Magwangala
JF-Expert Member
- Oct 4, 2011
- 2,413
- 1,534
Nilikuwepo eneo la tukio, Komando Sele hakuwa mfanyakazi wa mgodi wa Geita bali alikuwahi kufanya kazi Barick Bulyankulu lakini jambazi aliyekubuhu,si mara moja amewahi kuteka gari la mshahara (maana advance walikuwa wanachukulia dirishani) Siku ya tukio yeye na wenzake kama 8 hivi walipanga kuiba dhahabu yote kabla haijapakiwa kwenye ndege, dhahabu kutoka Gold Room husafirishwa na gari maalum ambalo ni bullet proof likilindwa na askari maalumu wa mgodi,Sele na wenzake walikuwa wametangulia air port na kujificha msituni,mara tu gari la dhahabu lilipofika tayari kupakia dhahabu ndegeni ndipo akina Sele wakaanza kurusha risasi kwa walinzi ambao walifanikiwa kuwakimbiza majambazi wote na akabaki Sele pekee, walinzi wote wa mgodi walijificha akabaki Kaburu mmoja dhidi ya Seli, ilikuwa kama muvi,kwa mara moja Sele na Kaburu walipigana risasi za mwisho, Sele alipigwa kwenye paji la uso wakati Kaburu ilimpata begani na kukimbizwa South Africa ambako alipona, huo ndio ukawa mwisho wa Komando Sele aliyesumbua sehemu mbalimbali za kanda ya Ziwa, inasemekana majambazi wengine walikuwa ni WanyarwandaShukran ndugu japo kwa ufupi umenifungua kidogo kuhusu tukio hilo