Jokate: Wilaya ya Temeke yatengewa zaidi ya Tsh bilioni 4 za kutekeleza miradi ya maendeleo

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Jan 5, 2013
658
821
WILAYA YA TEMEKE YATENGEWA ZAIDI YA TSH BILIONI 4 KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO,SHUKRANI KWA RAIS SAMIA - DC TMK MHE.JOKATE MWEGELO

Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe.Jokate Mwegelo kwa niaba ya Uongozi wa Wilaya ya Temeke ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuwapatia fedha Tsh Bilioni 4.491,851,456.06 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Mhe Jokate ameeleza namna ambavyo fedha hizo zimetengwa katika matumizi mbalimbali ya kuleta Maendeleo ambapo Takribani Tsh B 3.14 zitatumika katika ujenzi wa vyumba vya madarasa mapya 157 kwa shule za sekondari,Tsh M 250 kutumika katika ujenzi wa kituo cha afya Tuangoma,Tsh M 300 kutumika katika ujenzi wa Jengo la Huduma za dharura (EMD),Tsh M 700 kutumika katika ujenzi wa bweni la shule ya sekondari Kibasila pamoja na Tsh M 101,851,456.06 kutumika katika kampeni ya chanjo ya UVIKO-19 ikiwa ni ngao madhubuti dhidi ya uginjwa wa corona.

Aidha Mhe.Jokate ametoa shukrani kwa Rais Samia kwa kuwapatia magari 2 mapya kwa ajili ya kubebea wagonjwa (Ambulance) na usimamizi wa huduma za afya.

"Natoa shukrani kwa Mhe.Rais Samia kwakweli ni ukweli usiopingika Mwanamama huyu alishika nchi kipindi kigumu lakini ameonesha ukakamavu wa akina mama na ameweza kutuvusha salama na amefanya maamuzi mengi mengine magumu lakini ni kwaajili ya Taifa letu la Tanzania" Alisema Mhe.Jokate.

Mhe.Jokate ameyasema hayo leo Oktoba 13,2021 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Iddi Nyundo wakati akitambulisha rasmi ujio wa kampeni ya TEMEKE GULIO yenye lengo la kuwainua wafanyabiashara wadogo (wamachinga).

#KaziIendelee

IMG_20211013_210152_887.jpg
 
Mitanzania ni mimutu ya hovyo sana..eti pesa za samia huyo ana hela gani ya kutoa..kama sio hela za walipa kodi..hiyo mikopo nayochukua anazidi kuwanenesha mizgo wa deni la taifa wananchi..wakiahindwa kulipa mabeberu yaanze kuzigawana raslmasli..hana uchungu na tanganyika.

#MaendeleoHayanaChama
 
NAPINGA: Ujinga wa kutuambia Samia ametoa pesa...

Samia, or anyone for that matter, HANA pesa ya kuendeshea serikali! Kwani mkisema "serikali imetoa...."kuna tatizo gani?

NAUNGA MKONO: Suala la kushughulikia ujenzi wa madarasa mapema.

CCM wanakera sana... unakuta ikifika January, full matamko ya ujenzi wa madarasa na hapo ndipo akina JPM walipokuwa wanasifiwa eti "katoa wiki moja madarasa yawe yamejengwa"

Ukiuliza ina maana serikali ilikuwa haijui kwamba nchi ina upungufu wa madarasa, MATAGA utawasikia "huo upungufu ni kwa sababu kuna watoto wanaanza darasa la kwanza na wengine wanaingia Form I"!

Yaani wanavyoongea utasema serikali huwa haifahamu Tanzania kuna madarasa mangapi nchi nzima, na watoto wa wangapi wanarajia kujiunga Darasa I na Form IV ili hatimae wafanye maandalizi mapema!!

Ila ajabu ya Utawala wa CCM, usishangae tunaingia January, bado same old story ya uhaba wa madarasa ikawa inaendelea!!
 
