Nyenyere
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 14,769
- 10,645
Hivi kuna chama katika Tanzania kinachoitwa kwa jina hili?Chama cha ADA -TADEA kimempitisha John Shibuda kuwa mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kupata kura 120 kati ya kura 130 zilizopigwa na wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho huku mgombea mwenzake Mastadia Hilari akiambulia kura 10
Aidha, Chama hicho kimechangua Juma Ali Khatib kuwa mgombea wa urais kwa upande wa Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu
Shibuda ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa amesema akishinda Urais atahakikisha anaweka usawa kwa wananchi ikiwemo kuendesha shighuli za kisiasa pasipo kuweka upendeleo kwa yeyote