John Pombe Magufuli ni pandikizi la CHADEMA?

Uswe

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
2,204
626
Waziri John Pombe Maguli, tofauti kabisa na ilivo kawaida ya mawaziri wengine wa CCM, anaonekana ni mtu makini, anayezingatia utawala wa sheria, asiyechanganya siasa na kazi na mtu mwenye kujali maslahi ya umma kuliko maslahi ya mafisadi wachache

.
Inawezekana John Pombe Magufuli akawa ni pandikizi la chandema ndani ya ccm?
 
Sio pandikizi la Chadema ila ni mchapa kazi asiyependa kunufaisha wachache. Hongera sana Magufuli na Chadema ni chama ambacho kinazingatia maendeleo ya nchi
 
Kwa mda mrefu sana mimi nimeamini kwamba Magufuli ni pandikizi la CDM. Hii imethibitika wiki iliyopita pale waziri mkuu alipompinga wazi wazi. Sababu hasa ya kumpinga mbele za watu ni kuonesha kwamba huyupo katika kundi lao. Nafurahi sana kuona CDM tayari imeshapata mapandikizi.
 
Nyote hamumfahamu vizuri Siwakuwa pandikizi chadema,kwani chadema wana historia naye kwa mgombea wa chato!!
 
Thanks again kuiinua CHADEMA,Yes Magufuli ni mwanachadema damu! na tunamtayarisha kuivunja CCM, utagundua kipindi cha kugombea urais 2015. (utopia)
 
nina amini kabisa kuwa mh pombe ni mmoja wa awatu makini waliopo ndani ya ccm.
la msingi ni walio ndani ya ccm kuwaondoa wote waliochafuka ili mfumo uwe kwa ajili ya kuleta maendeleo ya wananchi
 
Magufuli alikuwa mchapakazi hodari tangu enzi za mkapa wakati chadema bado haijaonekana kwenye ramani ya siasa za tanzania nakumbuka mkapa aliwahi kutamka waziwazi kwamba katika mawaziri wake wote magufuli alikuwa mchapa kazi hodari na akampa mlinzi wa kumlinda (bodyguard). Ina maana wakati ule magufuli alikuwa pandikizi la NCCR MAGEUZ!
 
Tukumbuke kuna vyama vya siasa na kuna wanasiasa, haimaanishi kuwa kwa sababu chama cha CCM kimeshikwa na wanasiasa MAFISADI basi miongoni mwa wanasiasa/wanachama wa CCM hakuna wachapakazi au watu safi. Ni MAGUFULI huyuhuyu alisimama kidete kuhusu kuuzwa kwa jumba za serikali na baadhi ya nyumba anatuhumiwa kuchakachua uuzaji wake watu wote walimshambulia hata wasio safi mfano. ROSTAM kupitia gazeti lake la RAI walibeba Bango sana kuhusu kashfa hiyo sababu si mwanamtandao wenzao. Leo karudi tena kwenye CHAT, CDM mnaanza kudai ni member wenu mmempandikiza CCM je alipochakachua kuhusu mijengo ya UMMA mbona hatukuwasikia kusema ni Pandikizi lenu ndani ya CCM?
Tabia hii ya CDM kukimbilia majina makubwa (wanasiasa) inaanza kuwatafuna bila wao kuelewa oneni mlivyo mkumbatia MABERE MARANDO bingwa wa kutetea MAFISADI mahakamani ktk kesi wanazo shtakiwa kwa UFISADI wa Rasilimali za UMMA. Pia mmembeba SHIBUDA ambaye kwenye nyeupe anasema nyeupe na nyeusi anasema nyeusi mnaanza kumuona MZIGO. Sasa MAGUFULI anarudi kwenye kiwango chake mnadai PANDIKIZI lenu. Kweli siasa ni mchezo wa karata tatu.
Tukumbuke CCM,CUF,CDM,NCCR,TLP,NLD,NRA,UMD,UPDP,JAHAZI ASILIA vyote ni vyama vya siasa ambavyo ndani yake kuna wanasiasa, wanasiasa hao wamo wasafi na wachafu, wazalendo na Mafisadi. Hivyo Tusizame katika kushabikia vyama kama vile vinaongozwa na MALAIKA tukummbuke vyama vyote vinaongozwa na wanasiasa hivyo ni jukumu letu kuwapima na kuamua nani anatufaa kuwa kiongozi wetu
 
