Joseph Warioba na Salim A. Salim wazungumza

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
54,363
58,386
Joseph Warioba na Salim A. Salim wazungumza 04/11/2010



Mawaziri wakuu wastaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jaji mstaafu, Joseph Sinde Warioba, pamoja na mwanadiplomasia wa Kimataifa, Dk. Salim Ahmed Salim, kwa nyakati tofauti wametoa maoni yao kuhusu nguvu ya vyama vya upinzani kutwaa majimbo mengi ya uchaguzi.
1062579.png
Joseph Sinde Warioba​
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa mahojiano maalumu na Shirika la Utanganzaji Tanzania (TBC) jana Warioba, alisema CCM imepoteza majimbo si kutokana na upinzani, bali ni matatizo yaliyojitokeza ndani ya Chama chenyewe.

“Nafiriki ndani ya CCM kura za maoni zilileta mgawanyiko.“

Kwa mujibu wa Warioba, hivi sasa kuna mwamko pamoja na hamasa kwa wananchi ambao sehemu nyingine wamesikiliza sera za vyama hivyo na wamedhani wakiwapa ridhaa wanaweza kufanya mabadiliko.

“Nadhani kuna mwamko… tulitokea katika historia ya chama kimoja na wananchi walielewa hicho chama, itikadi yake na sera zake na hasa vijijini walikuwa wamezoea hivyo,” alisema.

Hata hivyo mwamko wao wa kule kupata fursa ya kusikiliza hizo sera za vyama vingine, umewachukua muda mrefu kuchukua uamuzi wa kufanya mabadiliko.

“Ninaona vyama vya upinzani wanavyoongoza, kwa mfano Mwanza, mahali pazito pale, wanaingia vijana waliozalizwa miaka ya 1970 …na hata ukiona kwenye mikutano, vijana wameamka na hii ni dalili nzuri kwani vijana ndiyo nguvu ya Taifa,” alisema.

8482078.png
Salim Ahmed Salim​
Warioba alisema kuwa vijana ndiyo wanaoleta mabadiliko na kwamba ukikuta mahali mawazo ya vijana na wazee yanafanana, ujue hapo pamedumaa.

“Lazima vijana wawe na mtazamo mpya tofauti na wazee, watachukua uzoefu wao na kuanzia hapo, lazima pawe na mabadiliko,” alisisitiza Warioba.

Naye Dk. Salim, akitoa maoni yake kupitia TBC jana, alisema wakati umefika kwa CCM kujifanyia tathimini ya mambo mbalimbali.

Alisema uchaguzi umekwenda vizuri, licha ya kuwepo kwa dosari za hapa na pale ambapo hata wachunguzi wa kimataifa waliokuwepo nchini, wameridhika na ulivyofanyika kwa utulivu na amani.

Pamoja na kuzungumzia mambo mbalimbali juu ya uchaguzi huo, Dk Salim ameshauri CCM sasa ifike mahali ijitathimini na akaongeza kuwa upinzani kushinda katika baadhi ya majimbo si jambo baya.

“Tunazungumzia demokrasia, kuiimarisha demokrasia, hilo halina wasiwasi wowote …kuna mahali vijana wetu wanashinda na maeneo mengine, pengine ndugu zetu upinzani wanashinda,“ alisema Dk Salim.



from: Joseph Warioba na Salim A. Salim wazungumza -
 
Nawapongeza sana wazee wetu hawa, ndugu Salim Ahmed Salim na Joseph Sinde Warioba kwa uchambuzi wao ambao ni wa kina, objective, wa kiufasaha na mi binafsi nawapa pongezi kwa vile wanaonekana kujua na kuelewa vizuri si tu umuhimu wa demokrasia katika nchi, bali vile vile wanaonekana kutambua fika umuhimu wa mabadiliko hasa yale yanayosukumwa na watu wenyewe kwa ajili ya maendeleo na mustakabari wa taifa lao.Thanks and God grant them more wisdom and long life.
 
Nawaheshimu hawa wazee wangu wawili









" ... wao wana pesa, sisi tuna Mungu .. " (Godbless Lema, MB)
 
Wazee hawa pamoja na UOZO ulioko CCM bado wamebaki humohumo. Hawana jipya. Waoga.
 
