John Shibuda na mgogoro wa Kauli ya kuisifia CCM; Kauli za wana CHADEMA

MBUNGE wa Maswa Mashariki (Chadema), John Shibuda jana alirudia kauli yake ya kumuomba Rais Jakaya Kikwete awe meneja wake wa kampeni wakati atakapojitosa kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.Shibuda alifanya hivyo mbele ya wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Spika wa Bunge, Anne Makinda na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta.


Kauli hiyo imekuja wakati Shibuda akiwa ameiligawa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) baada ya mwenyekiti wake, John Heche kupingana hadharani na makamu wake, Juliana Shonza kuhusu msimamo wa baraza hilo dhidi ya hatua ya mbunge huyo kutangaza nia ya kuwania urais, akiwa ndani ya kikao cha Nec ya CCM.

Siku mbili baadaye Shibuda aliibuka tena na kumshukia Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, kuwa ndiye anayewatumia vijana hao kumhujumu, kauli ambayo ilipingwa vikali na Dk Slaa.

Lakini, jana akiwa katika semina ya wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki iliyowahusisha pia wenyeviti wa kamati zote za kudumu za Bunge wakiwemo wa Kamati ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama, Shibuda alirudia kauli yake na kuwafanya washiriki wa semina hiyo kuangua kicheko.

“Mimi naitwa John Shibuda ni Mbunge wa Maswa Mashariki na Mjumbe wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, pia ninayetaka Rais Kikwete awe kampeni meneja wangu katika kampeni za mwaka 2015,” alisema wakati akijitambulisha.

Kauli hiyo ilizua zogo kwa baadhi ya washiriki wa semina hiyo ambao walianza kumpigia makofi huku Spika Makinda na Sitta wakiangua kicheko.

hili li ndumi la kuwili sijui limetutokea wapi jamani, yani bichwa kuuuuuuubwa akili nusu kijiko, au tumfungulie page kwenye fesi buku kama ile ya diva?????
 
CDM hakiwezi kushindwa na kichwa maji kama Shibuda 7bu ni chama makini na wanajua wanachokifaya, huyo mzee anatapatapa tu kashaona kuwa hana uelekeo wa kukubalika ktk chama chochote cha kisiasa hapa tz hivyo anaamua kuwa mropokaji tu.... kupingana kwa kauli za viongozi wa BAVICHA ni swala la kawaida ktk migogoro ya kisiasa na c ishara ya chama kushindwa na Shibuda. Viva CDM
 
Nimesikitishwa na kukasirishwa sana na taarifa iliyo kwenye gazeti moja la leo juu madai ya Shibuda kwamba anasakamwa ndani ya Chadema kwa sababu yeye ni Msukuma. Kwanza sikuamini kama Shibuda (katika akili timamu) anaweza kutamka maneno ya namna hiyo. Pili siamini kama kweli maneno hayo yanaweza kutamkwa na Msukuma halisi kwa maana ya kabila, tabia, na mtazamo. Hata hivyo baada ya kutafakari kauli za nyuma za Mh. Shibuda tangu mwaka 2005 hadi alipohamia Chadema mwaka 2010, nimejiridhisha kuwa maneno yale kweli huenda yametamkwa na yeye. Pengine kitu kigumu kabisa kwangu ni kuishawishi akili yangu ikubaliane na wazo kwamba maneno hayo yanaweza kutamkwa na Msukuma akiwa hajalewa, hana kichaa (kwa kisukuma "lusalo") au ugonjwa mwingine wa akili. Nitafafanua.

Kwanza, kama inavyofahamika kwa wengi, Wasukuma ndiyo kabila kubwa kuliko yote hapa nchini. Jamii ya wasukuma imeenea sehemu kubwa ya kanda ya Ziwa hasa Mwanza, Shinyanga na Tabora. Kwa tabia na aina ya shughuli zao za kiuchumi, wasukuma wamesambaa pia katika mikoa ya Morogoro, Mbeya, Katavi, Tanga, na Pwani. Takwimu za idadi ya watu katika sensa ya mwaka 2002 zinaonesha kuwa kulikuwa na Wasukuma karibia milioni 8 kati ya watanzania milioni 36 wa wakati huo. Kwa kutambua wingi wao hapa nchini, Wasukuma wamejijengea tabia ya kujiamini na kutotishwa na uwepo au mafanikio ya kabila jingine mahali popote.

