Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,343
- 217,375
Taarifa kutoka Jimbo la Rombo Mkoani Kilimanjaro zinadai kwamba , Ndugu Joseph Selasini , ambaye ameshirikiana na ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa kufanya vikao haramu vya kumpindua Mwenyekiti wa halali wa NCCR MAGEUZI James Mbatia si Mwanachama wa NCCR MAGEUZI bali ni mwanachama wa Chadema , aliyeomba kurejea Chadema baada ya kukihama chama hicho wakati wa uchaguzi Mkuu wa 2020 na kujiunga na NCCR MAGEUZI na kusimikwa kuwa Mgombea ubunge wa Rombo .
Baada ya kuomba radhi na kuipiga magoti Chadema , Joseph Selasini amepewa msamaha na amekabidhiwa kadi mpya ya Chadema ( namba yake inahifadhiwa kwa sasa ) , barua ya msamaha wa Joseph selsini imezagaa mitandaoni , Tayari ndugu Selasini ameitwa na Chadema Rombo , ili kujieleza Sababu za yeye kushiriki Kuanzisha vurumai kwenye chama kingine cha siasa huku akiwa si mwanachama wa chama hicho .
Sheria za Tanzania zinaeleza kwamba uanachama wa mtu kwenye chama fulani hukoma mara moja , mara tu anapojiunga na chama kingine cha siasa na kukabidhiwa kadi ya uanachama , ndio maana hata akirudi tena kwenye chama cha awali hupewa kadi upya kabisa tena yenye namba nyingine , kwa mfano , Lowassa , Wassira na mamluki wengine waliporejea CCM walipewa kadi mpya kabisa .
Je, kwenye njama hii iliyobumbuluka hawa ofisi ya Msajili hawakufahamu chochote au hapo ndio ulipoishia uwezo wao ?
ANGALIZO : CHADEMA inapaswa kuwa Makini sana na hawa Mamluki wanaoomba kurejea tena kwenye chama chao tulishasema mara nyingi kwamba Chama ni watu , LAKINI NI LAZIMA HAO WATU WENYEWE WAWE BINADAMU .
Baada ya kuomba radhi na kuipiga magoti Chadema , Joseph Selasini amepewa msamaha na amekabidhiwa kadi mpya ya Chadema ( namba yake inahifadhiwa kwa sasa ) , barua ya msamaha wa Joseph selsini imezagaa mitandaoni , Tayari ndugu Selasini ameitwa na Chadema Rombo , ili kujieleza Sababu za yeye kushiriki Kuanzisha vurumai kwenye chama kingine cha siasa huku akiwa si mwanachama wa chama hicho .
Sheria za Tanzania zinaeleza kwamba uanachama wa mtu kwenye chama fulani hukoma mara moja , mara tu anapojiunga na chama kingine cha siasa na kukabidhiwa kadi ya uanachama , ndio maana hata akirudi tena kwenye chama cha awali hupewa kadi upya kabisa tena yenye namba nyingine , kwa mfano , Lowassa , Wassira na mamluki wengine waliporejea CCM walipewa kadi mpya kabisa .
Je, kwenye njama hii iliyobumbuluka hawa ofisi ya Msajili hawakufahamu chochote au hapo ndio ulipoishia uwezo wao ?
ANGALIZO : CHADEMA inapaswa kuwa Makini sana na hawa Mamluki wanaoomba kurejea tena kwenye chama chao tulishasema mara nyingi kwamba Chama ni watu , LAKINI NI LAZIMA HAO WATU WENYEWE WAWE BINADAMU .