Joshua Nassari ana wakati mgumu sana kushinda ubunge Arumeru kutokana na mila zao

Wanabodi,
Kwa mujibu wa habari kutoka kwa wakazi wa Arumeru Mashariki wanasema mgombea wa Chadema Joshua Nassari, nafasi yake ya kuchukuwa kiti cha ubunge ni ndogo sana.

Katika mila zao Wamasai na Wameru hazitofautiani sana. Wazee wa kimila wamesikitishwa sana na kitendo cha Chadema kuwaletea mtoto ili awaongoze.

Wanasema Nassari, bado mtoto analelewa na wazazi wake, hana mke hana mtoto, hatuwezi kumpima hata kwa uongozi wa familia yake, anawezaje kuongoza wazee!

Wanasema Nassari mwenyewe anajua mila na desturi zetu Wameru, haziruhusu watoto kushiriki vikao vya wazee.

Nassari anajitetea kuwa mbona wengine hawajaoa kina David Silinde, Zitto Kabwe, Joseph Mbilinyi, John Mnyika.

Wazee wakamwambia hawa wote wana mila na desturi zao, inawezekana baadhi yao hawana hata mila moja.

Hiyo haiwezi kuhalalisha sisi tuvunje mila zetu kwa kuongozwa na watoto wadogo ambao wanalelewa na baba na mama.

Hizo mila desturi za Wameru na Wamasai ndio limekuwa tatizo kubwa kwa Jossua Nassari kushinda ubunge.


Kama umri ni kigezo Nassari asingepata wingi wa kura aliopata 2010 na pia kura hazipigwi na wazee peke yao bali wanajimbo wote walioandikishwa ambao ni vijana kwa asilimia kubwa sana.......1/04/2012 itadhibitisha
 
Chadema wamekosea sana kumsimisha mtoto mdogo kwenye uchaguzi wa Arumeru Mashariki.

Kuna sehemu za kumsimamisha mgombea mwenye umri mdogo lakini sio Arumeru Mashariki.

Hawa jamaa wanaheshimu sana mila na desturi zao.
Wee ritz hebu niambie 'mtoto' anaanzia umri gani na kuishia umri gani kwa mujibu wa sheria za hii nchi?

Halafu kama kwa mila za wa Meru Nassari ni 'mtoto', waanzaje tena kusema 'hajaoa', watoto huko Meru wanatakiwa kuoa?
 
Anaongoza wazee wa kimila au wananchi wa jimbo la Arumeru?

Hunajua wakati mwingine lazima tuwe wakweli wewe kwa akili yako unaona Nassari anakubalika sana Arumeru, wakati sio kweli.

Ebu turudi nyuma kidogo Nassari alikuwa miongoni mwa wagombea wa Uenyekiti Bavicha Taifa aliambulia kura tatu tu.

Sasa usije ukashangaa nguvu ya vijana iliyotumika kumkataa Bavicha ndio ikatumika Arumeru Mashariki.
 
Mleta mada hembu angalia hii picha halafu niambie hawa watoto wanamsikiliza huyu jamaa? au wanasubiri kile kitu kinachoitwa cheka na Watoto?
Wasira.jpg
 
RITZ naomba nionyesha kwenye hiyo picha hao wazee wakimila wako wapi hapo?
 
Hivi Ubwabwa wote huu anakula mtu mmoja??
balaa hili..........watoto watakula kweli kwa mtingo huu!!!

13.jpg
 
Mleta mada hembu angalia hii picha halafu niambie hawa watoto wanamsikiliza huyu jamaa? au wanasubiri kile kitu kinachoitwa cheka na Watoto?
View attachment 49830
wasiwasi wangu mm ni hayo Matusi hawa jamaa wanayoporomosha Jukwaani ilihali kuna watoto wadogo wanasikia!
wasira, Lusinde, Mchemba na ole sendeka Tafadhali maneno yasiwe makali kwenye umati wa watoto chini ya umri wa miaka 18 kama huu(pichani).
 
Mzee Elimeleki, wa Usa River anasema "Uongozi wa mtu unapimwa kuanzia kwenye familia yake. Kama ni kiongozi wa ovyo, utaona anavyoishi na familia yake. Kama ni kiongozi mzuri, utaona familia yake inavyoishi kwa kuheshimu mila na pia kumheshimu mungu kwa kushiriki shughuli za kanisa...sasa huyu Nassari tutampima wapi jamani?
 
Wanabodi,
Kwa mujibu wa habari kutoka kwa wakazi wa Arumeru Mashariki wanasema mgombea wa Chadema Joshua Nassari, nafasi yake ya kuchukuwa kiti cha ubunge ni ndogo sana.

Katika mila zao Wamasai na Wameru hazitofautiani sana. Wazee wa kimila wamesikitishwa sana na kitendo cha Chadema kuwaletea mtoto ili awaongoze.

Wanasema Nassari, bado mtoto analelewa na wazazi wake, hana mke hana mtoto, hatuwezi kumpima hata kwa uongozi wa familia yake, anawezaje kuongoza wazee!

Wanasema Nassari mwenyewe anajua mila na desturi zetu Wameru, haziruhusu watoto kushiriki vikao vya wazee.

Nassari anajitetea kuwa mbona wengine hawajaoa kina David Silinde, Zitto Kabwe, Joseph Mbilinyi, John Mnyika.

Wazee wakamwambia hawa wote wana mila na desturi zao, inawezekana baadhi yao hawana hata mila moja.

Hiyo haiwezi kuhalalisha sisi tuvunje mila zetu kwa kuongozwa na watoto wadogo ambao wanalelewa na baba na mama.

