Josephat Manyerere kuwa Meya wa jiji la Mwanza

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
CDM-Jiji la Mwanza kimemteua Diwani wa Nyakato, Josephat Manyerere, kuwa mgombea wa umeya wa jiji hilo, huku nafasi ya unaibu ikichukuliwa na Charles Machinchibera wa Mahina.

Chama hicho pia kimefanikiwa kupata madiwani wanne zaidi wa viti maalumu na kufikisha madiwani 15 wakati huo CCM ikiambulia madiwani watatu wa viti maalumu na kufikisha idadi ya madiwani 12.

Akizungumzia mchakato wa uundaji wa Jiji la Mwanza, Dk. Slaa alitoa angalizo kuwa ni lazima wananchi watumikiwe kwa masilahi ya umma na si mtu binafsi.

Hongera Dr. Slaa kwa kukamilisha uteuzi kwa amani tunakuomba usichoke elekea Musoma ukaweke mambo sawa huko nasikia madiwani wawili wa CUF wanakiunga CDM mkono.
 
Asante mkuu kutupa habari njema

aluta continue.....
Kufuatia ujumbe wa bongo tz ndani ya jf-watanzania tunatoa wito kutenda yafuatayo

1. Tuendelee kuamsha umma wa watanzania madai ya katiba mpya na tume huru chini ya uongozi wa umma wa dr slaa nje ya bunge na mpiganaji mbowe ndani ya bunge.

2. Kama anavyofanya mh thomas nyimbo kufungua matawi jimbo lake lote vivyo hivyo chadema jimbo la kinondoni tumeanza rasmi kazi hiyo, tunawataka vijana kuanza kazi hii nchi nzima ili wakati tunasubiri marekebisho ya katiba na tume huru, tuwe tumepanga safu kuanzia ngazi ya shina nchi nzima

3. Kufungua matawi kutatufanya kushika hatamu kwenye chaguzi za serikali za mitaa ili kumkomboa mtanzania

4. Chadema makao makuu opresheni sangara sasa mikoa yote tanzania chini ya wasomi prof baregu, na kiongozi wa umma dr slaa

5. Tusamabaze katiba ya chadema inayolenga katika nguvu ya umma kufikia mabadiliko ya kweli.

6. Wabunge wetu wote wakabidhiwe mikoa ya kusimamia shuguli za chama kimkakati ili kupanga safu za kisomi na kiufundi kila ngazi ya uongozi

haya yote tunayaweza na yatatufanya kuweka historia tanzania kama ilivyotokea sasa
 
Ongera CDM, penye nia pana njia!
Ninakubali kazi iliyofanyika na inayoendelea kufanyika ili kumkomboa mtanzania. "Mungu ibariki Tanzania"!
 
Jana Dr. Slaa alikua Musoma, alikua na kikao na madiwani na mbunge Nyerere. Nadhani keshapanga safu vizuri tayari kwa mashambulizi

Source: Star TV habari ya saa 2 usiku
 
CDM-Jiji la Mwanza kimemteua Diwani wa Nyakato, Josephat Manyerere, kuwa mgombea wa umeya wa jiji hilo, huku nafasi ya unaibu ikichukuliwa na Charles Machinchibera wa Mahina.

Chama hicho pia kimefanikiwa kupata madiwani wanne zaidi wa viti maalumu na kufikisha madiwani 15 wakati huo CCM ikiambulia madiwani watatu wa viti maalumu na kufikisha idadi ya madiwani 12.

Akizungumzia mchakato wa uundaji wa Jiji la Mwanza, Dk. Slaa alitoa angalizo kuwa ni lazima wananchi watumikiwe kwa masilahi ya umma na si mtu binafsi.

Hongera Dr. Slaa kwa kukamilisha uteuzi kwa amani tunakuomba usichoke elekea Musoma ukaweke mambo sawa huko nasikia madiwani wawili wa CUF wanakiunga CDM mkono.

Msukuma akisema 'yaya' basi andika maumivu.

CCM watake wasitake.

Chadema lazima kiongoze halmashauri ya jiji la mwanza.

Watashangaa zaidi pale madiwani wa CCM watakapompigia kura Manyerere.
 
hakuna mwaka nafurahia uchaguzi wake kama mwaka 2010 japo kuna jitu limekwiba kura ..lakini salamu zimefika kuwa hapendwi na hawezi kuongoza ...
 
wadau nidokezeni na arusha pia nani kachukua umea? kuna tetesi kuwa CHADEMA imechukua pia
 
Hongera dr. slaaa kwa kusimamia mchakato wa kumpata meya wa jiji la mwanza na musoma,Tukishirikiana kwa pamoja tunaweza,peoplessssssssssssss powerrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
 
Huo ni Mwanzo Tu, Shinyanga nayo itakuwa ni ya chadema 2015!
Hongera sana Dr. Slaa tuko pamoja.
Peoples....POwers:peace:
 
2015 jiji la dar es salaam meya atatoka CDM..............INAWEZEKANA NA ITAWEZEKANA ..................... UMOJA NA NGUVU TU NDIO VINAVYO ITAJIKA
 
Moshi ccm ndo wasahau kabisa hata kama dr slaa asipokuja maana MADIWANI viti maalumu walioongewa cdm 6 ccm 1 jumla inakuwa viti 23 kwa 5.source nipashe ya dec 1.
 
CDM-Jiji la Mwanza kimemteua Diwani wa Nyakato, Josephat Manyerere, kuwa mgombea wa umeya wa jiji hilo, huku nafasi ya unaibu ikichukuliwa na Charles Machinchibera wa Mahina.

Chama hicho pia kimefanikiwa kupata madiwani wanne zaidi wa viti maalumu na kufikisha madiwani 15 wakati huo CCM ikiambulia madiwani watatu wa viti maalumu na kufikisha idadi ya madiwani 12.

Akizungumzia mchakato wa uundaji wa Jiji la Mwanza, Dk. Slaa alitoa angalizo kuwa ni lazima wananchi watumikiwe kwa masilahi ya umma na si mtu binafsi.

Hongera Dr. Slaa kwa kukamilisha uteuzi kwa amani tunakuomba usichoke elekea Musoma ukaweke mambo sawa huko nasikia madiwani wawili wa CUF wanakiunga CDM mkono.

Mpaka nasikia raha ya kutokea Lake zone. Halafu mtu anasema CDM ya wachaga, toka lini Machinchibera na Manyerere wakawa kina meku??? Go CDM gooooooooooooo!
 
Ina vyo elekea Arusha wataongoza kwa kupokezana CDM na CCM, maana Chadema 14 na CCM 14 ila chadema inamtegemea diwani wa TLP ili CDM wawe 15 na CCM watakuwa 14...nasikia CCM wanajaribu kupindisha sheria wanataka kuingiza kichwa kingine kwa ujanja ujanja tusubili tuone Arusha itaongozwa na CDM au CCM...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom