daud magigo
JF-Expert Member
- Sep 5, 2014
- 979
- 423
Huku siku zina zidi kuyoyoma wananchi wa kata ya Kitangiri wamezidi kuonyesha imani yao kubwa kwa mgombea udiwani kata ya Kitangiri wilayani Ilemela.Wakiwa wamechoshwa na siasa za ubabe na maamuzi yasiyowashirikisha wananchi,Mwita(HILL SIDE) anazidi kuaminiwa na wananchi wengi baada ya diwani aliyepita kushindwa kuleta mabadiliko na matumaini aliyoahidi.HILL SIDE ambaye anagombea kwa tiketi ya UKAWA ameonekana kuungwa mkono na kundi na akina Mama na Vijana ambao wamekuwa wahanga wa siasa za Diwani aliyepita.Diwani aliyepita aliahidi kupeleke usafiri hadi Mihama Ziwani kitu ambacho alishindwa licha ya kuwa Meya wa Ilemela.Pia vijana aliahidi kuaanzishia miradi mbalimbali ya kukidhi maisha yao kitu ambacho ameshindwa.