Hizo mila desturi za Wameru na Wamasai ndio limekuwa tatizo kubwa kwa Jossua Nassari kushinda ubunge.

sawa tutamchagua SIYOI ili apate mshahara wa kulea familia maana kafiwa na babake...
 
Wanabodi,
Kwa mujibu wa habari kutoka kwa wakazi wa Arumeru Mashariki wanasema mgombea wa Chadema Joshua Nassari, nafasi yake ya kuchukuwa kiti cha ubunge ni ndogo sana.

Katika mila zao Wamasai na Wameru hazitofautiani sana. Wazee wa kimila wamesikitishwa sana na kitendo cha Chadema kuwaletea mtoto ili awaongoze.

Wanasema Nassari, bado mtoto analelewa na wazazi wake, hana mke hana mtoto, hatuwezi kumpima hata kwa uongozi wa familia yake, anawezaje kuongoza wazee!

Wanasema Nassari mwenyewe anajua mila na desturi zetu Wameru, haziruhusu watoto kushiriki vikao vya wazee.

Nassari anajitetea kuwa mbona wengine hawajaoa kina David Silinde, Zitto Kabwe, Joseph Mbilinyi, John Mnyika.

Wazee wakamwambia hawa wote wana mila na desturi zao, inawezekana baadhi yao hawana hata mila moja.

Hiyo haiwezi kuhalalisha sisi tuvunje mila zetu kwa kuongozwa na watoto wadogo ambao wanalelewa na baba na mama.

Hizo mila desturi za Wameru na Wamasai ndio limekuwa tatizo kubwa kwa Jossua Nassari kushinda ubunge.

Tofautisha uongozi wa kimila na uongzi wa kisiasa. Unajifanya ng'ombe ili nani akukamwue, hujui kwamba viongozi wengi wa kimila hawajui kusoma wala kuandika. Ile hali sifa kuu ya uongozi wa kisiasa ni lazima uwe unajua kusoma na kuandika na Nassari ana sifa hiyo kwa asilimia 100%. Na kumbusha tena Nassari hatafuti ubunge ili awaongoze wazee wakimeru kimila bali ili awaongoze wameru wote kisiasa. Full stop!!
 
Mzee Elimeleki, wa Usa River anasema "Uongozi wa mtu unapimwa kuanzia kwenye familia yake. Kama ni kiongozi wa ovyo, utaona anavyoishi na familia yake. Kama ni kiongozi mzuri, utaona familia yake inavyoishi kwa kuheshimu mila na pia kumheshimu mungu kwa kushiriki shughuli za kanisa...sasa huyu Nassari tutampima wapi jamani?
Huyo mzee naye ni gamba linamuwasha, Yusufu kipindi anachaguliwa kuwa Waziri mkuu alikuwa na familia? (ref.BIBLE)
 
jaribu kutueleza urafiki wa JK na Rais wa Botswana Ian Khama ambaye hana mke wa ki-vp kwanza kabla ya kuanza kumshambulia Nassari kwa kutokuwa na mke
 
teh teh unatakiwa uje arumeru ujionee mwenyewe alafu ndio useme, joshua anakubalika na kila rika yani kwa wazee ndo usiseme, kwa sisi tuliopo huku arumeru na hasa hapa usa river ndo tunajua ukweli jinsi sioi atakavyoanguka vibaya, we umefikiri joshua anagombea nafasi ya kimila nini!? watu wanataka mtu anayeweza kusimama na kujenga hoja kwa kujiamini, sasa huyu sio yeye haongei muda wote ni wapambe wake ndo kina wasira hawa na lusinde ambao wanaongea pumba badala ya hoja, na yeye akisimama anasema nichagueni jamani changamoto ni nyingi eti ndo ashamaliza,
sijui akienda bungeni kama ataweza hata kutetea kitu coz hata hayo maeneo ya meru hayajui mpaka watu wamwambie sema kitu fulan. karibuni sana arumeru mapambano yanaendelea tupo makumira hapa
 
teh teh unatakiwa uje arumeru ujionee mwenyewe alafu ndio useme, joshua anakubalika na kila rika yani kwa wazee ndo usiseme, kwa sisi tuliopo huku arumeru na hasa hapa usa river ndo tunajua ukweli jinsi sioi atakavyoanguka vibaya, we umefikiri joshua anagombea nafasi ya kimila nini!? watu wanataka mtu anayeweza kusimama na kujenga hoja kwa kujiamini, sasa huyu sio yeye haongei muda wote ni wapambe wake ndo kina wasira hawa na lusinde ambao wanaongea pumba badala ya hoja, na yeye akisimama anasema nichagueni jamani changamoto ni nyingi eti ndo ashamaliza,
sijui akienda bungeni kama ataweza hata kutetea kitu coz hata hayo maeneo ya meru hayajui mpaka watu wamwambie sema kitu fulan. karibuni sana arumeru mapambano yanaendelea tupo makumira hapa

Mkuu, hayo ni maneno yako ambayo umeamua kujiliwaza tu Nassari, angekuwa anakubalika asingepata kura 3 kwenye uchaguzi wa Bavicha.
 
jaribu kutueleza urafiki wa JK na Rais wa Botswana Ian Khama ambaye hana mke wa ki-vp kwanza kabla ya kuanza kumshambulia Nassari kwa kutokuwa na mke

Geza Ulole,
Nadhani nyie Chadema ndio mgetueleza kwa nini viongozi wenu pamoja na wabunge wenu hawajaolea wala kuoa kama utapenda takutajia.
 
Back
Top Bottom