Mondoros
JF-Expert Member
- Aug 29, 2015
- 629
- 472
Jokate Mwegelo
Jana,22/12/2016 katika uchaguzi wa CHADEMA kanda ya Nyasa umenifanya niyakumbuke maneno ya mwanamitindo na Mjasiriamali Nguli Afrika, Jokate Mwegelo alipoulizwa na moja ya vyombo vya habari kuwa anakipenda chama gani cha siasa nchini, Naye akajibu bila woga kuwa anakipenda Chama cha Mapinduzi kwasababu HAKINA MWENYEWE. Wakati anayasema hayo kipindi kile sikumwelewa ila Uchaguzi wa Chadema kanda ya Nyasa uliofanyika Jana ndo ulinipa akili za ziada ya kumwelewa Jokate.
Kwanza nianze kwa kumpa pole za dhati kabisa Makamu wangu Mwenyekiti wa bavicha, bw Patrick Ole Sisopi kwa kufanyiwa ukatili ule na Mwenyekiti Mbowe dakika chache kabla ya kupiga kura.Ingawa mimi hili halikunishangaza kutokana na uhodari wa Mbowe wa kubadilisha Gia angani kwa kubadili(binafsi) maamuzi ya Halmashauri kuu ya chama chetu;
· Ikumbukwe Agosti,2015 Mbowe alibadili maamuzi ya Halmashauri kuu ya chama ya februari na juni ya kumpitisha Dr. wilbrod Slaa kuwa mgombea wa Chama chetu pia Mbowe alifuta taratibu za uchaguzi wa ndani wa kumpata mgombea urais wa CHADEMA, Mbowe alituleta Lowassa toka CCM akasema tu kuwa kabadili gia angani.
Mwenyekiti Mbowe
· Mwaka 2013, Mbowe alibadili katiba ya Chama chetu na kuweka kifungu cha mwanachama kutokwenda kutafuta haki Mahakamani kwa maamuzi yoyote yale ya Vikao vya chama.
· Mwaka 2013, Mbowe alimtimua ZItto uanachama kwasababu alijipanga kugombea uenyekiti ndani ya Chama chetu, alitimua pia watu wote waliokuwa wanamuunga mkono Zito kuchuana na Mbowe kwenye uenyekiti
· Mwaka 2009, Mbowe alitumia baraza la wazee kumuengua Zitto katika kinyang’anyiro cha uenyekiti wa chama chetu,,akabaki peke yake
· Mwaka 2008, Mbowe alisimamishwa uongozi(Umakam mwenyekiti Bara) Chacha Wangwe, huku uanachama wake ukisubir kujadiliwa. Baada ya Marehem Chacha Wangwe Kuitisha Vyombo vya habari ili kutolea ufafanuzi wa hoja alizoziita za kizushi za usimamishwaji wa uongozi wake na kujadiliwa kwa uanachama wake pia aliahidi kuendelea kudai haki yake mpaka kieleweke ndani ya chama pamoja na kuhakikisha chama chetu kinasimama imara, NADHANI KILA MTU ANAJUA KILICHOMPATA CHACHA WANGWE. Ikimbukwe Marehemu Chacha Wangwe alitangaza kugombea Uenyekiti wa Chadema Taifa katika uchaguzi wa mwaka 2009.
Patrick Ole Sisopi
· Ikumbukwe pia mwaka 2004, Mbowe alikabidhiwa Chama na Marehemu Bob Makani ambaye aliyemuoa dada yake wa Muasisi wa Chama chetu ambaye pia ni Mkwe wa Mwenyekiti wetu wa sasa, Mbowe. Kabla ya Makani Chama chetu kiliongozwa na Edwin Mtei
Kwahiyo alichokifanya Jana Mbowe kwa kumuondoa Patrick Ole halikuwa jambo geni kufanywa na Mbowe.
Binafsi namuomba Mbowe kama anapinia Demokrasia nchini basi tuione anaitekeleza ndani ya chama chetu. Haipendezi ccm wajibu hoja zetu nzito za kudai demokrasia kwa ule msemo maarufu wa ‘Nyani haoni kundule’
Said Amiri Said- Mwanachana Chadema