Haijawahi kutokea Msukuma halisi akalalamika juu kuingiliwa na kabila jingine au kutishiwa na mafanikio ya kabila jingine. Wasukuma ni wapole, wavumilivu, wenye busara, na hawana wivu na mafanikio ya mtu au kabila jingine. Ndiyo maana hata katika ngazi mbalimbali za uongozi, watu wa makabila mengine ni rahisi sana kukubalika na na hata kupigiwa kura kuwa viongozi katika maeneo ya wasukuma bila kujali wanakotoka. Kwa ujumla, linapokja suala la kutohisi au kujali ukabila, wasukuma wamestaarbika muda mrefu sana pengine kuliko kabila jingine lolote hapa nchini. Wengine wanaona huo ni ujinga. Sisi wasukuma tulioenda shule vizuri na kuona yanayotokea kwingine duniani tunaita huu ni ustaarabu. Hili la ustaarabu wa wasukuma hata Shibuda mwenyewe analijua, na kwa bahati mbaya nalo limekuwa likimsumbua. Ndiyo maana napata taabu kuelewa aina ya wasukuma anaowawakilisha Shibuda katika baadhi ya matamshi yake.

Pili, kwa hulka halisi ya Kisukuma (hasa wale wa Mwanza; Shibuda ni Msukuma wa Shinyanga) si rahisi kumkuta baba mzima wa kisukuma akilialia kuonewa au kubaguliwa na mtu au kabila lolote. Wasukuma ni watu wa kujiamini. Wanajiona ni wengi, wenye nguvu, mali nyingi, na kama baba wa 'vikabila' vingine vyote hapa chini (situmii neno 'vikabila" kwa maana ya kudharau makabila mengine bali ni namna tu ya msemo wa kisukuma wenye kuonesha hali ya kutotishwa: kumbuka neno 'vijisenti'?). Ukisikia mwanaume mzima wa kisukuma analalamika; iwe kumlalamikia mtu mwingine au kundi au kabila jingine ujue huyo ni msukuma aliyechanganyikiwa au kushindwa maisha (kwa kisukuma "balemelwa").

Kwa asili na historia yao, wasukuma hawajawahi kulalamika kubaguliwa mahali popote na mtu yoyote nchini. Hata inapotokea kweli wakadhulumiwa, wakanyanyaswa, au kutumiwa (kama ilivyofanya CCM kwa zaidi ya mika 50) wasukuma huvumilia huku wakijipanga. Na muda unapofika huonesha msimamo wao kwa vitendo (rejea yaliyotokea Nyamagana na Ilemela uchaguzi 2010). Ni wasukuma wachache sana (wa aina ya Shibuda) wanaoweza kudekeza vijembe na vijimaneno vya ushwahilini kwa lengo la kutafuta huruma ya watu. Tangu lini kabila kubwa lenye uwezo, mali, na historia ya kujiamini kama wasukuma likaanza kupiga kelele ya kuonewa na watu wa makabila madogo? Hicho ni kilio cha Shibuda na tumbo lake na si kilio cha wasukuma.

Mwisho, nataka Mh Shibuda aweke wazi kuwa matatizo yake na Chadema si matatizo ya wasukuma na Chadema. Kama anahisi kubaguliwa na Chadema kwa sababu ya 'aina ya usukuma wake' basi atambue pia kuwa anabaguliwa hata na wasukuma wenzake ambao sasa wamejaa ndani ya Chadema. Na mimi nataka kusisitiza kuwa kama anafanya vurugu zote hizi kwa lengo la kuitisha Chadema au kuvuta hisia za wasukuma na huruma zao ili wampe urais kwa kigezo cha ukubwa wa kabila lake basi ajue ameaumia. Wasukuma hawako tayari kuwakilishwa na mtu wa aina ya Shibuda (labda wale wa jimboni kwake tu). Kuna wasukuma wengi wasomi, waelewa, wastaarabu, na wenye hekima mara elfu kumi ya Shibuda. Kwa ujumla, karata ya ukabila haichezeki uskumani. Hata kama itatokea waaamue kuicheza, hawatakuwa tayari kuunga mkono mtu wa kuwaharirisha mbele ya makabila mengine (madogo) nchini kama Shibuda. Ndani ya wasukuma kuna majembe ya ukweli yanayoweza kugombea urais na kufanikiwa lakini si jembe butu na lililochoka kama Shibuda.

Kama Msukuma mwenzake na mwelewa wa tabia na mtazamo wa kabila langu, namwomba kaka yangu Shibuda asizidi kutuaibisha na kututengenezea taswira tusiyokuwa nayo miongoni mwa watanzania. Asitulazimishe kukubaliana na hisia zake za kipuuzi zinazotokana na msukumo wa wake wa kimaslahi na kutafuta sifa za kijinga na pengine huruma ya wapiga kura wake atakaporudi kugombea tena kwa tiketi ya chama chake halisi yaani CCM. Na kama anataka kweli kutumia karata ya ukabila kulazimisha kugombea urais kupitia Chadema basi akaanzie jimboni kwakwe alikotokea ili tuone kama kweli anaweza kuwazidi akili wasukuma wote wa huko hata kuwafanya waingiwe na hisia potofu zisizotokana na hulka halisi za Kisukuma.