WILAYA YA TEMEKE YATENGEWA ZAIDI YA TSH BILIONI 4 KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO,SHUKRANI KWA RAIS SAMIA - DC TMK MHE.JOKATE MWEGELO Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe.Jokate Mwegelo kwa niaba ya Uongozi wa Wilaya ya Temeke ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuwapatia fedha Tsh Bilioni 4.491,851,456.06 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo. Mhe Jokate ameeleza namna ambavyo fedha hizo zimetengwa katika matumizi mbalimbali ya kuleta Maendeleo ambapo Takribani Tsh B 3.14 zitatumika katika ujenzi wa vyumba vya madarasa mapya 157 kwa shule za sekondari,Tsh M 250 kutumika katika ujenzi wa kituo cha afya Tuangoma,Tsh M 300 kutumika katika ujenzi wa Jengo la Huduma za dharura (EMD),Tsh M 700 kutumika katika ujenzi wa bweni la shule ya sekondari Kibasila pamoja na Tsh M 101,851,456.06 kutumika katika kampeni ya chanjo ya UVIKO-19 ikiwa ni ngao madhubuti dhidi ya uginjwa wa corona. Aidha Mhe.Jokate ametoa shukrani kwa Rais Samia kwa kuwapatia magari 2 mapya kwa ajili ya kubebea wagonjwa (Ambulance) na usimamizi wa huduma za afya. "Natoa shukrani kwa Mhe.Rais Samia kwakweli ni ukweli usiopingika Mwanamama huyu alishika nchi kipindi kigumu lakini ameonesha ukakamavu wa akina mama na ameweza kutuvusha salama na amefanya maamuzi mengi mengine magumu lakini ni kwaajili ya Taifa letu la Tanzania" Alisema Mhe.Jokate. Mhe.Jokate ameyasema hayo leo Oktoba 13,2021 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Iddi Nyundo wakati akitambulisha rasmi ujio wa kampeni ya TEMEKE GULIO yenye lengo la kuwainua wafanyabiashara wadogo (wamachinga). #KaziIendelee View attachment 1973604






Safi Sana Rais Samia, Jokate endelea kuchpa kazi
 
Hii hata Civic form 2 inakushinda.Fedha za mkopo IMF ambayo mimi na wewe na watoto & Wajukuu watalipa eti Samia katoa.

Ebu punguza ujinga
Mjinga huamini kua kila mtu ni mjinga kama yeye,haya endelea kufuga huo ujinga wako ili siku moja uje uvune unachokifuga.
 
Mitanzania ni mimutu ya hovyo sana..eti pesa za samia huyo ana hela gani ya kutoa..kama sio hela za walipa kodi..hiyo mikopo nayochukua anazidi kuwanenesha mizgo wa deni la taifa wananchi..wakiahindwa kulipa mabeberu yaanze kuzigawana raslmasli..hana uchungu na tanganyika.

#MaendeleoHayanaChama
Tuambie wewe ungekuwa rais ungefanya nini kupunguza matatizo ya watanzania ndani ya wakati bila kukopa hizo pesa?
 
NAPINGA: Ujinga wa kutuambia Samia ametoa pesa...

Samia, or anyone for that matter, HANA pesa ya kuendeshea serikali! Kwani mkisema "serikali imetoa...."kuna tatizo gani?

NAUNGA MKONO: Suala la kushughulikia ujenzi wa madarasa mapema.

CCM wanakera sana... unakuta ikifika January, full matamko ya ujenzi wa madarasa na hapo ndipo akina JPM walipokuwa wanasifiwa eti "katoa wiki moja madarasa yawe yamejengwa"

Ukiuliza ina maana serikali ilikuwa haijui kwamba nchi ina upungufu wa madarasa, MATAGA utawasikia "huo upungufu ni kwa sababu kuna watoto wanaanza darasa la kwanza na wengine wanaingia Form I"!

Yaani wanavyoongea utasema serikali huwa haifahamu Tanzania kuna madarasa mangapi nchi nzima, na watoto wa wangapi wanarajia kujiunga Darasa I na Form IV ili hatimae wafanye maandalizi mapema!!

Ila ajabu ya Utawala wa CCM, usishangae tunaingia January, bado same old story ya uhaba wa madarasa ikawa inaendelea!!
Kama mlipinga na mnapinga hata samia kuwa raisi, mtaachaje kupinga kutajwa jina lake?!! Endeleeni.......
 
Here goes another choir member from our very own praise and worship team ☺️☺️
 
Iyo miliyoni 100 kwa ajili ya kampenj za korona ndio kifuta jasho chake hapo.

Sahivi zile pesa za magufuli zilizokua zinajenga hadi vibanda vya mahindi zimeisha ahahah nchi ya maigizo sana.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom