Wana JF.
Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari na madiwani 29 wa Chadema wameshinda kesi ya uharibifu wa mali iliyokuwa ikiwakabili muda huu mahakamani.
Hivi huwa serikali ndio inakurupuka katika kuwashtaki au hawa jamaa wanabambikiwa kesi zisizo na ushahidi ?
Mbona mara zote serikali inashindwa dhidi yao?
Kuna haja sasa waanze kuhakiki vyeti na kwa hawa waandaa mashtaka
Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha imeifuta kesi ya jinai iliyokuwa ikimkabili Mbunge wa Arumeru Mashariki,Joshua Nassari, na Madiwani 29 wa jimbo la Arumeru Mashariki. Waliofutiwa kesi wote ni wa CHADEMA.
Kesi hiyo imefutwa kufuatia Serikali kuwasilisha Hati ya Kutokuwa na Nia ya kuendelea na kuwashtaki akina Nassari. Hati hiyo imewasilishwa chini ya kifungu cha 91 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Tanzania. Nassari na wenzake walikuwa wakikabiliwa na shtaka la kuharibu mali.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.