Imeandikwa na Ikwalal M. Ikwalala
Wa Mwanza.

Sijui huyu jamaa huwa anaelewaga?
 
Kunatarifa za chini chini zinabainisha kuwa shibuda anaendelea kuitesa chadema kutokana na kukataa kufuata aina ya siasa wanazotaka chadema,

shibuda amekuwa na msimamo wake binafsi kisiasa kwa kukataa kutumika na chadema na kujikita kuwatumikia watu waliomchagua,

Shibuda amekuwa na mfumo wa kukataa kususia vikao vya bunge kama chadema wanavyotaka na kuendelea kuwatumikia watu waliomchagua,

shibuda pia amekuwa hakubaliani na msimamo wa viongozi wakumtaka ambatane na wenzake kwenye mandamano ya chadema kitu ambacho kinawakela sana viongozi wake,

Baada ya mijadala mirefu ndani ya chadema wengine wakitaka shibuda afukuzwe na wengine wakitaka apuuzwe lakini wapo waliodai pia kuwa shibuda anaonewa kwa sababu ya usukuma wake kama alivyowahi kusema yeye mwenyewe,

Lakini pia wapo waliowaonya chadema kuwa kama shibuda watamgusa anauwezo wa kuiua chadema kanda ya ziwa kwa mikono yake mwenyewe kwa vile yeye ndiye aliipereka kwa mikono yake mwenyewe wakimgusa moto utawaka na kamwe hawataweza kuuzima wao kama chadema ndiyo maana chadema wako kimya kwa shibuda.
 
Kunatarifa za chini chini zinabainisha kuwa shibuda anaendelea kuitesa chadema kutokana na kukataa kufuata aina ya siasa wanazotaka chadema,

shibuda amekuwa na msimamo wake binafsi kisiasa kwa kukataa kutumika na chadema na kujikita kuwatumikia watu waliomchagua,

Shibuda amekuwa na mfumo wa kukataa kususia vikao vya bunge kama chadema wanavyotaka na kuendelea kuwatumikia watu waliomchagua,

shibuda pia amekuwa hakubaliani na msimamo wa viongozi wakumtaka ambatane na wenzake kwenye mandamano ya chadema kitu ambacho kinawakela sana viongozi wake,

Baada ya mijadala mirefu ndani ya chadema wengine wakitaka shibuda afukuzwe na wengine wakitaka apuuzwe lakini wapo waliodai pia kuwa shibuda anaonewa kwa sababu ya usukuma wake kama alivyowahi kusema yeye mwenyewe,

Lakini pia wapo waliowaonya chadema kuwa kama shibuda watamgusa anauwezo wa kuiua chadema kanda ya ziwa kwa mikono yake mwenyewe kwa vile yeye ndiye aliipereka kwa mikono yake mwenyewe wakimgusa moto utawaka na kamwe hawataweza kuuzima wao kama chadema ndiyo maana chadema wako kimya kwa shibuda.

Hakuna aliye na akili timamu anayehangaika na John Shibuda, he is ignored totally, ndio maana hata yeye anajua hivyo hata anaona aibu kushirikiana na wenzake kwa vile amevuna alichopanda.

Wanaohangaika na Shibuda ni CCM ambao kwa lugha nyingine ni kwamba wanayarudia matapishi yao wenyewe. Kwa vile leo wanamhitaji kwa ajili ya Chadema basi Shibuda ni chanda cha dhahabu, lakini wakati alipokuwa mwiba kwa CCM walimtosa ubunge na hata alipogombea kupitia Chadema walimtikisha hadi kumtia ndani mpaka siku ya uchaguzi alikuwa mahabusu.

Shibuda hana msimamo, hana ustaarabu, hana shukrani, ni ndumila kuwili, wa kuogopwa kama ukoma. Kumbuka nyoka aliyetaka kuhatarisha uhai wake hadi akamtoroka leo anamfuata huko huko pangoni kwake.
 
Duh,hii kali! Shibuda ndiye aliipeleka Chadema Kanda ya Ziwa na kwa mikono yake mwenyewe!
 
Hakuna aliye na akili timamu anayehangaika na John Shibuda, he is ignored totally, ndio maana hata yeye anajua hivyo hata anaona aibu kushirikiana na wenzake kwa vile amevuna alichopanda.

Wanaohangaika na Shibuda ni CCM ambao kwa lugha nyingine ni kwamba wanayarudia matapishi yao wenyewe. Kwa vile leo wanamhitaji kwa ajili ya Chadema basi Shibuda ni chanda cha dhahabu, lakini wakati alipokuwa mwiba kwa CCM walimtosa ubunge na hata alipogombea kupitia Chadema walimtikisha hadi kumtia ndani mpaka siku ya uchaguzi alikuwa mahabusu.