Warioba, alisema CCM imepoteza majimbo si kutokana na upinzani, bali ni matatizo yaliyojitokeza ndani ya Chama chenyewe.

"Nafiriki ndani ya CCM kura za maoni zilileta mgawanyiko."

Wazee wetu kuweni wa kweli......CCM is a dying horse.....you do not flog a dead horse you just dig a grave and bury it..........................Ufisadi na wala siyo kura za maoni ndani ya CCM ndiyo chanzo cha wapigakura kukichukia..........mshahara wa dhuluma ni mauti yatokanayo na laana........
 
Hawa ni wanafki tu,pamoja na kuvunda,kuoza na kunuka kote kwa CCM lakini bado wamo humo humo,hawana jipya.
 
Hawa wazee ingekuwa hamu yao wangehama CCM tatizo wanaogopa hujuma za chama Tawala
 
Ni analysis nzuri..nachukia sana ccm kuwakumbatia watu kama kinana ambao wanakurupuka na sababu za ****** eti alitoka na mavi kwa sababu alikosea hakuingia na maji!!!! hizi sabau za kusingizia kura za maoni ni mufilisi na kuacha ukweli kwamba utumishi wa ccm kwa maendeleo ya nchi yetu ni wa mashaka ili sasa kutoa mwanya wa kujirekebisha.Usalama wa Taifa wanatakiwa waongeze kasi ya kuelewa hilo ili waweze kuanza kuwatumikia watanzania wote badala ya kubaki kulinda maslahi ya matajiri wachache..uchaguzi huu umefungua ukurasa mpya wa kuelekea kwenye FAIR DISTRIBUTION of national resources hivyo hakuna wa kuendelea kuzuia hilo
 
Wazee hawa pamoja na UOZO ulioko CCM bado wamebaki humohumo. Hawana jipya. Waoga.

Inamaana mkeo uliye nao kwenye ndoa ni lazima umuache na kumwoa mwingine ndio kutatua matatizo ya ndoa yako??? Tafakari kwa makini.

CCM kwa sasa inahitaji kweli tathimini makini na angalifu sasa kwani wao kuwepo kwao ndani ya CCM ndio kusema waoga? Kama kweli wewe ni mfuatiliaje mzuri wa Siasa za TZ unawaelewa hawa wazee fika ni mangapi wameshauriwa CCM na wameyapuuzi wakiongozwa na JK na mpaka kufikia kutoa maneno ya kejeli oooh wakati wenu mlishindwa iweje sasa ati mwajua kutukosoa sisi, As a President hutakiwi kuji hivyo au kwani ungenyemaza na kuto ruhusu mipasho asinge pungukiwa na kitu is just a matter of working on issue mentioned period. Wajua yawezekana kabisa hata hao viongozi wa zamani walikuwa na mapungufu lakini usifananishe na yakwao waliyo yakosea unatakiwa uyatafutie ufumbuzi na unasonga mbele kwa Rais makini ndivyo anastahili kufanya hivyo na si kupuuzia tuuuu kwa kua ana IMMUNITY !!!

Sasa kutokuwa makini kwa mambo ya kimsingi na Taifa lako na Chama chako ndiko kinaporomosha kwanza Chama chako ambacho ulitegemea kinge tawala miaka mingi na sasa tizama chafa mikononi kwao JK
 
Wazee wetu kuweni wa kweli......CCM is a dying horse.....you do not flog a dead horse you just dig a grave and bury it..........................Ufisadi na wala siyo kura za maoni ndani ya CCM ndiyo chanzo cha wapigakura kukichukia..........mshahara wa dhuluma ni mauti yatokanayo na laana........

Hazo ni Nyufa muhimu za kwanza kabisa zinazo kiua CCM

Hawana Black and White ndani yao kuna majitu yakiambiwa ni mabishi, hawajui kujenga HOJA za kuwatoa matajiri ndani ya chama na wawe wanachama wa kawaida tuu ili kulinda uadilifu na uongozi bora.

