The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,186
- 4,938
"Tulishauri kuwa chama (CHADEMA) kiende kikasaini kanuni za maadili na tume ya taifa ya uchaguzi ambayo yalikuwa yanasainiwa tarehe 12 Aprili 2025. Ushauri wetu tuliotoa chama hakikuzingatia hata kidogo, na ilipofika tarehe 12 hawakwenda kusaini. Lakini vilevile tunapenda kuchukua fursa hii kuwashukuru na kuwapongeza viongozi wa dini ambao wameona umuhimu wa kufanyika kwa reforms, na wote wameunga mkono msimamo wetu wa G55 na ushauri wetu kwa chama, hakuna kiongozi wa dini aliyesema kwamba tukazuie uchaguzi. "
"Wote wamehimiza waumini wao kwamba waende wakashiriki uchaguzi lakini uchaguzi uwe huru, wa haki na wa amani, kwahiyo mahubiri yote ya Pasaka yameendana na tahadhari tuliyoitoa kwa chama kwamba tunaona hatari ya kupoteza kundi muhimu kama tukiendelea na msimamo kwamba tunakwenda kuzuia uchaguzi, na viongozi wa dini wameungana na G55 kwamba wanaunga mkono mageuzi lakini wanataka watu wakashiriki uchaguzi"- Mrema.
John Mrema kwa niaba ya wafuasi wenzake wa Kundi la G55 ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akizungumza na waandishi wa habari siku ya Jumanne Aprili 22, 2025 mkoani Dar es Salaam juu ya yanayoendelea kufanywa na chama hicho hasa suala zima la kutoshiriki uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025.
"Wote wamehimiza waumini wao kwamba waende wakashiriki uchaguzi lakini uchaguzi uwe huru, wa haki na wa amani, kwahiyo mahubiri yote ya Pasaka yameendana na tahadhari tuliyoitoa kwa chama kwamba tunaona hatari ya kupoteza kundi muhimu kama tukiendelea na msimamo kwamba tunakwenda kuzuia uchaguzi, na viongozi wa dini wameungana na G55 kwamba wanaunga mkono mageuzi lakini wanataka watu wakashiriki uchaguzi"- Mrema.
John Mrema kwa niaba ya wafuasi wenzake wa Kundi la G55 ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akizungumza na waandishi wa habari siku ya Jumanne Aprili 22, 2025 mkoani Dar es Salaam juu ya yanayoendelea kufanywa na chama hicho hasa suala zima la kutoshiriki uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025.