Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,792
- 71,206
Nimesikitishwa na kauli hii kutoka kwa aliyekuwa mbunge wa Rombo. Kwamba nchi hii iko huru na hao viongozi wa upinzani wanao kamatwa na kuwekwa ndani ni wahalifu tuu kama wahalifu wengine.
Kuna kuteleza na kuanguka lakini huku sio kuteleza bali ni kujibwaga chini ili tuu kuwafurahisha watawala na kuwavunjia heshima wananchi na viongozi wenzake aliokuwa nao katika mapambano awali.
Iko wazi kuwa alikuwa muongo na mzandiki hata kwa wanarombo na kuna siku atamkana kijana wao aliyepotea Ben Saanane na kuwaambia watu wa Rombo ambao bado wana uchungu kuwa kijana alikuwa Jambazi hivyo pengine kapotelea kwenye shughuli hizo.
Selasini, umefikia hatua hiyo kweli? Mbona unakubali kuziingiza mvi zako kaburini kwa fedheha kiasi hicho?
Kuna kuteleza na kuanguka lakini huku sio kuteleza bali ni kujibwaga chini ili tuu kuwafurahisha watawala na kuwavunjia heshima wananchi na viongozi wenzake aliokuwa nao katika mapambano awali.
Iko wazi kuwa alikuwa muongo na mzandiki hata kwa wanarombo na kuna siku atamkana kijana wao aliyepotea Ben Saanane na kuwaambia watu wa Rombo ambao bado wana uchungu kuwa kijana alikuwa Jambazi hivyo pengine kapotelea kwenye shughuli hizo.
Selasini, umefikia hatua hiyo kweli? Mbona unakubali kuziingiza mvi zako kaburini kwa fedheha kiasi hicho?