Kushindwa kurekebisha mapungufu machache yaliyomo kwenye Azimio la Arusha, ili kuleta usawa na haki kwa wananchi wote, viongozi kuwa wazalendo na kuijua miiko ya uongozi

 
Joseph Warioba na Salim A. Salim wazungumza 04/11/2010



Mawaziri wakuu wastaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jaji mstaafu, Joseph Sinde Warioba, pamoja na mwanadiplomasia wa Kimataifa, Dk. Salim Ahmed Salim, kwa nyakati tofauti wametoa maoni yao kuhusu nguvu ya vyama vya upinzani kutwaa majimbo mengi ya uchaguzi.
1062579.png
Joseph Sinde Warioba​
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa mahojiano maalumu na Shirika la Utanganzaji Tanzania (TBC) jana Warioba, alisema CCM imepoteza majimbo si kutokana na upinzani, bali ni matatizo yaliyojitokeza ndani ya Chama chenyewe.

"Nafiriki ndani ya CCM kura za maoni zilileta mgawanyiko."

Kwa mujibu wa Warioba, hivi sasa kuna mwamko pamoja na hamasa kwa wananchi ambao sehemu nyingine wamesikiliza sera za vyama hivyo na wamedhani wakiwapa ridhaa wanaweza kufanya mabadiliko.

"Nadhani kuna mwamko… tulitokea katika historia ya chama kimoja na wananchi walielewa hicho chama, itikadi yake na sera zake na hasa vijijini walikuwa wamezoea hivyo," alisema.

Hata hivyo mwamko wao wa kule kupata fursa ya kusikiliza hizo sera za vyama vingine, umewachukua muda mrefu kuchukua uamuzi wa kufanya mabadiliko.

"Ninaona vyama vya upinzani wanavyoongoza, kwa mfano Mwanza, mahali pazito pale, wanaingia vijana waliozalizwa miaka ya 1970 …na hata ukiona kwenye mikutano, vijana wameamka na hii ni dalili nzuri kwani vijana ndiyo nguvu ya Taifa," alisema.

8482078.png
Salim Ahmed Salim​
Warioba alisema kuwa vijana ndiyo wanaoleta mabadiliko na kwamba ukikuta mahali mawazo ya vijana na wazee yanafanana, ujue hapo pamedumaa.

"Lazima vijana wawe na mtazamo mpya tofauti na wazee, watachukua uzoefu wao na kuanzia hapo, lazima pawe na mabadiliko," alisisitiza Warioba.

Naye Dk. Salim, akitoa maoni yake kupitia TBC jana, alisema wakati umefika kwa CCM kujifanyia tathimini ya mambo mbalimbali.

Alisema uchaguzi umekwenda vizuri, licha ya kuwepo kwa dosari za hapa na pale ambapo hata wachunguzi wa kimataifa waliokuwepo nchini, wameridhika na ulivyofanyika kwa utulivu na amani.

Pamoja na kuzungumzia mambo mbalimbali juu ya uchaguzi huo, Dk Salim ameshauri CCM sasa ifike mahali ijitathimini na akaongeza kuwa upinzani kushinda katika baadhi ya majimbo si jambo baya.

"Tunazungumzia demokrasia, kuiimarisha demokrasia, hilo halina wasiwasi wowote …kuna mahali vijana wetu wanashinda na maeneo mengine, pengine ndugu zetu upinzani wanashinda," alisema Dk Salim.



from: Joseph Warioba na Salim A. Salim wazungumza -

Hoja ya Warioba haina nguvu; hata kama ndani ya CCM kungekuwa shwari pigo lingekuwa pale pale - mimi si mwanachama wa chama chochote na nimepiga kura. Hoja ya msingi ni nusu karne bado watoto wanamaliza shule ya msingi wakiwa na uwezo wa kusoma na kuandika kama mwanafunzi wa darasa la tatu, mzazi gani atakubali? Bora hata hoja ya Dr. Salim.
 
Hawa wazee ni moja ya viongozi wachache ambao waliweka maslahi ya taifa mbele, utendaji wao kazi ulikuwa mzuri si lazima kila kiongozi ahame chama kama hakubaliani na chama chake, kwa nafasi zao walizoshika serikalini ni vigumu sana wao kuihama CCM lakini wameongea ukweli.
 
NILIPATA NAFASI YA KUTEMBELEA SHANGHAI EXPO 2010 KATIKA PAVILION YA "AU" African Union Jina la Dr.salim Ahmed Salim ni maarufu sana , huyu mzee ametuletea heshima kubwa sana nchi yetu alipokuwa AU.. nilipowaambia natoka TZ i thought ningepewa strory za nyerere ! kwa mshangao walikuwa wakiongea na mimi kwa furaha na bashasha wakinipa sifa za huyu bwana! nikawa najiuliza hivi hawa watu hamjui nyerere ama.?
 
