'' basi

hahahaa...B bana...hebu niulize swali la ufahamu? unajua ndo maana watu wanafeli kwenye mitihani ya ki ivyo manake wao wanasoma hadi nukta kutahamaki muda umeisha na swali hajajibu hata moja!:D
 
mmmmmmmmmh yani mwanakijiji ww!hadhithi nzuri sana,zo ni hadith but sadasada hakuna mataa bana na wala jamaa hawana mpango wwte wa kuyaweka yani ni chinja chinja tu!pia huyo mama mmmh mbn maharage ya mbeya hivyo?

khaa.halafu eti mchagga ndo aliponimaliza.....:D

hivi kumbe inawezekana kutongozana kwa macho eeh?:rolleyes:
 
hahahaa...B bana...hebu niulize swali la ufahamu? unajua ndo maana watu wanafeli kwenye mitihani ya ki ivyo manake wao wanasoma hadi nukta kutahamaki muda umeisha na swali hajajibu hata moja!:D

hahaaa usinikumbushe mitihani ya hivo, unasoma swali kwanza afu unaenda kutafuta jibu kwenye stori

ujue nimepata mawazo labda wewe na preta wakati MMK anaandika nyie mnaisoma. alipogonga key ya mwisho na nyie mkamalizia.......dah nyie wakali
 
Vip tena shem........
Hii hadithi sijui ni true story au ya kufikirika tu! maana yake ni hatari tupu.


shemeji we acha tu..kumbe na wewe umeipenda eeh? hii ni ya kufikirika si ndo maana ni hadithi....
 
Back
Top Bottom