Haya mambo ya umakini, uadilifu, ufisadi sio mambo ya IMANI. Angalia barabara nyingi alizosimamia je ziko vizuri? zinakaa kipindi kilichokusudiwa kabla ya kuanza kuharibika? Je manunuzi ya wizara anayoisimamia hayana mashaka? Vivuko, boti za kasi nakadhalika zina thamani halisi ya fedha iliyolipwa? Je anachukua maamuzi sahihi kwa wakati muafaka yasiyoingizia taifa hasara? (hapa unaweza tafakari samaki wa magufuli), Je anasimama kidete kupinga sera sizizo na maslahi mapana ya nchi kama kuuza nyumba za watumishi wa serikali kisha watumishi hao hao kukaa hotelini? Je hana papara katika kuamua, akizungukwa na watu wanaomshangilia anamudu huo umaarufu au atafanya vioja? Ukipata majibu ya maswali kama haya waweza sasa kusema huyu ni mtu makini ndani ya chama. SI SWALA LA KUWA NA IMANI JUU YA UMAKINI WAKE.nina amini kabisa kuwa mh pombe ni mmoja wa awatu makini waliopo ndani ya ccm.
la msingi ni walio ndani ya ccm kuwaondoa wote waliochafuka ili mfumo uwe kwa ajili ya kuleta maendeleo ya wananchi