Joseph Warioba na Salim A. Salim wazungumza 04/11/2010



Mawaziri wakuu wastaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jaji mstaafu, Joseph Sinde Warioba, pamoja na mwanadiplomasia wa Kimataifa, Dk. Salim Ahmed Salim, kwa nyakati tofauti wametoa maoni yao kuhusu nguvu ya vyama vya upinzani kutwaa majimbo mengi ya uchaguzi.
1062579.png
Joseph Sinde Warioba​
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa mahojiano maalumu na Shirika la Utanganzaji Tanzania (TBC) jana Warioba, alisema CCM imepoteza majimbo si kutokana na upinzani, bali ni matatizo yaliyojitokeza ndani ya Chama chenyewe.

"Nafiriki ndani ya CCM kura za maoni zilileta mgawanyiko."

Kwa mujibu wa Warioba, hivi sasa kuna mwamko pamoja na hamasa kwa wananchi ambao sehemu nyingine wamesikiliza sera za vyama hivyo na wamedhani wakiwapa ridhaa wanaweza kufanya mabadiliko.

"Nadhani kuna mwamko… tulitokea katika historia ya chama kimoja na wananchi walielewa hicho chama, itikadi yake na sera zake na hasa vijijini walikuwa wamezoea hivyo," alisema.

Hata hivyo mwamko wao wa kule kupata fursa ya kusikiliza hizo sera za vyama vingine, umewachukua muda mrefu kuchukua uamuzi wa kufanya mabadiliko.

"Ninaona vyama vya upinzani wanavyoongoza, kwa mfano Mwanza, mahali pazito pale, wanaingia vijana waliozalizwa miaka ya 1970 …na hata ukiona kwenye mikutano, vijana wameamka na hii ni dalili nzuri kwani vijana ndiyo nguvu ya Taifa," alisema.

8482078.png
Salim Ahmed Salim​
Warioba alisema kuwa vijana ndiyo wanaoleta mabadiliko na kwamba ukikuta mahali mawazo ya vijana na wazee yanafanana, ujue hapo pamedumaa.

"Lazima vijana wawe na mtazamo mpya tofauti na wazee, watachukua uzoefu wao na kuanzia hapo, lazima pawe na mabadiliko," alisisitiza Warioba.

Naye Dk. Salim, akitoa maoni yake kupitia TBC jana, alisema wakati umefika kwa CCM kujifanyia tathimini ya mambo mbalimbali.

Alisema uchaguzi umekwenda vizuri, licha ya kuwepo kwa dosari za hapa na pale ambapo hata wachunguzi wa kimataifa waliokuwepo nchini, wameridhika na ulivyofanyika kwa utulivu na amani.

Pamoja na kuzungumzia mambo mbalimbali juu ya uchaguzi huo, Dk Salim ameshauri CCM sasa ifike mahali ijitathimini na akaongeza kuwa upinzani kushinda katika baadhi ya majimbo si jambo baya.

"Tunazungumzia demokrasia, kuiimarisha demokrasia, hilo halina wasiwasi wowote …kuna mahali vijana wetu wanashinda na maeneo mengine, pengine ndugu zetu upinzani wanashinda," alisema Dk Salim.



from: Joseph Warioba na Salim A. Salim wazungumza -


- Sawa sawa hapo tupo pamoja sana kama nilivyosema mapema, naona hatuko mbali sana, CCM ijiangalie maana imepigana na kivuli chake kwenye huu uchaguzi.

William.
 
Hawa wazee kuna mambo mengi mazuri walifanya, lakini kitendo chao cha kukaa kimya na kutozungumzwa chochote juu ya uchakachuaji unaonendelea kinawavunjia heshima mbele ya wananchi. Ni lazima ifike sehemu watu wajifunze kuweka maslahi ya taifa mbele, CCM sio Tanzania!
 
..hawa ni wawili ni waoga wakubwa.

..wana mtandao wa CCM wamewachafua lakini wameendelea kung'ang'ania humohumo ndani ya CCM.

..kama walishindwa kujitetea wenyewe dhidi ya siasa za maji taka za wanamtandao usitegemee wakawatetea wananchi hata siku moja.
 
Back
Top Bottom