Shibuda hana msimamo, hana ustaarabu, hana shukrani, ni ndumila kuwili, wa kuogopwa kama ukoma. Kumbuka nyoka aliyetaka kuhatarisha uhai wake hadi akamtoroka leo anamfuata huko huko pangoni kwake.
Mkuu unataka kuniambia kuwa kunampango wa shibuda kurudi tena ccm au unamaanisha nini kusema kuwa ccm wanarudia matapishi yao.
 
Mchumia tumbo huyu CHADEMA alishastukiwa siku nyingi hivyo kamwe hawezi kuitesa CHADEMA kwa lolote lile tunamuona JUHA tu!
 
Mkuu unataka kuniambia kuwa kunampango wa shibuda kurudi tena ccm au unamaanisha nini kusema kuwa ccm wanarudia matapishi yao.

Rudia kusoma tena upata nini naongelea maana ya CCM kurudia matapishi ya walichokicheua wenyewe katika uchaguzi mkuu uliopita.
 
Chadema wanajua kuwa katika msafara wa mamba kenge hawakosekani. Kuna siku na saa ya kumtupa nje na bado haijawadia. Hakuna haraka mradi tu hahatarishi uhai wa chama!!
 
Katika watu niliowasahau kuwa wapo ndani ya Chadema ni Shibuda.!!!
 
Katika watu niliowasahau kuwa wapo ndani ya Chadema ni Shibuda, afadhali mleta mada uminikumbusha kuwa yupo.!!!
 
Mkuu unataka kuniambia kuwa kunampango wa shibuda kurudi tena ccm au unamaanisha nini kusema kuwa ccm wanarudia matapishi yao.
Kwani shibuda alishatoka ccm lini?!! Wenye akili zetu tunajua kwamba bado ni mwana ccm aliyepelekwa CDM kwa kazi maalum ambayo nayo alistukiwa mapema akashindwa kuitekeleza.
 
Kunatarifa za chini chini zinabainisha kuwa shibuda anaendelea kuitesa chadema kutokana na kukataa kufuata aina ya siasa wanazotaka chadema,

shibuda amekuwa na msimamo wake binafsi kisiasa kwa kukataa kutumika na chadema na kujikita kuwatumikia watu waliomchagua,

Shibuda amekuwa na mfumo wa kukataa kususia vikao vya bunge kama chadema wanavyotaka na kuendelea kuwatumikia watu waliomchagua,

shibuda pia amekuwa hakubaliani na msimamo wa viongozi wakumtaka ambatane na wenzake kwenye mandamano ya chadema kitu ambacho kinawakela sana viongozi wake,

Baada ya mijadala mirefu ndani ya chadema wengine wakitaka shibuda afukuzwe na wengine wakitaka apuuzwe lakini wapo waliodai pia kuwa shibuda anaonewa kwa sababu ya usukuma wake kama alivyowahi kusema yeye mwenyewe,

Lakini pia wapo waliowaonya chadema kuwa kama shibuda watamgusa anauwezo wa kuiua chadema kanda ya ziwa kwa mikono yake mwenyewe kwa vile yeye ndiye aliipereka kwa mikono yake mwenyewe wakimgusa moto utawaka na kamwe hawataweza kuuzima wao kama chadema ndiyo maana chadema wako kimya kwa shibuda.

rais mpya ninaomba ufahamu kila kiti cha ubunge kwenye chama chochote ni muhimu sana especially vyama ambavyo bado vinajijenga. utambue vyama kama CAHADEMA kina upinzani mkubwa na wakila aina! kwa mantiki hii ndiyo maana huyu jamaa anaachwa aendelee na aweze kujifunza! Lakini kumbuka kuwa CHADEMA ni chama ambacho kinaweza kuachana naye na bado kikaendelea kuishi! huyu jamaa ana matatizo kwani hata ndugu zake CCM wanayajua hata yeye anajua mwenyewe. kwa hiyo swala la shibuda haliwezi kukinyima CHADEMA usingizi hata kidogo! hebu nisijilizishe kuwa wewe ni mwana LUMUMBA!
 
Shibuda anajimaliza yeye mwenyewe kwani amebainika ni mtu wa aina gani Chadema hawezi kupoteza muda kumjadili.
 
Shibuda anaitesa chadema au anateseka mwenyewe. Kuna lipi alilonalo la kuitesa CDM. HUYO NDIO MWISHO WAKE UMEFIKA TAYARI.
Tena yaweza kuwa ccm walimtuma ila kashindwa kutimiza alichotumwa. Aliekuwa anaua vyama alikuwa mrema, kwa sasa haaminiwi tena hata na familia yake kuhusu siasa, ilikuwa lazima ccm watafute mrithi na bado watakuja wengine. Kwangu mimi ni CDM kuwa makini na baadhi ya wanachama,wabunge na viongozi basi, ili waonekane tu wenyewe kuwa ni mapandikizi.
 
Back
Top Bottom