Haiwezekani. Sawa sawa Uswe?

sasa mbona utendaji kazi wake unakinzana kabisa na msimamo wa CCM? unakumbuka ile issue ya samaki? unaona jinsi anavosimamia sheria huyu bwana? mi napata taabu kuamini huyu jamaa ni CCM
 
What is Good is always Good, hakuna cha upandikizi hapo ni uchapakazi wake tu hata ndani ya CDM mnayotaja kuna wasio na uzalendo kama walivyo kwa CCM, kinachotakiwa ni wananchi kuwatambua na kuwamwaga wakati wa uchaguzi 2015 bila kujali itikadi. Kama mtu wa Chadema, CUF au NCCR hafai usimpe kura kwasababu unataka wapinzani waongoze au kwasababu mtu ni wa CCM chama chako ushakula posho na Tshirt na Kofia umebeba unapiga kura halafu unaanza kujutia. Tulia, tafakari chukua hatua.
 
Waziri John Pombe Maguli, tofauti kabisa na ilivo kawaida ya mawaziri wengine wa CCM, anaonekana ni mtu makini, anayezingatia utawala wa sheria, asiyechanganya siasa na kazi na mtu mwenye kujali maslahi ya umma kuliko maslahi ya mafisadi wachache

.
Inawezekana John Pombe Magufuli akawa ni pandikizi la chandema ndani ya ccm?

Inaonekana wewe ndie pandikizi la mafisadi na unajaribu kufanya kazi uliyotumwa hapa jamvini.

Ciao,

Tiba
 
Uswe uswe uswe..........kwangu mimi binafsi sioni kama hizo sifa anazo magufuli peke yake na tujifunze sana siasa za tanzania na msione Raila Odinga ni njinga alipokuja hapa tz baada ya kushindwa uchaguzi,na kabla Jacob Zuma hajapata uraisi alikuja hapa pia kwa muda wa siku chache,leo hii Museven anajitapa kama a good product of tanzania,tusijifanye hatumjui Milton Obote alitokea wapi,Joachim Chisano na Samora Mashel hatuwakumbuki?Laurent Kabila na mwanae je hatujala nao mihogo ya kukaanga hapa tz?...orodha ni ndefu sana CCM huwa wanacheza na hii jamii yetu jinga kwa kututafutia mtu ambaye anakubalika sana lakini matokea yake ni haya ya kaka yetu JK yuleee anaondoka na uchumi wetu...tujifunze kujua tatizo siyo mtu ...tatizo hapa ni chama chenye wazuri wachache na wabaya wengi.

kauli ya kingunge; wakati wote chama chetu kinanatafuta mgombea atakayekifanya chama kijinadi kupitia yeye...do we remember him what he said?


usafi wa mwili si usafi wa roho hata mnikate kichwa.....because I was born so, do not expect I will leave it to you.
 
Ccm humchakachuaga kila mara , toka enzi za Nkapa hadi baby face Pinda
 
Waziri John Pombe Maguli, tofauti kabisa na ilivo kawaida ya mawaziri wengine wa CCM, anaonekana ni mtu makini, anayezingatia utawala wa sheria, asiyechanganya siasa na kazi na mtu mwenye kujali maslahi ya umma kuliko maslahi ya mafisadi wachache

.
Inawezekana John Pombe Magufuli akawa ni pandikizi la chandema ndani ya ccm?

Pombe Hafai Kuwa Hata Katibu Kata Kwani ni Muhasherati Kupindukia.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom